Vyama vya Upinzani na Wanaharakati Wote Andaeni Maandamano ya Amani Kudai Katiba

Gosbertgoodluck

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
2,855
401
Ndugu zangu wana JF,
Kasi ya kudai katiba mpya naona kama imepoa. Wananchi wengi mitaani wanaongelea habari ya katiba mpya lakini wanakosa uongozi wa kuwakusanya ili kuonyesha hisia zao. Jaji Mkuu Mhe. Augustino Ramadhani na viongozi wengi waandamizi ikiwa ni pamoja na Mhe. Jaji Sinde Warioba wameeleza bayana kuhusu umuhimu wa kuwa na katiba mpya inayokidhi matakwa na matarajio ya watanzania kwa ujumla.

Naomba mnifahamishe wana JF, hivi hakuna uwezekano wa chadema na vyama vingine vya upinzani pamoja wanaharakati nchini kuandaa maandamano makubwa ya amani katika mikoa yote ili kutoa fursa ya wananchi kueleza dukuduku lao na kuishinikiza serikali ianze mara moja mchakato wa kuunda katiba mpya? Mimi nina hakika hilo likifanyika litaitikisa serikali na kuiamsha kutoka kwenye usingizi mzito. Mnasemaje wazee?
 
Vyama vya upinzani Tanzania ni CHADEMA peke yake, mengine ni matawi ya CCM.

Sema CHADEMA na wanaharakati wote waandae maandamano hapo utaeleweka broda!
 
Back
Top Bottom