Vyama vya ushindani(upinzani) wahini viti bungeni kwanza..

Mtarajiwa

JF-Expert Member
Feb 29, 2008
440
11
Imekuwa kasumba kwa wapinzani kung'ang'ania kugombea nafasi ya urais wakati wa uchaguzi mkuu.Nadiriki kusema ni kung'ang'ania kwa sababu ya msingi kabisa.Iweje mtu kama Prof Shayo au Dr.Mvungi,agombee urais hali akijua kabisa hata akigombea ubunge ni bahati sana kuchaguliwa?Kwa siasa za Tanzania naamini wapinzani kwa ujumla wao wanajua kabisa kuking'oa CCM kwenye nafasi ya kushika dola ni kitu kigumu sana au kisichowezekanika kabisa kwa kipindi hiki.Na sababu yake iko wazi kabisa na wenyewe wanaifahamu.Acha Mapungufu ya katiba,Tume huru ya uchaguzi na vyombo vya dola kama polisi kukipendelea CCM kama wanavyodai,lakini sababu muhimu kabisa ni mizizi ya propaganda ya CCM iliyowaingia watanzania hasa wa vijijini na hata kudhani kuwa CCM ndiyo baba yao na mama yao,hivyo wataambatana nacho hata kiama.
Sasa walau watanzania wameanza kuzinduka.Wito wangu kwa wapinzani wote kuachana na ndoto za kuwa Rais kwa kipindi hiki.Badala yake kwenye uchaguzi ujao waweke nguvu nyingi kwenye majimbo ili wawe na wabunge wengi.Wakishakuwa na nguvu bungeni,chachu ya mabadiliko kwa watanzania itazidi kuongezeka na kuimarika,kwani watakuwa na nafasi nzuri zaidi ya hoja zao kusikika,kuondoa 'ndiyo mzee' ya wabunge wa CCM na kukwamisha miswada yote 'famba'.Naamini hata chances za kuibua ufisadi zitaongezeka.
Hapa siachi hata mmoja,ni wote kina Mbowe,Mtikila,Prof.Baregu,Dr.Mvungi,Mrema,Lipumba,Makaidi,Mbatia nk wakagombee ubunge 2010 na siyo Urais.Muache Mizengwe,kufitiniana nyinyi kwa nyinyi na kutumiwa na CCM.Tunataka upinzani wa kweli tanzania.Tunataka clear majority 2010.Mkishakubalika Tanzania nzima ndipo labda 2015,muweke sasa mgombea urais.Tena awe mmoja,siyo utitiri wa wababaishaji.
Nakaribisha pia wakosoaji!
 
Mkuu Mtarajiwa,

Ni kweli vyama vya upinzani vingefanikiwa zaidi kama vingeweza kuwaelimisha wananchi tokea vijijini haswa sehemu ambazo CCM imejikita kwa miaka mingi, natumaini wataanza kufanya hivyo kama hawajaanza; siyo kazi ndogo, tumeshuhudia chaguzi ndogondogo hizi CCM imekuwa ikishinda vizuri tu pamoja na tuhuma za ufisadi na ziara za mikoani za akina Zito, Mbowe, Dr.Slaa na wapinzani wengine. Huu uchaguzi wa Kiteto juzijuzi tu CCM imeshinda kwa nafasi tu. Sasa wewe jiulize pamoja na makashfa yote yaliyoanikwa dhidi ya serikali ya CCM, upinzani bado hoi...

Wakati mwingine najiuliza hivi kweli wananchi walio wengi si ajabu hawauelewi upinzani wala hawaoni umuhimu wake, si ajabu wanaona waendelee na "zimwi likujualo" maana upinzani nao saa nyingine unang'ang'ania kupinga na kulaumu weee hali inayoweza kupelekea kuonekana "sizitaki mbichi hizi"!
 
Mwakilishi Mkuu,


Hiki ni kichekesho kama siyo kituko kwa mtu kwenda kugombea Urais wakati hata jimboni kwake alikozaliwa afahamiki sawasawa.Mtu anagombea urais wakati hata MKEWE hayuko tayari kumpa kura yake!!!
 
Wajizatiti kuchuku viti vingi vya ubunge kama wapinzani na sio kama chama. nina hakika wakiwa bungeni kwa wingi wataweza kubadilisha mambo mengi sana yatakayo watengenezea njia katika chaguzi zijazo hata kama sio wao watakuwa wagombea.

Hii itawezekana tu pale ambapo wandugu hawa wataweza kuweka ubinafsi wao kando na kuonyesha uzalendo wa kweli. kwa upande wangu mpaka sasa sijaona mgombea yeyote wa uraisi kutoka chama chochote kile including CCM ambaye anaifikiria hii nchi wakati wa kutafuta hicho kiti.

2010 sio mbali mikakati inatakiwa iwe imeshakamilika, lakini pia kuna muda wa kuketi pamoja kama watz kuamua mnataka nini kwa sababu nina imani pale utakapo fanyika muungano wa kweli na sio wa maneno mabadiliko makubwa yaweza kutokea.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom