R.B
JF-Expert Member
- May 10, 2012
- 6,296
- 2,571
[h=2] [/h] Jumatano, Novemba 28, 2012 04:52 Na Amina Omari, Tanga
VYAMA vya upinzani mkoani Tanga, vimempa siku 90 Rais Jakaya Kikwete kumwajibisha Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo. Vyama hivyo, vimefikia hatua hiyo kwa kile kinachodaiwa kuwa, Waziri Muhongo alitoa maneno ya kashfa dhidi ya wananchi wa Mkoa wa Tanga, kuwa hawapendi kazi.
Wakitoa tamko kwa waandishi jana, Katibu wa Chama cha PPT Maendeleo Mkoa wa Tanga, Ramadhani Manyeko alisema, Waziri Muhongo alitumia muda mwingi kutoa hotuba ya kukejeli, jambo lililowakwaza viongozi hao.
Alisema hatua ya kwanza ni kumtaka Waziri Muhongo kuomba radhi, lakini pia atafute mbinu na mikakati itakayosaidia kuwatoa watu wa Tanga katika umaskini walionao.
Naye, Mwakilishi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Jonathan Bahweje alisema kauli za Muhongo ni za kejeli hazipaswi kuvumiliwa.
Muhongo amediriki kutuita sisi viongozi wa vyama vya siasa kuwa ni watu wa mitaani, wenye elimu duni tena ya ngumbalo, alisema Bahweje.
Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Rashid Amir alisema kauli ya Waziri Muhongo imewaondolea heshima na utu wakazi wa mkoa wake.
Huyu Muhongo aliwahi kuonywa na Spika wa Bunge, Anne Makinda na kutakiwa aache tabia ya kusema mambo ambayo hana nayo uhakika, alisema Amiri.
Katika kikao hicho, Waziri Muhongo aliwahakikishia wadau waliyotaka kujua hatima ya mgawo wa umeme ambapo alipinga na kudai hakuna kitu kama hicho.
Wiki iliyopita, Waziri Muhongo katika mkutano wake na wadau wa madini uliyofanyika kwenye ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, anadaiwa kutoa maneno ya kejeli kwa wadau hao wakiwemo viongozi wa vyama vya siasa ni watu wenye elimu duni, maskini, wapuuzi wapenda harusi na wavivu tegemezi.
VYAMA vya upinzani mkoani Tanga, vimempa siku 90 Rais Jakaya Kikwete kumwajibisha Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo. Vyama hivyo, vimefikia hatua hiyo kwa kile kinachodaiwa kuwa, Waziri Muhongo alitoa maneno ya kashfa dhidi ya wananchi wa Mkoa wa Tanga, kuwa hawapendi kazi.
Wakitoa tamko kwa waandishi jana, Katibu wa Chama cha PPT Maendeleo Mkoa wa Tanga, Ramadhani Manyeko alisema, Waziri Muhongo alitumia muda mwingi kutoa hotuba ya kukejeli, jambo lililowakwaza viongozi hao.
Alisema hatua ya kwanza ni kumtaka Waziri Muhongo kuomba radhi, lakini pia atafute mbinu na mikakati itakayosaidia kuwatoa watu wa Tanga katika umaskini walionao.
Naye, Mwakilishi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Jonathan Bahweje alisema kauli za Muhongo ni za kejeli hazipaswi kuvumiliwa.
Muhongo amediriki kutuita sisi viongozi wa vyama vya siasa kuwa ni watu wa mitaani, wenye elimu duni tena ya ngumbalo, alisema Bahweje.
Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Rashid Amir alisema kauli ya Waziri Muhongo imewaondolea heshima na utu wakazi wa mkoa wake.
Huyu Muhongo aliwahi kuonywa na Spika wa Bunge, Anne Makinda na kutakiwa aache tabia ya kusema mambo ambayo hana nayo uhakika, alisema Amiri.
Katika kikao hicho, Waziri Muhongo aliwahakikishia wadau waliyotaka kujua hatima ya mgawo wa umeme ambapo alipinga na kudai hakuna kitu kama hicho.
Wiki iliyopita, Waziri Muhongo katika mkutano wake na wadau wa madini uliyofanyika kwenye ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, anadaiwa kutoa maneno ya kejeli kwa wadau hao wakiwemo viongozi wa vyama vya siasa ni watu wenye elimu duni, maskini, wapuuzi wapenda harusi na wavivu tegemezi.