Vyama vya upinzani mmechangia kwa asilimia kubwa kudhoofisha Demokrasia Tanzania

mshale21

JF-Expert Member
Apr 8, 2021
2,050
4,904
Ndugu wana JF kupitia jukwaa la siasa, nawasalimu Kwa jina la Demokrasia jibuni 'kwa pamoja tuipiganie'

Ndugu wana JF, Naomba nianze kwa kunukuu maneno machache toka katika katiba ya JMT (1977) sura ya Kwanza, ibara ndogo ya kwanza katika ibara ya 8
"(1) Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Nchi inayofuata misingi ya demokrasia na haki ya kijamii, na kwa hiyo -
(a) wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na Serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wananchi kwa mujibu wa Katiba hii;
(b) lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa wananchi;
(c) Serikali itawajibika kwa wananchi;
(d) wananchi watashiriki katika shughuli za Serikali yao"
Mwisho wa kunukuu!

Ndugu wana JF, Katiba yetu ya JMT inatambua na inaelekeza vyema kabisa ya kuwa nchi yetu imepaswa kufuata misingi ya Demokrasia na haki ya jamii, Madaraka na Mamlaka yote itoke kwa wananchi, lakini ukijaribu kupima ili upate uharisia wa kile kinachoelekezwa na Katiba na kile kinachofanyika sometimes n tofauti kabisa, kwa mfano, uchaguzi uliofanyika mwaka 2020 mwezi wa 10, uligubikwa na janga kubwa liitwalo KUPITA BILA KUPINGWA, hili janga lilileta Mshangao na taharuki kubwa Sana katika jamii zetu kwani upande mmoja wa karata ulipita kwa kwa asilimia kadhaa kupitia mfumo huo lakini upande wa pili ulibaki kulalama hku ukikosa sehemu ya kwenda, hili swala liliwanyima watu haki yao ya kidemokrasia kwa mujibu wa Katiba ya nchi.

Ni kwa nini hali hii ilijitokeza?
Ukifuatilia vizur viongozi wa Vyama pinzani watakwambia ni kwa sababu ya sheria mbaya za uchaguzi kitu ambacho hata Mimi nakubaliana nao,
LAKINI binafsi Mimi Nina mtazamo mwingine tofauti nikiwatazama wao nao wanamchango mkubwa katika kuididimiza Demokrasia nchini! Kwa nini nasema hivi?
1) yalipofanyika makubaliano ya kuanzishwa kwa Vyama vingi vya siasa, je viongozi hamkusoma vizur sheria zinazohusu tume ya uchaguzi ambayo wasimazi wake ( Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na wajumbe) wote wanateuliwa na Raisi? Kama mlisoma mlizielewa? Kama mlizielewa mlichukua hatua gani kabla ya kuanzisha vyama vyenu? Au mlifunika kombe mwanaharamu apite ili muwe na namna ya kupiga noti? Kama ndivyo, nani alaumiwe Sasa?

2); kwa Sasa mnajukumu kubwa la kuhakikisha Yale yaliyotokea mwaka Jana yasijitokeze tena! Lakini kinachoshangaza mko unorganized! Yan chama hiki kinashiriki uchaguzi lakin kingine hakishiri kwa madai tuwe sio huru, kinachoshiriki kinaonesha wazi kina imani na tume, kwa mwendo huu mtafika kweli? Kwa nini msiwe na organization ya kisheria pasipo kuingiliana kiitikadi lakin muwe na msimamo mmoja hasa mnapotaka kushinikiza mabadiliko ya sheria? Huitaji ufunuo kutoka mbinguni ili ujulushwe kuwa hapa mnakwama mnakwama, na bila kumung'unya maneno msipo lisimamia hili naomba niwaambie CCM itatawala milele, msidhani kuwa kuwa Kuna mwana CCM atabadili sheria za uchaguzi kirahisi, thubutu..…!!! Hilo halipo maana nao wanaombea sheria zibak hivyohivyo ili wapite bila kupingwa, ili tume iwe upande wao
 
Umeandika vizuri. Inahitajika tume huru ili kuitupa jalalani ccm yenye mafisadi papa wasio na uzalendo na nchi hii.

