Vyeti vya uraia na yaliyonikuta - a true story

Haya ya wajumbe kutojulikana ndio nasikia na wewe. Na nafikiri usiyeelewa hapa ni wewe na huyu mwenzio unayezidi kumpotosha. Chain ya utambuzi huanzia kwa hao unaosema hawajulikani. Kwa mfano, kama umeambiwa upate barua ya dhamana ya Afisa Mtendaji wa Kata, itakulazimu kufuata hatua zifuatazo:1. Uende kwa mjumbe wa nyumba kumi akuandikie barua ya utambulisho. Afisa Mtendaji wa mtaa atahitaji ushahidi toka kwa mjumbe wako kuwa anakufahamu. (Nikukumbushe kuwa Afisa Mtendaji wa Mtaa na Kata ni waajiriwa wa Serikali kuu na wanaweza wakawa si wakazi wa eneo husika)2. Baada ya Afisa Mtendaji wa Mtaa wako kuridhika (baada ya kupata uthibitisho wa mjumbe wa nyumba kumi) atakupa barua ya kukutambulisha kwa Afisa Mtendaji wa Kata kuwa umetokea kwenye mtaa wake. Na yeye ndio atakusikiliza.Nitashangaa sana kama Afisa Mtendaji wa Mtaa au Kata atakuandikia barua ilhali hajui unakaa nyumba gani wala uchochoro gani. Hebu tutumie akili zetu vizuri wakuu
Kitaifa,-- Serikali inaanzia kwa mwenyekiti wa Serikali ya mtaa, Afisa Mtendaji Hawezi kukusaidia lolote kama hautakuwa na utambulisho wa mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa unaoishi, Na mwenyekiti wa serikali ya MTaa pia hawezi kukusaidia kama hautakuwa na Barua ya Mjumbe wa Nyumba Kumi........................, Utaratibu ndio ulivyo, Ile barua ya Mjumbe wa nYumba kumi inaishia Kwa mwenyekiti wa serikali ya Mtaa, na Barua ya Mwenyekiti wa Seriklai ya Mtaa inaishia kwa Afisa Mtendaji, na Barua ya Afisa Mtendaji ndio inayoingia kwenye Maofisi yote na ndio Barua rasmi ya kiserikali inayokutambulisha ..............................Kama mambo ya Kimahakama, Uhamiaji, nk
 
Las Mas Bobos

Mmh ualimu mgumu,ujumbe mzuri lkn lugha iliyotumika naona kama inaweza kumkatisha tamaa mwanafunzi anayejifunza
 
Last edited by a moderator:
KUmbe mko wengi!

Hivi kwa akili tu ya kawaida, mwenyekiti wa serikali ya mtaa anaweza kuwatambua wakaaazi woooote wa mtaa wake?
umetoa majibu mazuri tu hapo juu, nnachotaka kusema ni kua hata hao makarani hawana uwezo mzuri wa kuwaelimisha watu, mi nafikiri kama Tiba angepata majibu kama uliotoas hapo hata asinge kuja kulalamika hapa. Wengi wao hawana uelewa mzuri wa zoezi hili
 
KUmbe mko wengi!

Hivi kwa akili tu ya kawaida, mwenyekiti wa serikali ya mtaa anaweza kuwatambua wakaaazi woooote wa mtaa wake?
kama tunadhani wajumbe wa nyumba 10 ni muhimu basi waajiriwe kama wale watendaji wa mitaa na wasifungamane na chama chochote cha siasa, unadhani kila chama kikiwa na mjumbe wa nyumba 10 itakuwaje huu ni uhuni kulazimisha watu waje na barua ya mjumbe wa nyumba 10 na kama ikitokea hamuivi kiitikadi unadhani atakuhudumia ipasavyo?
 
Content ya post ni tarehe au ukiritimba wa mwenyekiti wa mtaa? Anyway mwenye post atakuwa amenote!

My apology, tayari nimerekebisha hiyo tarehe. Inapashwa isomeke 31 July 2012.

