Bornvilla
JF-Expert Member
- Feb 17, 2011
- 924
- 271
Mh! Kweli sikuu ni siku ya kumuasi Muumba? Jana na leo amri ile ya sita inabanjuliwa tu! Tena wengine hadharani,kwenye magari na sasa guest house vyumba vimejaa. Huu uchafu unaofanyika kweli majanga yatatuacha? Kweli dhambi si kuzini peke yake lakini hii humshushia mtu hadhi yake. Kwa vile hakuna dini inaruhusu uchafu huu jamani kwa pamoja hebu tulikemee hili kwa nguvu ya pamoja! Kwa wale washiriki wa uchafu hivi hawajiulizi,mfano km dada yako,mtoto wako au mama yako akifanyiwa we unajisikiaje? Kama utajiskia vibaya,basi wengine nao wanajiskia vibaya jamaa au ndugu zao wanapofanyiwa uchafu. Sio kwenye sikukuu tu,hili limeshakuwa janga tulizuie,tukipinga kwa pamoja huenda tukafaulu.