Ufisadi na chama wapi na wapi. Mafisadi Ni watanzania. Hata wewe Kuna namna umeshatoa rushwa iwe ya hela. Muda. Uhuru wako binafsi. Mwili nk. Wanaokula hela Ni wa vyama vyote. Ni watanzania. So ukitaka maendelo kabla ya mavyama ambayo yote hutaka kula tu, Ni lazima wtz tujiform toka Familia kuheshimu Mali za wengine na za umma. Tuwe na uchungu na kuwa responsible na Mali na vitu vya wengine Lakini zaidi sana na maisha yetu. It’s a process. Njoo ulaya tembea barabarani mwite mtoto mpe Zawadi barabarani kama hajakushtaki atakuuliza huku akikataa Kwanini umpe kitu amefanya Kazi gani? Ukitaka kusolve haya mambo anza na wewe mwenyewe na watoto wako. So vyamaaa. Jingaaa
 
Ufisadi na chama wapi na wapi. Mafisadi Ni watanzania. Hata wewe Kuna namna umeshatoa rushwa iwe ya hela. Muda. Uhuru wako binafsi. Mwili nk. Wanaokula hela Ni wa vyama vyote. Ni watanzania. So ukitaka maendelo kabla ya mavyama ambayo yote hutaka kula tu, Ni lazima wtz tujiform toka Familia kuheshimu Mali za wengine na za umma. Tuwe na uchungu na kuwa responsible na Mali na vitu vya wengine Lakini zaidi sana na maisha yetu. It’s a process. Njoo ulaya tembea barabarani mwite mtoto mpe Zawadi barabarani kama hajakushtaki atakuuliza huku akikataa Kwanini umpe kitu amefanya Kazi gani? Ukitaka kusolve haya mambo anza na wewe mwenyewe na watoto wako. So vyamaaa. Jingaaa
Okay tumejua upo Ulaya. Asante kwa taarifa.
 
Umeandika vizuri. Inahitajika tume huru ili kuitupa jalalani ccm yenye mafisadi papa wasio na uzalendo na nchi hii.
Mie huwa bado najiuliza , hii tume huru ya uchaguzi tutaipataje? Nimejaribu kufuatilia mchakato wa kupata Jaji Mkuu wa Kenya nikagundua kama tunaweka utaratibu wa kufanya interview bado kuna uwezekano huyo anayewekwa akaingia kwa maelekezo ya wakuu.

Wasiwasi wangu ni vipi tutaendesha mchakato wa kumpata Mwenyekiti wa Tume huru ya uchaguzi? Na how independent itakuwa?
 
Vyama vingi ndio vimeharibu uchaguzi wa Serikali za mitaa 2019?
Je vyama vingi vimeharibu uchaguzi mkuu wa 2020 kwa kuingiza kura feki vituoni?
Je vyama vingi ndio viliwaamuru wakurugenzi waiootishe CCM kwa namna yoyote?
Je vyama vingi ndio vilioiga marufuku mikutano ya kisiasa?
Kamwe hamuwezi kumsafisha mwendazake kwa kuuchafua upinzani
 
Ufisadi na chama wapi na wapi. Mafisadi Ni watanzania. Hata wewe Kuna namna umeshatoa rushwa iwe ya hela. Muda. Uhuru wako binafsi. Mwili nk. Wanaokula hela Ni wa vyama vyote. Ni watanzania. So ukitaka maendelo kabla ya mavyama ambayo yote hutaka kula tu, Ni lazima wtz tujiform toka Familia kuheshimu Mali za wengine na za umma. Tuwe na uchungu na kuwa responsible na Mali na vitu vya wengine Lakini zaidi sana na maisha yetu. It’s a process. Njoo ulaya tembea barabarani mwite mtoto mpe Zawadi barabarani kama hajakushtaki atakuuliza huku akikataa Kwanini umpe kitu amefanya Kazi gani? Ukitaka kusolve haya mambo anza na wewe mwenyewe na watoto wako. So vyamaaa. Jingaaa
Zuzu ww
 
Ufisadi na chama wapi na wapi. Mafisadi Ni watanzania. Hata wewe Kuna namna umeshatoa rushwa iwe ya hela. Muda. Uhuru wako binafsi. Mwili nk. Wanaokula hela Ni wa vyama vyote. Ni watanzania. So ukitaka maendelo kabla ya mavyama ambayo yote hutaka kula tu, Ni lazima wtz tujiform toka Familia kuheshimu Mali za wengine na za umma. Tuwe na uchungu na kuwa responsible na Mali na vitu vya wengine Lakini zaidi sana na maisha yetu. It’s a process. Njoo ulaya tembea barabarani mwite mtoto mpe Zawadi barabarani kama hajakushtaki atakuuliza huku akikataa Kwanini umpe kitu amefanya Kazi gani? Ukitaka kusolve haya mambo anza na wewe mwenyewe na watoto wako. So vyamaaa. Jingaaa
Nikweli, ambaye hajawahi toa rushwa au kuiba anyooshe mkono.
Anaona nikidogo sababu nafasi uliyopo ni ndogo.
Ikiwa kubwa utafanya kama hao Mafisadi.
Mungu baba tuepushe na hizi roho za tamaa, tuwe na hofu yako, tu ndo itatuponya na tamaa.
 
Vyama vingi ndio vimeharibu uchaguzi wa Serikali za mitaa 2019?
Je vyama vingi vimeharibu uchaguzi mkuu wa 2020 kwa kuingiza kura feki vituoni?
Je vyama vingi ndio viliwaamuru wakurugenzi waiootishe CCM kwa namna yoyote?
Je vyama vingi ndio vilioiga marufuku mikutano ya kisiasa?
Kamwe hamuwezi kumsafisha mwendazake kwa kuuchafua upinzani
Mr. Bujibuji majibu katika hoja zako zote ni HAPANA! Lakin jiulize kwa kutafakari vizuri, ukipata akina jiwe watatu mfululizo miaka 30 unahisi kutakua hata na harufu ya Demokrasia? Hoja zangu hapa ni kwamba Kuna vyama vya upinzani haviko serious na democracy, mfano mzur ni Sasa kwenye mchakazo wa chaguzi ndogo, Kuna vyama vimekubali kushiriki kwenye uchaguzi wakati huo vingine vimekataa Yan tafsir yake n kwamba vingine vinakubal kuwa tume huru SI TATIZO, lakin vingine havikubalian, Sasa kwa nini wasiwe kitu kimoja kutoa misimamo ya pamoja, kama hawashiri wasishiriki wote ili kuishinikiza serikal iguswe na kwel uliopo? Kwa nini wasiunde organization ya kisheria ya umoja wa Vyama pinzani inayosimamia taratibu za kimisimamo ya vyama vyote il kudhibit chama fulan kisishiriki kwenye uchaguzi kwa matakwa yake chenyewe kama ilivyo Sasa , Hawa wanashiriki Hawa hawashiriki? Hawaoni wanasalitiana wao kwa wao? Je, sisi watazamaji na wadau tunapata picha gani zaidi ya kusema wapo kinasilahi zaidi?
 
Ufisadi na chama wapi na wapi. Mafisadi Ni watanzania. Hata wewe Kuna namna umeshatoa rushwa iwe ya hela. Muda. Uhuru wako binafsi. Mwili nk. Wanaokula hela Ni wa vyama vyote. Ni watanzania. So ukitaka maendelo kabla ya mavyama ambayo yote hutaka kula tu, Ni lazima wtz tujiform toka Familia kuheshimu Mali za wengine na za umma. Tuwe na uchungu na kuwa responsible na Mali na vitu vya wengine Lakini zaidi sana na maisha yetu. It’s a process. Njoo ulaya tembea barabarani mwite mtoto mpe Zawadi barabarani kama hajakushtaki atakuuliza huku akikataa Kwanini umpe kitu amefanya Kazi gani? Ukitaka kusolve haya mambo anza na wewe mwenyewe na watoto wako. So vyamaaa. Jingaaa
Upinzani nao ni mafisadi na disorganised angalia kundi la covid 19 walichofanya kuhujumu demokrasia nchini.
 
Ndugu wana JF kupitia jukwaa la siasa, nawasalimu Kwa jina la Demokrasia jibuni 'kwa pamoja tuipiganie'

Ndugu wana JF, Naomba nianze kwa kunukuu maneno machache toka katika katiba ya JMT (1977) sura ya Kwanza, ibara ndogo ya kwanza katika ibara ya 8
"(1) Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Nchi inayofuata misingi ya demokrasia na haki ya kijamii, na kwa hiyo -
(a) wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na Serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wananchi kwa mujibu wa Katiba hii;
(b) lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa wananchi;
(c) Serikali itawajibika kwa wananchi;
(d) wananchi watashiriki katika shughuli za Serikali yao"
Mwisho wa kunukuu!

Ndugu wana JF, Katiba yetu ya JMT inatambua na inaelekeza vyema kabisa ya kuwa nchi yetu imepaswa kufuata misingi ya Demokrasia na haki ya jamii, Madaraka na Mamlaka yote itoke kwa wananchi, lakini ukijaribu kupima ili upate uharisia wa kile kinachoelekezwa na Katiba na kile kinachofanyika sometimes n tofauti kabisa, kwa mfano, uchaguzi uliofanyika mwaka 2020 mwezi wa 10, uligubikwa na janga kubwa liitwalo KUPITA BILA KUPINGWA, hili janga lilileta Mshangao na taharuki kubwa Sana katika jamii zetu kwani upande mmoja wa karata ulipita kwa kwa asilimia kadhaa kupitia mfumo huo lakini upande wa pili ulibaki kulalama hku ukikosa sehemu ya kwenda, hili swala liliwanyima watu haki yao ya kidemokrasia kwa mujibu wa Katiba ya nchi.

Ni kwa nini hali hii ilijitokeza?
Ukifuatilia vizur viongozi wa Vyama pinzani watakwambia ni kwa sababu ya sheria mbaya za uchaguzi kitu ambacho hata Mimi nakubaliana nao,
LAKINI binafsi Mimi Nina mtazamo mwingine tofauti nikiwatazama wao nao wanamchango mkubwa katika kuididimiza Demokrasia nchini! Kwa nini nasema hivi?
1) yalipofanyika makubaliano ya kuanzishwa kwa Vyama vingi vya siasa, je viongozi hamkusoma vizur sheria zinazohusu tume ya uchaguzi ambayo wasimazi wake ( Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na wajumbe) wote wanateuliwa na Raisi? Kama mlisoma mlizielewa? Kama mlizielewa mlichukua hatua gani kabla ya kuanzisha vyama vyenu? Au mlifunika kombe mwanaharamu apite ili muwe na namna ya kupiga noti? Kama ndivyo, nani alaumiwe Sasa?

2); kwa Sasa mnajukumu kubwa la kuhakikisha Yale yaliyotokea mwaka Jana yasijitokeze tena! Lakini kinachoshangaza mko unorganized! Yan chama hiki kinashiriki uchaguzi lakin kingine hakishiri kwa madai tuwe sio huru, kinachoshiriki kinaonesha wazi kina imani na tume, kwa mwendo huu mtafika kweli? Kwa nini msiwe na organization ya kisheria pasipo kuingiliana kiitikadi lakin muwe na msimamo mmoja hasa mnapotaka kushinikiza mabadiliko ya sheria? Huitaji ufunuo kutoka mbinguni ili ujulushwe kuwa hapa mnakwama mnakwama, na bila kumung'unya maneno msipo lisimamia hili naomba niwaambie CCM itatawala milele, msidhani kuwa kuwa Kuna mwana CCM atabadili sheria za uchaguzi kirahisi, thubutu..…!!! Hilo halipo maana nao wanaombea sheria zibak hivyohivyo ili wapite bila kupingwa, ili tume iwe upande wao

Kwa Katiba ya sasa yenye Majeraha mengi na Vidonda vingi visivyokauka ulitegemea kweli Vyama vya Siasa nchini viweze Kuimarika na kuwa Taasisi ya Kuaminika kwa Uuma kama kilivyo CCM? Tuwe tunatumia vyema Akili tulizopewa na Mwenyezi Mungu Kufikiri.
 
Kwa Katiba ya sasa yenye Majeraha mengi na Vidonda vingi visivyokauka ulitegemea kweli Vyama vya Siasa nchini viweze Kuimarika na kuwa Taasisi ya Kuaminika kwa Uuma kama kilivyo CCM? Tuwe tunatumia vyema Akili tulizopewa na Mwenyezi Mungu Kufikiri.
Mkuu, ndo maana nikahoj waasisi wa Vyama pinzani, kabla ya kuanzisha Vyama vyao na kuingia rasmi katika mfumo wa Vyama vingi hawakupitia Katiba na sheria za uchaguzi na kuona kuna kasoro kubwa? Ni kama vile walitegwa wakategeka! Haiwezekan maandishi katika katiba yanaonesha mfumo wa mpira wetu, refa wetu nyinyi njooni tushindane mkategemea kushinda, hao waasisi hawakuona hatari ambayo imetufikisha tulipo hapa Leo? Kwa nin pale pale mwanzoni kabisa katika utunzi wa sheria na katiba wasipinge na kuomba marekebisho ya kisheria mpaka wamesubiri MIZIZI iote?
 