Tiba
 
Mi ninavyojua...kuna watu walikuwa wakipita kila nyumba kuandikisha majina...sasa kama ulikuwapo kwenye ilw list then huna haja ya barua we ni kwenda tu direct ukajaze form...Ila kama hukuandikwa kipindi kile then inabidi uende kwa mjumbe wako(sijui wa nyumba 10 ama mtaa) halafu yeye atakupa barua ambayo inabidi uipeleke katika serikali ya mtaa...then kule unaandikishwa tena kwenye lile daftari. Baada ya hapo sasa unachukua zile copies zako unaelekea shule ya msingi...huko ambako wewe Tiba uliletewa zengwe...huko ndio unakojiandikisha.

Mkuu wengine hatushindi ndani kusubiri kuja kuandikishwa. Kama kweli balzo wa CCM anahusishwa na hili zoezi kama unavyothibitisha wewe, then tuna tatizo kubwa sana hapa. Ukiritimba wa chama kimoja bado hatujaachana nao.

Tiba
 
Inawezekana kabisa mdada haelewi tofauti kati ya balozi wa CCM na Mwenyekiti wa Serikali za Mitaa.

Kaona umemletea ujuaji ofisini kwake, kaamua kukuletea ngumu tu kwa kuwa hataki ku lose face.

Nishakutana nazo sana hizi bongo. Mtu yuko ofisini kwake, hajui kazi, ukimuuliza maswali sana na kuonekana unaelewa issues kuliko yeye anakuwekea ngumu tu.

Hakieleweki mpaka barua ya Balozi wa CCM.

Mtu yuko ofisini kwake.

Noma.

Mkuu hii ni hatari sana. Kwa nini tuulizwe barua za balozi wa CCM? Mbona kwenye matangazo yao hilo hawalisemi?

Tiba
 
Mkuu Tiba mie naona tatizo liko kwako, kabla ya zoezi la kujaza fomu, hawa makarani walipita nyumba hadi nyumba wakiandika majina ya wakaazi wakiwa na huyo mjumbe wa ccm. Iwapo kwako walipita na labda hukuwapa ushirikiano basi ndio haya yalikukuta.

Mkuu, walipita siku gani? Mimi sikai nyumbani kusubiri kuandikishwa ndugu yangu, nina mihangaiko kibao hapa mjini. Nikitoka saa 12 asubuhi narudi wakati mwingine usiku mwingi.

Tiba
 
Mdau Tiba kuna tatizo kubwa sana Dar kuhusu namna mfumo wa serikali unavyofanya kazi tangu mwaka 1992 nchi ilipoingia kwenye vyama vingi. Dar watu wengi including watumishi wa taasisi mbalimbali hawajui namna mfumo wa serikali ya mtaa na serikali kuu inavyofanya kazi japokuwa ni kitovu cha nchi na ndio maana utakuta mabalozi wa nyumba kumi au wajumbe wanakuwa wana sauti wakati kwenye mfumo wa serikali hawajulikani na wakati mwingine unaweza kwenda na barua ya mtendaji wa kata ukaambiwa leta barua ya mujumbe badala ya mwenyekiti wa mtaa au mtendaji wa mtaa ambao wanatambulika kisheria. Huwa tunawasingizia watu wa vijijini sijui elimu itolewe kwao lakini kiukweli ukienda kijijini haya hata kama kipo Itabagumba, Kebanchbancha, Imalamakoye au Ubenanzomonzi wanajua kabisa kwamba anaetakiwa ku-verify taarifa ni mtendaji wa kijiji au kata but reference inatoka kwa mwenyekiti wa kitongoji but kwa mjini ni mtendaji wa mtaa kama yupo japo miji mingi huwa hawapo au mwenyekiti wa mtaa ambae ataverify ila kuipa nguvu unakwenda kwa mtendaji wa kata ambae anamwakilisha mkuruguenzi wa manispaa. Pole sana haya ndio matatizo yaliyopo Dar wajumbe na mabalozi wana nguvu kama nini mpaka kwenye kuuziana ardhi (somo halijafika kwa watu wengi tangu 1992 tulipoingia vyama vingi wakati vijijini wao hawana shida na hili)

