Mwana Wa Maryam
Member
- Oct 22, 2007
- 64
- 2
Mwana wa Marium,
Sasa wewe unaona ni bora kwa taifa changa kuanza kuangalia namna ya kuwa na idadi ndogo za watu? No- and big no! Tunahitaji watoto- nadhani sehemu zingine Tz ni pori tu kwa kuwa watu ni wachache sana! Tz tuna vyanzo vingi vya maji hata kuliko Nigeria- angalia mito na maziwa kila mahali!
Your definition of usomi- is intersting! Well taabu yangu na wasomi kama ulivyosema huchelewa sana kuolewa/kuoa wakati wanasoma. Ila kumbuka pia hata akiolewa na miaka 27 bado mwanamke msomi Tz atazaa only 2 childern! Hili ndo kwangu ni issue. Hata mwanamme msomi at 30 anaoa mwal. at 24 wanazaa tu watoto wawili!
Yet wamachinga ndo tunawacha wanazaa watoto wengi- it is my view that kwa kufanya hivi we dont do justice for the welfare of future of our nation!
MzalendoHalisi:
Kizazi kinachokuja kinategemea zaidi misingi ya maisha utakayo waachia kuliko idadi yao. Vile-vile mapori unayoyaona wewe si mapori yaliokaa bure. Na utakuwa hutoi hukumu nzuri kwa kizazi kijacho, iwapo utataka idadi iongezeke kwa sababu kuna mapori.
Mapori yaliopo sasa ni kiini cha ENEGY ya sehemu kubwa wananchi wa Tanzania. Mapishi ya chakula Tanzania yanategemea sana mapori ambayo wewe unaona yanakaa bure. Miaka 20 iliyopita, kuni zilikuwa zinapatikana katika umbali wa mita 100 lakini sasa zaidi ya kilometa 2.
Vile vile mapori hayo ni yanategemewa na wanyama na wafugaji. Na vile vile ni vyanzo vya mito tuliyonayo. Na unanitia mashaka na wasiwasi mkubwa kutoelewa mchango wa mapori yetu. Machafuko kama ya Darfur chanzo chake ni ukosefu wa mapori.
Kinachoweza kuturudisha nyuma sana sio wasomi kuwa na watoto wachache bali ni kuwa na uwezo wa kuwapa watoto wao elimu ya kutosha kupambana na maisha ya kisasa. Na wamachinga kuwa na watoto wengi wasio na elimu. Na hali hiyo inajionyesha sasa na wala hakuna sababu ya kusubiri vizazi vinavyokuja. Machafuko ya kitabaka yanaweza kutokea.
Na vilevile siungi mkono sera za uzazi wa majira. Sera hizo hazina manufaa iwapo milango ya kazi na elimu itaendelea kuwa umefungwa kama sasa. Toka tumepata uhuru tunaendesha nchi kama jeshi. Jeshini unakuwa na makamanda wachache na wapiganaji wengi. Mawazo ya Nyerere na viongozi wengine yalikuwa kuwa na wasomi wachache na kundi kubwa la wenye elimu ya msingi linalopokea amri. Kosa la wasomi wa Tanzania ni kutaka kuendelea kuwa makamanda na wengine wapiganaji (wamachinga).