Ndugu wana JF kupitia jukwaa la siasa, nawasalimu Kwa jina la Demokrasia jibuni 'kwa pamoja tuipiganie'

Ndugu wana JF, Naomba nianze kwa kunukuu maneno machache toka katika katiba ya JMT (1977) sura ya Kwanza, ibara ndogo ya kwanza katika ibara ya 8
"(1) Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Nchi inayofuata misingi ya demokrasia na haki ya kijamii, na kwa hiyo -
(a) wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na Serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wananchi kwa mujibu wa Katiba hii;
(b) lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa wananchi;
(c) Serikali itawajibika kwa wananchi;
(d) wananchi watashiriki katika shughuli za Serikali yao"
Mwisho wa kunukuu!

Ndugu wana JF, Katiba yetu ya JMT inatambua na inaelekeza vyema kabisa ya kuwa nchi yetu imepaswa kufuata misingi ya Demokrasia na haki ya jamii, Madaraka na Mamlaka yote itoke kwa wananchi, lakini ukijaribu kupima ili upate uharisia wa kile kinachoelekezwa na Katiba na kile kinachofanyika sometimes n tofauti kabisa, kwa mfano, uchaguzi uliofanyika mwaka 2020 mwezi wa 10, uligubikwa na janga kubwa liitwalo KUPITA BILA KUPINGWA, hili janga lilileta Mshangao na taharuki kubwa Sana katika jamii zetu kwani upande mmoja wa karata ulipita kwa kwa asilimia kadhaa kupitia mfumo huo lakini upande wa pili ulibaki kulalama hku ukikosa sehemu ya kwenda, hili swala liliwanyima watu haki yao ya kidemokrasia kwa mujibu wa Katiba ya nchi.

Ni kwa nini hali hii ilijitokeza?
Ukifuatilia vizur viongozi wa Vyama pinzani watakwambia ni kwa sababu ya sheria mbaya za uchaguzi kitu ambacho hata Mimi nakubaliana nao,
LAKINI binafsi Mimi Nina mtazamo mwingine tofauti nikiwatazama wao nao wanamchango mkubwa katika kuididimiza Demokrasia nchini! Kwa nini nasema hivi?
1) yalipofanyika makubaliano ya kuanzishwa kwa Vyama vingi vya siasa, je viongozi hamkusoma vizur sheria zinazohusu tume ya uchaguzi ambayo wasimazi wake ( Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na wajumbe) wote wanateuliwa na Raisi? Kama mlisoma mlizielewa? Kama mlizielewa mlichukua hatua gani kabla ya kuanzisha vyama vyenu? Au mlifunika kombe mwanaharamu apite ili muwe na namna ya kupiga noti? Kama ndivyo, nani alaumiwe Sasa?

2); kwa Sasa mnajukumu kubwa la kuhakikisha Yale yaliyotokea mwaka Jana yasijitokeze tena! Lakini kinachoshangaza mko unorganized! Yan chama hiki kinashiriki uchaguzi lakin kingine hakishiri kwa madai tuwe sio huru, kinachoshiriki kinaonesha wazi kina imani na tume, kwa mwendo huu mtafika kweli? Kwa nini msiwe na organization ya kisheria pasipo kuingiliana kiitikadi lakin muwe na msimamo mmoja hasa mnapotaka kushinikiza mabadiliko ya sheria? Huitaji ufunuo kutoka mbinguni ili ujulushwe kuwa hapa mnakwama mnakwama, na bila kumung'unya maneno msipo lisimamia hili naomba niwaambie CCM itatawala milele, msidhani kuwa kuwa Kuna mwana CCM atabadili sheria za uchaguzi kirahisi, thubutu..…!!! Hilo halipo maana nao wanaombea sheria zibak hivyohivyo ili wapite bila kupingwa, ili tume iwe upande wao
Na wale waliokimbia na mabox ya kura wao wamechangiaje kuimarisha demokrasia.
 
Na wale waliokimbia na mabox ya kura wao wamechangiaje kuimarisha demokrasia.
Mkuu, ndo maana nikasema 'vimechangia' nkiwa na maana Kuna upande wa pili unaominya kabisa habar hyo! Shida ya viongozi wengi wa upinzani hawana ushirikiano na mshikamano baina ya Vyama vyao, jiulize kwa kipindi hki ambapo bunge n la upande mmoja watapataje hyo katiba mpya na tume huru ya uchaguzi nakat wako disorganized?!
 