Ndugu yangu nimekuelewa. Ni kweli tuna tatizo hapa. Lakini yule binti nilimwomba aniruhusu nimletee barua kutoka kwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa akakataa kwamba yeye anataka ya balozi wakati balozi kwa watendaji wa serikali yeye hayumo. Na kwa mfumo wa vyama vingi kila chama kina mfumo wake wa utendaji na mabalozi wanatumiwa na CCM. Mimi sina uhusiano wowote na huyo balozi wa CCM kwani mara nyingi nimempigia kelele kwa upumbavu wake anaoufanya mtaani.

Hili serikali haipashwi kukaa na kulifumbia macho hata kidogo.


Tiba
 
Haya ya wajumbe kutojulikana ndio nasikia na wewe. Na nafikiri usiyeelewa hapa ni wewe na huyu mwenzio unayezidi kumpotosha. Chain ya utambuzi huanzia kwa hao unaosema hawajulikani. Kwa mfano, kama umeambiwa upate barua ya dhamana ya Afisa Mtendaji wa Kata, itakulazimu kufuata hatua zifuatazo:
1. Uende kwa mjumbe wa nyumba kumi akuandikie barua ya utambulisho. Afisa Mtendaji wa mtaa atahitaji ushahidi toka kwa mjumbe wako kuwa anakufahamu. (Nikukumbushe kuwa Afisa Mtendaji wa Mtaa na Kata ni waajiriwa wa Serikali kuu na wanaweza wakawa si wakazi wa eneo husika)
2. Baada ya Afisa Mtendaji wa Mtaa wako kuridhika (baada ya kupata uthibitisho wa mjumbe wa nyumba kumi) atakupa barua ya kukutambulisha kwa Afisa Mtendaji wa Kata kuwa umetokea kwenye mtaa wake. Na yeye ndio atakusikiliza.

Nitashangaa sana kama Afisa Mtendaji wa Mtaa au Kata atakuandikia barua ilhali hajui unakaa nyumba gani wala uchochoro gani. Hebu tutumie akili zetu vizuri wakuu

Hao wajumbe na mabolozi wa nyumba kumi sikatai kwamba hawakubaliki ila katika mazingira ya watu roho safi na wasiomind vitu vidogovidogo na ndio maana serikali inatambua mpaka vyeti vya ubatizo kama kielezo. Hao viongozi ni wa kichama na si wa kiserikali na hiyo shughuli ni ya kiserikali na ndio maana mwaka 1992 tulipoingia vyama vingi kulikuwa kuna watu wanaitwa makatibu kata ambao walikuwa wanafanya kazi kama watendaji wa chama na watendaji wa serikali wakaondolewa na kuleta position ya Mtendaji wa kata ili afanye kazi za serikali bila bias watu wasiseme ni wa chama flani pia katika ngazi ya mtaa ikawekwa post ya mwenyekiti wa mtaa ambae huwa anachaguliwa na wananchi wa mtaa husika na ambae ndio mwakilishi wa rais ktk ngazi ya mtaa pia kunakuwa na afisa mtendaji wa mtaa ambae anamwakilisha mkurugenzi wa manispaa.

Mtandaji wa kata anachukua utambulisho toka kwa mtendaji wa mtaa ambae anafanya kazi kwa karibu na mwenyekiti wa mtaa ambae ni mwakilishi wa wananchi ambae anatambuliwa na sheria mpya ya serikali za mitaa na ndie anaishi na hao wananchi mtaani na anawafahamu watu wake nikiwa na maana yeye kama mwenyekiti ndio anatakiwa atumie mbinu kuhakikisha kwamba yule ni mkazi wake si mjumbe au balozi wa nyumba kumi ambao ni viongozi wa kichama ambao wanawakilisha issues zote related na siasa.

