Vyama vya Upinzani, kubalini kwamba sio udikteta wote ni mbaya

CDM wala haipo tena. Haina ushawishi popote zaidi ya Kilimanjaro na Arusha kidogo. Chama cha wahuni nani anataka?
Arusha ipi mkuu.Ilishazikwa muda mrefu.Kiongozi wa maana wa mwisho alikuwa ni Ally Bananga.
Hakuna uongozi wa Chadema Arusha.Lema nae kawa mkimbizi.
 
Haya ni matamanio ya kila mwanaccm kuwa CHADEMA ipoteze nguvu, ila CHADEMA wakifanya movement hata moja na kujaza watu, utaona CCM inaanza tena kujishikisha na vyombo vya dola

Iko hivi, CCM sio chama cha kizazi hiki, na haitakaa tena ivute hisia za watu hasa vijana wa kizazi hiki. CCM haina uwezo tena wa kushinda uchaguzi wowote kihalali, na haitakaa iwe tena na uwezo huo.

Ni kweli kuwa inaweza kuendelea kukaa madarakani, ila sio kwa ushawishi tena wa kisiasa, bali ni mashirikiano yao ya kihalifu na vyombo vya dola. Mfano mrahisi ni sasa, CCM iko zaidi ya 97% kwenye sehemu zote za uwakilishi, lakini isiyo na mvuto kabisa, huku wananchi wakipuuza box la kura.

Matokeo haya ya wananchi kulipuuza box la kura ni ishara ya wazi ya kuichoka CCM, na hii itapelekea machafuko huko mbeleni ili kuitoa CCM madarakani. Tuombe machafuko hayo yasiwe makubwa, maana yataliharibu Taifa letu.
Machafuko gani tena?

Kwani mungu wenu si alishawasaidia kumuondoa dhalimu wenu bila kumwaga damu? Sasa machafuko tena kwani dhalimu bado yupo?

Hiiii bangosha..
 
Wanabodi,

Inabidi tusome nyaraka za wakati katika kipindi ambacho wapinzani wanaishiwa nguvu. Labda kupungua kwa ushawishi wa vyama vya upinzani umesababishwa na chama tawala. Vile vile labda sera zao zimepitwa na wakati. Maoni mbali mbali kuhusu harakati za vyama vya upinzani yametolewa lakini takwimu muhimu ni kwamba chama kikuu cha upinzani (CHADEMA) kilipata mbunge mmoja tu wakuchaguliwa kwenye uchaguzi wa 2020.

Sidhani kama vyama vya upinzani vitafanya vizuri kwenye uchaguzi wa 2025 na kwasababu hiyo, nimeanza kujiandaa kisaikolojia kwa ajili ya serikali yenye wawakilishi wa chama kimoja tu. Hii ni ishara ya kuelekea kwenye udikteta lakini sio udikteta wote ni mbaya.

"Benevolent dictatorship" ni aina ya udikteta ambao viongozi hufanya maamuzi sahihi na yenye manufaa kwa wananchi bila kuminya haki na uhuru wa wananchi wao. Hii hupunguza sana urasimu na michezo ya kisiasa iliyopo kwenye demokrasia.

Serikali iliyopo madarakani itakuwa imejihakikishia ushindi kwenye kila chaguzi na mamlaka ya kufanya maamuzi yoyote bila kuwashirikisha wengi. Kwasababu hiyo, ni muhimu kwa mfumo huu kuhakikisha uwepo wa nidhamu, na umakini katika kuhakikisha kwamba serikali haikosei.
Kilichopo ni kwamba CCM siyo chama Cha siasa Sasa hivi, CCM wakirudi kuwa chama cha siasa na kikategemea sanduku la kura, basi kesho tu asubuhi hawapo. Hiki chama kipo kwa nguvu ya TISS na Polisi, Hawa ndo sanduku lao la kura. CCM wakisema tunataka serikali za mitaa nchi nzima, TISS na Polisi wanatekeleza. CCM wakisema tunataka bunge la kijani tu, TISS na Polisi wanatekeleza bunge linakuwa la Chama kimoja. CCM siyo chama Cha siasa.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Lini nchi hii middle class wetu wataanza kuwa wakweli? Why middle class wetu wana huluka ya uongo,pretending?hivi hamuelewi kuwa tabia hii inatuletea generations za ajabu ambazo hazijiamini?

Mtoa hoja ur out of touch au ni mnafiki uliyelelewa kwenye familia ya kinafiki na UONGO mwingi,waambie chama dola waitishe UCHAGUZI mkuu even next week na playing field sawa na watanzania waamue kwa haki.
Uchaguazi ukiitishwa next week, wengi tutaamia upinzani ili kwenda kuona kuna nini huku. Porojo za ccm kujisifia kila siku bila kuruhusu kuhojiwa zimetukifu.
 
Wanabodi,

Inabidi tusome nyaraka za wakati katika kipindi ambacho wapinzani wanaishiwa nguvu. Labda kupungua kwa ushawishi wa vyama vya upinzani umesababishwa na chama tawala. Vile vile labda sera zao zimepitwa na wakati. Maoni mbali mbali kuhusu harakati za vyama vya upinzani yametolewa lakini takwimu muhimu ni kwamba chama kikuu cha upinzani (CHADEMA) kilipata mbunge mmoja tu wakuchaguliwa kwenye uchaguzi wa 2020.

Sidhani kama vyama vya upinzani vitafanya vizuri kwenye uchaguzi wa 2025 na kwasababu hiyo, nimeanza kujiandaa kisaikolojia kwa ajili ya serikali yenye wawakilishi wa chama kimoja tu. Hii ni ishara ya kuelekea kwenye udikteta lakini sio udikteta wote ni mbaya.