Mr. Bujibuji majibu katika hoja zako zote ni HAPANA! Lakin jiulize kwa kutafakari vizuri, ukipata akina jiwe watatu mfululizo miaka 30 unahisi kutakua hata na harufu ya Demokrasia? Hoja zangu hapa ni kwamba Kuna vyama vya upinzani haviko serious na democracy, mfano mzur ni Sasa kwenye mchakazo wa chaguzi ndogo, Kuna vyama vimekubali kushiriki kwenye uchaguzi wakati huo vingine vimekataa Yan tafsir yake n kwamba vingine vinakubal kuwa tume huru SI TATIZO, lakin vingine havikubalian, Sasa kwa nini wasiwe kitu kimoja kutoa misimamo ya pamoja, kama hawashiri wasishiriki wote ili kuishinikiza serikal iguswe na kwel uliopo? Kwa nini wasiunde organization ya kisheria ya umoja wa Vyama pinzani inayosimamia taratibu za kimisimamo ya vyama vyote il kudhibit chama fulan kisishiriki kwenye uchaguzi kwa matakwa yake chenyewe kama ilivyo Sasa , Hawa wanashiriki Hawa hawashiriki? Hawaoni wanasalitiana wao kwa wao? Je, sisi watazamaji na wadau tunapata picha gani zaidi ya kusema wapo kinasilahi zaidi?

Una hoja fulani ambazo ziko kinadharia sana. Hivi vyama vyote kuanzia vya upinzani mpaka ccm kila kimoja kimeanzishwa kwa malengo yake. Hakuna uwezekano na wala sio lazima vyama hivyo kuwa na misimamo sawa. Ukitaka hivyo vyama vya upinzani viwe na msimamo mmoja, inabidi vyote viwe na lengo moja, vyama vingine ni matawi ya ccm, na vingine n matokeo ya misiguaono ndani ya vyama mbalimbali vya siasa. Katika mazingira hayo ni ngumu hiki unachoshauri kutekelezeka.

Ww tusaidie kwa jambo moja, nenda mahakamani kafungue kesi kwenye ukiukwaji wowote wa sheria kuanzia za uchaguzi, mpaka za vyama vya siasa.
 
Una hoja fulani ambazo ziko kinadharia sana. Hivi vyama vyote kuanzia vya upinzani mpaka ccm kila kimoja kimeanzishwa kwa malengo yake. Hakuna uwezekano na wala sio lazima vyama hivyo kuwa na misimamo sawa. Ukitaka hivyo vyama vya upinzani viwe na msimamo mmoja, inabidi vyote viwe na lengo moja, vyama vingine ni matawi ya ccm, na vingine n matokeo ya misiguaono ndani ya vyama mbalimbali vya siasa. Katika mazingira hayo ni ngumu hiki unachoshauri kutekelezeka.

Ww tusaidie kwa jambo moja, nenda mahakamani kafungue kesi kwenye ukiukwaji wowote wa sheria kuanzia za uchaguzi, mpaka za vyama vya siasa.
Mkuu naungana na hoja yako! Lakin si Kuna viongozi wa Vyama husika, kwa nn wasifanye ushaur wako huu??
 
Mkuu naungana na hoja yako! Lakin si Kuna viongozi wa Vyama husika, kwa nn wasifanye ushaur wako huu??

Kama hao viongozi hawana hilo wazo, na ww unaona ni sahihi, kwanini usilitekeleze kwa faida vya demokrasia?
 
Upinzani nao ni mafisadi na disorganised angalia kundi la covid 19 walichofanya kuhujumu demokrasia nchini.
Na hao wanaoitwa covid 19 wakaamua kutumia haki yao kwa katiba ya chama kilichowafukuza kukata rufaa. Chombo kilichotakiwa kusikiliza rufaa yao mpaka leo hakijakaa, na mmoja wa viongozi waandamizi wa chama alitoa tamko kuwa chama hakiwezi kukaa kujadili wasaliti.

Chama cha namna hii kinaweza kuwaambia nini wananchi kuhusu demokrasia!
 
Kama hao viongozi hawana hilo wazo, na ww unaona ni sahihi, kwanini usilitekeleze kwa faida vya demokrasia?
Basi tukubaliane kwa pamoja kuwa sometimes nao wanayumba katika swala la kuiweka democracy ya Tanzania kwenye mstar wake
 
Back
Top Bottom