Vyama vya Upinzani, kwanini mliususia Uchaguzi wa Serikali za mitaa 2019 na mkakubali kuingia kwenye Uchaguzi Mkuu 2020?

Kiboko ya Jiwe

JF-Expert Member
Apr 7, 2020
12,702
36,124
Kuna vitu vinatufanya sisi wananchi tufanye hitimisho kuwa viongozi wakuu wa upinzani ni wabinafsi wanaojali matumbo yao tu.

Twende kwenye swali husika ambalo linavijiswali vidogo ndani yake;
- Kwanini mliususia Uchaguzi wa Serikali za mitaa 2019 na mkakubali kuingia kwenye Uchaguzi Mkuu 2020?

Je, Uchaguzi Mkuu 2020 haukuwa na viashiria vya ukiukwaji wa kanuni za Uchaguzi kama mlivyodai kwenye local government election 2019?

Je, mliususia Uchaguzi wa Serikali za mitaa kwakuwa haukugusa maslahi yenu(nafasi za ubunge mlizokuwa nazo)?.

NEC mliisema sio tume huru, ilikuwaje mliingia kwenye Uchaguzi Mkuu bila kuona maboresho ndani ya hii tume?.

Mlidhani mngeutwaa ubunge kwa umaarufu wenu?

Kutokuwapigania wagombea wa serikali za mitaa 2019 kwakuwa haukugusa maslahi yenu kumesababisha na nyie mpepetwe kama ngano.
 
Walitaka shibe.

Uchaguzi wa Serikali za mitaa ulikuwa hauwahusu wao moja kwa moja!
 
Kwa maoni yangu nadhani Upinzani umeamua kuingia uchaguzi huu ili kudhihirishia wananchi na Dunia kwa ujumla kile walichokuwa wanakilalamikia kila mara. Kwamba:
-Umuhimu wa tume huru ya uchaguzi
-Uonezi kwa wapinzani
-Kukosekana uhuru wa kupata na kutoa habari
-Mihimili ya nchi wakati mwingine kuingiliana majukumu
-Katiba, Sheria na miongozo mingi kutofuatwa ipasavyo

Kiukweli kwa asilimia kubwa hili Jambo limekuwa wazi na mkanganyiko unazidi kujidhihiri kila siku. Kwa upande huo wamefanikisha, maana wananchi na Dunia inajionea kwa mifano dhahiri.
 
Serikali za mitaa hazikuwa na maslahi kwa mbowe na genge lake, hata viti maalumu ni sababu vinahusu wanawake

Chadema ni wachumia tumbo,amini nakuambia hata kina Mdee wana baraka zote za Mbowe, sababu main objective ni RUZUKU na ile michango ya 1,500000 mara wabunge 19

Chadema nayo ina wenyewe bila Connection hutoboi Imagine Hilda Newton Kakosa Ubunge wakati alishinda Viti Maalum kwenye Chama!
Imagine Jesca Kishoa Mke wa Kada wa CCM David Kafulila Katoboa Ubunge Viti Maalum CHADEMA ila Hilda Newton Kakosa!

EnnTYNjUwAAoBqO.jpg
Life is not fair kabisa
 
Kwa maoni yangu nadhani Upinzani umeamua kuingia uchaguzi huu ili kudhihirishia wananchi na Dunia kwa ujumla kile walichokuwa wanakilalamikia kila mara. Kwamba:
-Umuhimu wa tume huru ya uchaguzi
-Uonezi kwa wapinzani
-Kukosekana uhuru wa kupata na kutoa habari
-Mihimili ya nchi wakati mwingine kuingiliana majukumu
-Katiba, Sheria na miongozo mingi kutofuatwa ipasavyo

Kiukweli kwa asilimia kubwa hili Jambo limekuwa wazi na mkanganyiko unazidi kujidhihiri kila siku. Kwa upande huo wamefanikisha, maana wananchi na Dunia inajionea kwa mifano dhahiri.

Kosa la kubwa walilifanya wapinzani 2015 kwa kutokuwa na umoja itagarimu upinzani kwa kipindi cha siyo chini ya karne moja(one century), viongozi walionyima upinzani USHINDI 2015 walikuwa wawili - Kiongozi wa Act Wazalendo na Kiongozi moja wa CUF aliyekuwa mwenyekiti!! Mwaka huu 2020 walitegemea nini wakati CCM ambayo 2015 ilikuwa ICU imeshaimarishwa na Dr Magufuli Rais wa Tanzania!! Sasa tujue na kufahamu kuwa KATIBA siyo Msaafu wala Biblia, muulize Rais Putin au Angela Merkel au Kagame au Museveni Kaguta mjue kuwa Rais mzalendo lazima apewe muda wa kutosha wa kunyoosha nchi kwa faida ya TAIFA.
 
"Kabla ya uchaguzi mkuu wa 2020 ukiuliza swali kama hili makamanda watakujibu"haya kachukue buku saba"
Ila kwasasa wanakupa majibu yenye kunyooka,akili zimerudi.
 
Unapima pumzi uliyo nayo halafu unachagua, ikiwa ugombanie matembele wakati unajua kuku wanakuja au uhifadhi nguvu kwaajili ya mipaja ya kuku.
 
Back
Top Bottom