Tiba
JF-Expert Member
- Jul 15, 2008
- 4,604
- 3,163
Wana Jamvi,
Juzi tarehe 31 July 2012 niliamua niwe mmojawapo wa raia wema kwa kuitikia mwito wa kwenda kujiandikisha. Kwa yanayotangazwa redioni na kwenye magazeti, tunapashwa kwenda kujiandikisha kwa kuonyesha kitu ambacho kinaweza kuthibitisha kwamba mimi ni raia. Nilikwenda kujiandikisha pale Ubungo Maziwa ambako mwenyekiti wetu wa mtaa anaitwa Jovin Ndimbo. Huyu jamaa anajulikana kwa kupokea rushwa na ofisi yake haiwezi kukupa huduma yoyote bila kutoa pesa.
Nilifika pale kituoni kwenye mida ya saa kumi jioni na kupanga foleni kwa karibu dakika 45 kabla zamu yangu ya kuandikishwa haijafika. Binti aliyekuwa anaandikisha pale ana umri kama wa miaka 22 hivi. Nilipofika akaniuliza barua ya balozi iko wapi? Nikamuuliza balozi yupi huyo? Akaniambia balozi wako wa nyumba kumi. Nikamuuliza balozi wa chama gani? Akaniambia balozi wa CCM. Nikamuuliza balozi wa CCM anaingilianaje na zoezi la watu kuandikishwa uraia?
Yule binti nilimuonyesha passport yangu original na vyeti vyangu vya shule vya ngazi mbali mbali lakini (nilikuwa na copy ya vitu vyote vile vile) alikataa kabisa na kusisitiza kwamba bila barua ya balozi hawezi kuniandikisha. Nilisikitika sana.
Je ni kweli barua ya balozi wa CCM ni mojawapo ya masharti ya mtu kuandikishwa uraia? Hapa balozi wa CCM wanahusikaje? Nilimwambia kama anataka barua ya mwenyekiti wa serikali ya mtaa ninaweza kumuelewa lakini balozi wa CCM hapana. Binti alikataa kuniandika na kwa kuwa sikutaka kubisha naye, niliamua kuondoka na hivyo kushindwa kujiandikisha.
Nina wasiwasi huyu Ndimbo ambaye ni mwenyekiti wa mtaa ameamua kuwashirikisha mabalozi na kuwaamrisha kupokea kitu kidogo kabla ya kutoa barua. Baadae nilitaarifiwa kwamba bila Shs. 2,000 balozi hakupi hiyo barua.
Halafu tukiichukia CCM watu wanatushangaa!!!! Je kuna mtu mwingine amekutana na hadha hii?
Tiba
Juzi tarehe 31 July 2012 niliamua niwe mmojawapo wa raia wema kwa kuitikia mwito wa kwenda kujiandikisha. Kwa yanayotangazwa redioni na kwenye magazeti, tunapashwa kwenda kujiandikisha kwa kuonyesha kitu ambacho kinaweza kuthibitisha kwamba mimi ni raia. Nilikwenda kujiandikisha pale Ubungo Maziwa ambako mwenyekiti wetu wa mtaa anaitwa Jovin Ndimbo. Huyu jamaa anajulikana kwa kupokea rushwa na ofisi yake haiwezi kukupa huduma yoyote bila kutoa pesa.
Nilifika pale kituoni kwenye mida ya saa kumi jioni na kupanga foleni kwa karibu dakika 45 kabla zamu yangu ya kuandikishwa haijafika. Binti aliyekuwa anaandikisha pale ana umri kama wa miaka 22 hivi. Nilipofika akaniuliza barua ya balozi iko wapi? Nikamuuliza balozi yupi huyo? Akaniambia balozi wako wa nyumba kumi. Nikamuuliza balozi wa chama gani? Akaniambia balozi wa CCM. Nikamuuliza balozi wa CCM anaingilianaje na zoezi la watu kuandikishwa uraia?
Yule binti nilimuonyesha passport yangu original na vyeti vyangu vya shule vya ngazi mbali mbali lakini (nilikuwa na copy ya vitu vyote vile vile) alikataa kabisa na kusisitiza kwamba bila barua ya balozi hawezi kuniandikisha. Nilisikitika sana.
Je ni kweli barua ya balozi wa CCM ni mojawapo ya masharti ya mtu kuandikishwa uraia? Hapa balozi wa CCM wanahusikaje? Nilimwambia kama anataka barua ya mwenyekiti wa serikali ya mtaa ninaweza kumuelewa lakini balozi wa CCM hapana. Binti alikataa kuniandika na kwa kuwa sikutaka kubisha naye, niliamua kuondoka na hivyo kushindwa kujiandikisha.
Nina wasiwasi huyu Ndimbo ambaye ni mwenyekiti wa mtaa ameamua kuwashirikisha mabalozi na kuwaamrisha kupokea kitu kidogo kabla ya kutoa barua. Baadae nilitaarifiwa kwamba bila Shs. 2,000 balozi hakupi hiyo barua.
Halafu tukiichukia CCM watu wanatushangaa!!!! Je kuna mtu mwingine amekutana na hadha hii?
Tiba