"Benevolent dictatorship" ni aina ya udikteta ambao viongozi hufanya maamuzi sahihi na yenye manufaa kwa wananchi bila kuminya haki na uhuru wa wananchi wao. Hii hupunguza sana urasimu na michezo ya kisiasa iliyopo kwenye demokrasia.

Serikali iliyopo madarakani itakuwa imejihakikishia ushindi kwenye kila chaguzi na mamlaka ya kufanya maamuzi yoyote bila kuwashirikisha wengi. Kwasababu hiyo, ni muhimu kwa mfumo huu kuhakikisha uwepo wa nidhamu, na umakini katika kuhakikisha kwamba serikali haikosei.
Tulikuaga na demokrasia ya chama kimoja na wala nchi yetu haikua na utawala wa kidikteta.
Kuvishinda vyama vya upinzani hadi kutoka kapa kwenye uchaguzi pia sio udikteta. Kwenye nchi yenye kila sifa ya umoja watu wanaweza amua kua na imani na chama kimoja peke yake. Tusisahau wakati wa ukoloni watanganyika waliipa tanu kura kwa wabunge wote ila kiti kimoja tu. Wakoloni wasingeweza kuiba kura kwa niaba ya tanu.
 
Tulikuaga na demokrasia ya chama kimoja na wala nchi yetu haikua na utawala wa kidikteta.
Kuvishinda vyama vya upinzani hadi kutoka kapa kwenye uchaguzi pia sio udikteta. Kwenye nchi yenye kila sifa ya umoja watu wanaweza amua kua na imani na chama kimoja peke yake. Tusisahau wakati wa ukoloni watanganyika waliipa tanu kura kwa wabunge wote ila kiti kimoja tu. Wakoloni wasingeweza kuiba kura kwa niaba ya tanu.
Kwa sasa, asilimia 99 ya nafasi za uongozi kuanzia serikali za mitaa zime chukuliwa na chama cha mapinduzi. Wananchi wana ruhusiwa kupiga kura lakini hilo tu halitoshi katika kushiriki kwenye uongozi wa nchi. Lazima kuna maamuzi mengi yanayofanywa na serikali bila ya kuwa na ridhaa ya wananchi. Serikali kama taasisi ina mamlaka ya kufanya kitu chochote bila kuwashirikisha wawakilishi kutoka vyama vya upinzani. Udikteta tayari upo, sio lazima uone watu wengi wame beba bunduki barabarani
 
Tunaelewa ila Udikteta ni Mbaya sama Au kwakuwa hujakutana Na Mkono wake live?

Nimeongezeka kg 7 tokea Magufuli amefariki , alale alipo huko
 
Technically unakubali kwamba Tanzania kulikuwa na Udikteta. Sasa ulishasema udikteta unamaanisha autocratic leadership, sidhani kama ukisema autocratic leadership utakuwa unamaanisha kuwa ndio mfumo mzuri .

Labda ujiuzlize ni sawa .tu aseme upo ujambazi mzuri na mbaya, au mauaji mazuri na mabaya, first place ulishasema mauaji tayari sio kitu kozuri halafu unakuja na borrow mind kusema yapo mauaji mazuri.

Vijana wa siku hizi kadiri siku zinavyoenda ndio mnapoteza uwezo wa kufikiria vizuri . No wonder we need only robots maana hamna tofauti.
 
Technically unakubali kwamba Tanzania kulikuwa na Udikteta. Sasa ulishasema udikteta unamaanisha autocratic leadership, sidhani kama ukisema autocratic leadership utakuwa unamaanisha kuwa ndio mfumo mzuri .

Labda ujiuzlize ni sawa .tu aseme upo ujambazi mzuri na mbaya, au mauaji mazuri na mabaya, first place ulishasema mauaji tayari sio kitu kozuri halafu unakuja na borrow mind kusema yapo mauaji mazuri.

Vijana wa siku hizi kadiri siku zinavyoenda ndio mnapoteza uwezo wa kufikiria vizuri . No wonder we need only robots maana hamna tofauti.
Nitatumia neno "Systemic dictatorship" kuelezea hali iliyopo sasa hivi. Kutokana na "Mass psychology", viongozi wanaweza kuwafanya wananchi kufikiria kwamba nchi hii ni ya kidemokrasia wakati hali hiyo sio sahihi. Hali halisi ni kwamba mifumo iliyopo inaisaidia sana chama tawala kubaki madarakani na kuongoza bila ya kuwa na mpinzani. Hili lisipotumiwa vizuri linaweza kuzua jambo baya lakini hali hii ikisimamiwa kwa uangalifu kama ilivyo sasa hivi basi tutaendelea kuishi kwa amani na utulivu hata kama hatu shirikishwi sana kwenye shughuli za maendeleo.
 
Nitatumia neno "Systemic dictatorship" kuelezea hali iliyopo sasa hivi. Kutokana na "Mass psychology", viongozi wanaweza kuwafanya wananchi kufikiria kwamba nchi hii ni ya kidemokrasia wakati hali hiyo sio sahihi. Hali halisi ni kwamba mifumo iliyopo inaisaidia sana chama tawala kubaki madarakani na kuongoza bila ya kuwa na mpinzani. Hili lisipotumiwa vizuri linaweza kuzua jambo baya lakini hali hii ikisimamiwa kwa uangalifu kama ilivyo sasa hivi basi tutaendelea kuishi kwa amani na utulivu hata kama hatu shirikishwi sana kwenye shughuli za maendeleo.
And you find it plausible right?
 
Back
Top Bottom