kifupi kirefu
JF-Expert Member
- Oct 29, 2018
- 539
- 3,507
Media zetu zina kazi kubwa sana safari hii, wakati mapingamizi yaliyowekwa na wakasomewa content na context ya hayo mapingamizi walirekodi na wakawa wanafurahi jinsi hoja zilivyopangwa
Baada ya kurekodi na kuandika, hakuna chombo chochote kilichoripoti Kama habari kubwa kuwa Lipumba na Mzee wamewekewa pingamizi, vilikaa na habari zao kwenye flash hivyo walaji wa habari zao hawakujua kama Kuna mapingamizi.
Baadaye jioni au usiku Mkurugenzi wa uchaguzi akatoka majibu ya pingamizi, wakaenda kumsikiliza na kuandika alichowaambia Ni matokeo. Kwa amasa kubwa wakapost na kuripoti kwa nguvu zote ushindi waliopata waliowekewa pingamizi ngazi ya Urais.
Bila kujua madhara ya dhuluma, wakajikuta wamelazimika kuwahabarisha wananchi kuwa Tundu Lisu aliweka pingamizi ...na Sasa wananchi wakajua nini kinachoendelea. Lakini pia wakawahabarisha wananchi kuhusu mapingamizi hayo ila tu hawajawahabarisha msingi wa mapingamizi kwa sababu tume haijaweka wazi msingi wa mapingamizi na haijaeleza vifungu vilivyoelezwa kuvunjwa au kukiukwa na mweka mapingamizi.
Kwa aina hii ya vyombo vya habari, kwa aina hii ya waandishi na kwa aina hii ya wamiliki na wahariri...wanadhani wanayo haja kweli ya kwenda na flash na makamera yao kwa wagombea wa upinzani? Kwa Nini wasikae hizo gharama za mafuta na uendeshaji wakafanyia kazi nyingine?
Kitu ambacho kinaendelea na ambacho kimesambaa kwa kasi, Ni clip ya Tundu Lisu inayosambazwa na maasimu wa ccm bila kusambazwa clip yoyote ya hoja kinzani Jambo linalowafanya watu waamini kwa 100% aliyosema Tundu lisu Ni ya kweli kwa msingi wa kisheria.
Kitendo cha media kuacha kurusha hizi habari kinawanyima pia haki yakwenda kuomba ufafanuzi kwa wasomi wengine maana ili uweke mdahalo kuhusu hoja za Lisu lazima pia urushe kile alichokisema hasa tumekuwa tunamjenga kwa kasi kubwa na habari zake kusambaa kwa kasi kubwa kuliko zinavyosambaa habari za hao wengine.
Kwa mtu anayewaza kimkakati akipewa kazi ya kushauri kuhusu huu utaratibu ATAWAAMBIA MNACHOFANYA NI NIKUMPA POPULARITY LISU na kuwaminya wengine wasisikike kwa wanannchi
Baada ya kurekodi na kuandika, hakuna chombo chochote kilichoripoti Kama habari kubwa kuwa Lipumba na Mzee wamewekewa pingamizi, vilikaa na habari zao kwenye flash hivyo walaji wa habari zao hawakujua kama Kuna mapingamizi.
Baadaye jioni au usiku Mkurugenzi wa uchaguzi akatoka majibu ya pingamizi, wakaenda kumsikiliza na kuandika alichowaambia Ni matokeo. Kwa amasa kubwa wakapost na kuripoti kwa nguvu zote ushindi waliopata waliowekewa pingamizi ngazi ya Urais.
Bila kujua madhara ya dhuluma, wakajikuta wamelazimika kuwahabarisha wananchi kuwa Tundu Lisu aliweka pingamizi ...na Sasa wananchi wakajua nini kinachoendelea. Lakini pia wakawahabarisha wananchi kuhusu mapingamizi hayo ila tu hawajawahabarisha msingi wa mapingamizi kwa sababu tume haijaweka wazi msingi wa mapingamizi na haijaeleza vifungu vilivyoelezwa kuvunjwa au kukiukwa na mweka mapingamizi.
Kwa aina hii ya vyombo vya habari, kwa aina hii ya waandishi na kwa aina hii ya wamiliki na wahariri...wanadhani wanayo haja kweli ya kwenda na flash na makamera yao kwa wagombea wa upinzani? Kwa Nini wasikae hizo gharama za mafuta na uendeshaji wakafanyia kazi nyingine?
Kitu ambacho kinaendelea na ambacho kimesambaa kwa kasi, Ni clip ya Tundu Lisu inayosambazwa na maasimu wa ccm bila kusambazwa clip yoyote ya hoja kinzani Jambo linalowafanya watu waamini kwa 100% aliyosema Tundu lisu Ni ya kweli kwa msingi wa kisheria.
Kitendo cha media kuacha kurusha hizi habari kinawanyima pia haki yakwenda kuomba ufafanuzi kwa wasomi wengine maana ili uweke mdahalo kuhusu hoja za Lisu lazima pia urushe kile alichokisema hasa tumekuwa tunamjenga kwa kasi kubwa na habari zake kusambaa kwa kasi kubwa kuliko zinavyosambaa habari za hao wengine.
Kwa mtu anayewaza kimkakati akipewa kazi ya kushauri kuhusu huu utaratibu ATAWAAMBIA MNACHOFANYA NI NIKUMPA POPULARITY LISU na kuwaminya wengine wasisikike kwa wanannchi