Hii imekuja baada ya nchi kuingia katika mfumo wa vyama vingi 1992 lengo ni ku-avoid bias ila kwa issue ya vitambulisho si mbaya kumtumia pia mjumbe kwa kuwa ni issue ya kitaifa. Lakini linapokuja suala kama la uchaguzi mdau wangu Las Mas Bobos hapo inakuwa kasheshe mtu anapotaka kujiandikisha kupiga kura umwambie akalete barua kwa mjumbe au balozi). Huo utaratibu unaotumika Dar ni kile kitu tunachoita mazoea hivyo imetokea utaratibu ndio huo miaka kama minne iliyopita mpaka bank ilikuwa unaambiwa uje na barua ya mjumbe.

KWA MUJIBU WA SHERIA YA SERIKALI YA MITAA, SERIKALI INAANZIA KATIKA NGAZI YA mtaa kwa mjini na NGAZI YA kitongoji kwa vijijini, hiyo issue ya mabalozi wa nyumba kumi na wajumbe tunaitumia tu kimazoea ni kama vile issue inatakiwa aifanye Mkurugenzi wa mji,jiji au manispaa mtu anakwenda kwa meya wa mji au mkuu wa wilaya.
 
Kabla ya kujaza fomu za maombi ya KITAMBULISHO, NIDA kwa kushirikiana na Serikali za Mitaa, iliandaa zoezi la utambuzi wa kaya na makazi kwa kila mtaa. Makarani wa NIDA wakiambatana na WAJUMBE WA NYUMBA KUMI walipita nyumba hadi nyumba kuwasajili wakazi kwenye DAFTARI LA WAKAZI LA MTAA. (Wajumbe wa Nyumba 10 na sio wa CCM) Nikukumbushe kuwa, wengi wa mnaojifanya mmesoma (ilhali vichwani hamna kitu) mlipuuzia zoezi hili na kuwapa wakati mgumu makarani kwa kutotoa ushirikiano kwenu. Muda uliopangwa uliisha na NIDA iliongeza siku 7 za ziada, na bado wengine mligoma kusajiliwa.
Las Mas Bobos

Mkuu umejitahidi kueleza vizuri lakini umepoteza point ulipodai wajumbe wa nyumba 10 ni watendaji wa serikali. Hii imeanza lini? Hawa wajumbe wanapatikana vipi? Nipe hayo majibu kwanza, halafu tuendelee!!!!

Tiba
 
KUmbe mko wengi!

Hivi kwa akili tu ya kawaida, mwenyekiti wa serikali ya mtaa anaweza kuwatambua wakaaazi woooote wa mtaa wake?

Kwa nini unafikiri kwamba mwenyekiti wa serikali ya mtaa hawajui wakazi wa mtaa?

Tiba
 
Naomba mtambue Balozi wako wa nyumba 10 wala usijali ametokea Chama gani kwani yeye ndio anajua km kweli mwenye Nyumba wako kakupangisha, hata km umejenga lazima umtambue balozi wako kwani kati ya nyumba 10 mojawapo ni yako na 9 zilizobaki zote anazisimamia yeye. Fika kwake tu atakapogoma ndio kamshitaki kwa Mtendaji kuwa hakutambui kwa maugomvi yenu mengine

Mkuu tatizo langu sioni kwa nini mjumbe wa CCM hausishwe kwenye hili zoezi. Kwa nini wasiombe nilete barua ya mjumbe wa Chadema?

Tiba
 
hvyo ulikua na maana gan ulipoanza kumuuliza yule dada kua anahitaji barua ya baloz wa chama gan?nina wasiwasi na wrong perception ktk maelezo yko

Mkuu unless uelewi kuwa balozi wa nyumba kumi (Mjumbe) ni ngazi ya chini ya uongozi wa CCM, si ngazi ya utawala wa serikali. Katika mazingira ya vyama vingi, kila chama kina ngazi za uongozi na mimi sioni kwa nini balozi wa CCM ndie atumike kunitambulisha mimi ambaye sina uhusiano wowote na CCM.

Mbona bado mnafikiri as if bado tuko na chama kimoja?

