Ibrahim K. Chiki
JF-Expert Member
- Apr 5, 2011
- 594
- 163
Wana jf.....kiukweli vyama vyote vya upinzani vya tz buree kabisa, kila siku tunapiga kelele kuhusu hali mbya ya umeme na kuongezeka kwa ugumu wa maisha ya mtanzania wa kawaida, chakushangaza wao wapo kimya, sisi kama wananchi hatuwezi kuandaa maandamano, hebu kesho chama kimoja kitangaze tuu maandamano ya kupinga mgao wa umeme..awaone kama hatutatokea kwa wingi, kiukweli kabisa watz tumechoka na tupo tayari kwa chochote kwa sasa, mbona senegal wameweza? plz plz jamani vyama vyote vya upinzani mnaosoma hapa fikirieni kuhusu hili, na tutakua pamoja nanyi.