Nikiwa nimejiunga UDSM mwaka huu kwa ajili ya kuongeza Elimu toka nimeingia hapa mtu ukibanwa na haja inabidi ujifikirie mara mbili ama uende porini (Hasa Pori lile la Kuelekea Changanyikeni au ukimbilie Mlimani City.
Jana nilibanwa na haja kubwa kila choo ninachokwenda kimejaa/kuziba. Nilianza kule COET, kisha nikaja Botany, Maktaba, SRs, Mathematics, Physics vyote vimeziba/kujaa hivyo huwezi kukitumia.
Ninachojiuliza; Je, Uongozi wa Chuo Kikuu unaliona hili? Jumla ya wanafunzi zaidi ya 15,000 mlionao na hivi vyoo kujaa hamuoni ni hatari? Mnataka tujisaidie porini mpaka lini?
Bora sisi wanaume tunaweza kujistiri huko porini zaidi nawaonea huruma kina dada. Na hali zao si rahisi kusathimili MAPORINI kama sisi.
Jana nilibanwa na haja kubwa kila choo ninachokwenda kimejaa/kuziba. Nilianza kule COET, kisha nikaja Botany, Maktaba, SRs, Mathematics, Physics vyote vimeziba/kujaa hivyo huwezi kukitumia.
Ninachojiuliza; Je, Uongozi wa Chuo Kikuu unaliona hili? Jumla ya wanafunzi zaidi ya 15,000 mlionao na hivi vyoo kujaa hamuoni ni hatari? Mnataka tujisaidie porini mpaka lini?
Bora sisi wanaume tunaweza kujistiri huko porini zaidi nawaonea huruma kina dada. Na hali zao si rahisi kusathimili MAPORINI kama sisi.