Tiba
 
Kitaifa,-- Serikali inaanzia kwa mwenyekiti wa Serikali ya mtaa, Afisa Mtendaji Hawezi kukusaidia lolote kama hautakuwa na utambulisho wa mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa unaoishi, Na mwenyekiti wa serikali ya MTaa pia hawezi kukusaidia kama hautakuwa na Barua ya Mjumbe wa Nyumba Kumi........................, Utaratibu ndio ulivyo, Ile barua ya Mjumbe wa nYumba kumi inaishia Kwa mwenyekiti wa serikali ya Mtaa, na Barua ya Mwenyekiti wa Seriklai ya Mtaa inaishia kwa Afisa Mtendaji, na Barua ya Afisa Mtendaji ndio inayoingia kwenye Maofisi yote na ndio Barua rasmi ya kiserikali inayokutambulisha ..............................Kama mambo ya Kimahakama, Uhamiaji, nk

Mkuu umeeleza vizuri sana. Endapo yule binti angedai nimletee barua kutoka kwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa halafu nikaenda kwake akasema hanitambui, labda nianzie kwa huyo balozi wa CCM, hilo lingekuwa suala lingine. Huyu bi mdogo yeye alichokuwa anataka ni barua kutoka kwa balozi tu!!!! Kitu ambacho bado mimi sioni kama ni sahihi hata kidogo.

Tiba
 
Mmh ualimu mgumu,ujumbe mzuri lkn lugha iliyotumika naona kama inaweza kumkatisha tamaa mwanafunzi anayejifunza

Kiukweli hakuna wajumbe wa nyumba 10 kwa system ya serikali indugu Las Mas Bobos anatupotosha na ametumia maneno makali japokuwa ametoa point nzuri ila naungana nae pale aliposema kabla ya kujiandikisha serikali ilifanya mchakato wa kuandikisha wakazi wote wa maeneo husika hivyo mtoa hoja nae kama alikuwepo angepata room ya kutambuliwa, picha niliyopata hapa baada ya mchango wa Las Mas Bobos ni kwamba mtoa mada huenda hakuwepo wakati zoezi la utambuzi linafanyika na ndio maana akakutana na kadhia hii.

Aall in all mwenyekiti wa mtaa ndie anaetambua wananchi wake na si vinginevyo ila yeye kwa kutumia mbinu zake za ziada ndio anatakiwa awatumia wajumbe wa serikali ya mtaa ambao kila mtaa au kijiji huwa ni wajumbe 25 ambao wanaunda serikali ya mtaa hivyo hakuna issue ya wajumbe 10 hapa. Si kila issue inahitaji degree hapa kuna vitu vingine ni kuelimishana tu mpaka tunafikia consensus tukileta issue za degree hapa wakati raia wengi wa Tanzania ni STD 7 maana yake hatuwezi kufikisha ujumbe uliokusudiwa effectively. NIDA wametumia approach hiyo ili wawanase watu ambao watajifanya raia ndio maana viambatanisho vipo kibao mpaka vya ubatizo wanachukua lakini si kwamba kwa kuwa wametumia approach hiyo ndio tuhalalishe kwamba ndio utaratibu.

TUNAHITAJI ELIMU YA URAIA AMBAYO NI GENERAL KWANI MTU AKIWA ANA DEGREE VITU VYOTE ANAVIJUA MPAKA Local Government adminstration.
 
Ndugu yangu nimekuelewa. Ni kweli tuna tatizo hapa. Lakini yule binti nilimwomba aniruhusu nimletee barua kutoka kwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa akakataa kwamba yeye anataka ya balozi wakati balozi kwa watendaji wa serikali yeye hayumo. Na kwa mfumo wa vyama vingi kila chama kina mfumo wake wa utendaji na mabalozi wanatumiwa na CCM. Mimi sina uhusiano wowote na huyo balozi wa CCM kwani mara nyingi nimempigia kelele kwa upumbavu wake anaoufanya mtaani.

Hili serikali haipashwi kukaa na kulifumbia macho hata kidogo.


Tiba

Ni kuelimishana tu, tatizo hili lipo mjini ambako ndio tunajifanya wajuaji ukienda vijijini huwezi kutanana hii kitu mtu anakuja na barua toka kwa mwenyekiti wa kitongoji anaipeleka kwa mtendaji anamaliza na kama mwenyekiti wa kitongoji hayupo anakwenda directly kwa mtendaji wa kijiji anamaliza kila kitu
 
Hao wajumbe na mabolozi wa nyumba kumi sikatai kwamba hawakubaliki ila katika mazingira ya watu roho safi na wasiomind vitu vidogovidogo na ndio maana serikali inatambua mpaka vyeti vya ubatizo kama kielezo. Hao viongozi ni wa kichama na si wa kiserikali na hiyo shughuli ni ya kiserikali na ndio maana mwaka 1992 tulipoingia vyama vingi kulikuwa kuna watu wanaitwa makatibu kata ambao walikuwa wanafanya kazi kama watendaji wa chama na watendaji wa serikali wakaondolewa na kuleta position ya Mtendaji wa kata ili afanye kazi za serikali bila bias watu wasiseme ni wa chama flani pia katika ngazi ya mtaa ikawekwa post ya mwenyekiti wa mtaa ambae huwa anachaguliwa na wananchi wa mtaa husika na ambae ndio mwakilishi wa rais ktk ngazi ya mtaa pia kunakuwa na afisa mtendaji wa mtaa ambae anamwakilisha mkurugenzi wa manispaa. Mtandaji wa kata anachukua utambulisho toka kwa mtendaji wa mtaa ambae anafanya kazi kwa karibu na mwenyekiti wa mtaa ambae ni mwakilishi wa wananchi ambae anatambuliwa na sheria mpya ya serikali za mitaa na ndie anaishi na hao wananchi mtaani na anawafahamu watu wake nikiwa na maana yeye kama mwenyekiti ndio anatakiwa atumie mbinu kuhakikisha kwamba yule ni mkazi wake si mjumbe au balozi wa nyumba kumi ambao ni viongozi wa kichama ambao wanawakilisha issues zote related na siasa> Hii imekuja baada ya nchi kuingia katika mfumo wa vyama vingi 1992 lengo ni ku-avoid bias ila kwa issue ya vitambulisho si mbaya kumtumia pia mjumbe kwa kuwa ni issue ya kitaifa. Lakini linapokuja suala kama la uchaguzi mdau wangu Las Mas Bobos hapo inakuwa kasheshe mtu anapotaka kujiandikisha kupiga kura umwambie akalete barua kwa mjumbe au balozi). Huo utaratibu unaotumika Dar ni kile kitu tunachoita mazoea hivyo imetokea utaratibu ndio huo miaka kama minne iliyopita mpaka bank ilikuwa unaambiwa uje na barua ya mjumbe. KWA MUJIBU WA SHERIA YA SERIKALI YA MITAA, SERIKALI INAANZIA KATIKA NGAZI YA mtaa kwa mjini na NGAZI YA kitongoji kwa vijijini, hiyo issue ya mabalozi wa nyumba kumi na wajumbe tunaitumia tu kimazoea ni kama vile issue inatakiwa aifanye Mkurugenzi wa mji,jiji au manispaa mtu anakwenda kwa meya wa mji au mkuu wa wilaya.

Mkuu nakushukuru sana kwa somo hili. Wenye masikio, nawasikie. Nimekugongea thanks!!!!

Tiba
 
Mkuu Tiba mie naona tatizo liko kwako, kabla ya zoezi la kujaza fomu, hawa makarani walipita nyumba hadi nyumba wakiandika majina ya wakaazi wakiwa na huyo mjumbe wa ccm. Iwapo kwako walipita na labda hukuwapa ushirikiano basi ndio haya yalikukuta.
Kwanini mjumbe wa ccm wakati sio zoezi la kuandikisha wanachama wa ccm.
 
Back
Top Bottom