VVU kwa watoto U<15 na utayari wa wazazi wao kuwaanzishia dawa za kupunguza makali.

gfsonwin

JF-Expert Member
Apr 12, 2012
18,274
20,673
Nimatumaini yangu kwamba nyote mu wazima wa afya, lakin pia napenda kutoa pole zangu nyingi sana kwa mpendwa wetu mtangazaji wa ITV ufoo Saro kwa dhahama iliyomkuta. Pole sana na Mungu akuafu mpendwa.

Kwa muda mrefu kidogo mkoloni wangu amekuwa akinutuma kwenda kukaa kijiwen kuhesabu magari, nimekuwa nahangaika toka kijiwe kimoja kwenda kingine ili tu niweze pata data anazo taka huyu mkoloni.

Katika peke peke zangu hizo nimegundua jambo moja kubwa ambalo nafikiri labda halijakuwa addressed vyema, ama liko addressed lakini utekelezaji wake ni mbovu na hauna ufuatiliaji.

Sote tunajua vyema kwamba harakati za kumkinga mtoto na maabukizi ya VVU toka akwa mama ziliaza miaka ya 2005 hivi kwa hapa kwetu. Nyuma ya hapo ilikuwa kwamba mama akiwa muathirika basi atamzaa mtoto muathirika na wala haikupewa kipaumbele kwamba mtoto huathirika kivipi ama wakati gani, ingawa pia ilikuwa inajulikana wazi kwamba hakuna mahusiano yeyote kati ya damu inayozunguka mwilini kwa mama na ile inazunguka kwa kijusi. Hali hii ya kutojua mtoto akingwe vipi ilipelekea watoto wengi wanaozaliwa na mama wenye VVU Wazaliwe wakiwa tayari ni waathirika wa VVU.

Hata hivyo kampeni nyingi sana zilijitokeza za kukinga maambukizi ya mama kwenda kwa mtoto na hivyo kupunguza chances za mtoto kuzaliwa na VVU hata kama mama ni muathirika ingawa pia hii hai-garantee kwamba mtoto huyu aliyesalimika akiwa tumboni hadi kuzaliwa, hata weza kuambukizwa na mama yake wakati wa makuzi hasa kipindi cha kumyonyesha. Elimu juu ya unyonyeshaji wa mtoto anayezaliwa na mama mwenye VVU hutolewa bure kwa wamama ili tu kupunguza ile mianya michache iliyobaki inayoweza kumsababisha mtoto kupata maambukizi. Harta hivyo huu sio msingi wa mada yangu hii kwa leo.

Leo ninataka kujadili kidogo ama kwa upana juu ya utunzwaji wa watoto ambao tayari wana VVU. Kwanza kabisa naomba wazazi tuelewe kwamba watoto hawa hawana makosa na wala wewe mzazi pia haikuwa nia yako kumuambukiza huyu mtoto VVU hivyo usijilaumu kabisa kwa hali hii na kuamua kuificha.

Mathalan kwa hapa DSM siku ya ijumaa ndio siku ambayo imewekwa na CTC kwaajili ya kliniki ya watoto wenye VVU. Jambo la kushangaza kabisa ni kwamba siku hii ukienda kwenye vituo utakuta wazazi wanaoleta watoto wao kliniki ni wachache sana kuliko hata ilivyotegemewa.

Jambo la kushangaza zaidi siku ya Kliniki za watu wazima utakuta folen hadi unakosa pa kukanyaga. Sisemi kwamba idadi ya watoto wenye VVU ni sawa na ya watu wazima la hasah lkn namaanisha kwamba wale wachache wenye VVu huwa hawaletwi klinik wala hawaanzishiwi dawa mapema.

Hali ni mbaya zaid kwa wale ambao wana miaka kuanzia 7-hawa wazazi wao walishawakatia tamaa kabisa na huwa wanawatibu kienyeji (sina maana ya ugaga) yaani mtoto akiumwa mama atasema ni malaria atampeleka zahanati atapimwa malaria akikutwa nayo bas atapewa dawa za malaria basi, kesho akiumwa tena mama ataona uvivu atampa dawa anazojua last time alitumia mchezo umeisha.

kwa hali hii hupelekea watoto hawa kuripotiwa kuwa HIV+ wakiwa tayari wana hali mbaya sana. nimeshuhudia mwenyewe watoto wengi wakipelekwa hosp tayari wakiwa na MENINGO ama Toxo na tena hawa unakuta toka siku wanapata TB mpaka inaadvance inakuja kuwa relapse TB bado wazazi wanakuwa wagumu kukubali kuwapima HIV. hii haitoshi wazazi hawa hushuhudia watoto wao wakipoteza maisha kwa ajili ya uoga usiokuwa na tija.

Sababu kubwa ambayo niliipata kwamba kwann wazazi huogopa kumpima mtoto niliambiwa ni AIBU kwamba wazazi huona aibu lkn nikajiuliza hivi aibu hii haitawapata pindi mtoto atakapougua kiasi cha kumletea umauti??

Dr mmoja aliniambia wazi kwamba baadi ya wazazi hasa wamama hudiriki hadi kuongopa history ya ugonjwa wa mtoto hivyo kum-mislead Dr. sasa je hapa unampoteza Dr ama mtoto??

lakini pia nimegudua sheria zetu nazo zinahitaj marekebisho kwamba Dr aruhusiwe wakati fulan kuwa na maamuzi ambayo hata kama mzazi hayakubali lkn yanalenga kuokoa uhai wa mtoto basi ampime huyu mtoto.sion kama kuna faida kufuata msimamo wa mzazi wakati mwili unaoumizwa ni wa mtoto asiye weza kujisemea kwa kipindi hicho na pengine angepewa nafasi ya kujisemea basi angeweza kusema tofauti na mzazi anavyotaka.


Hebu basi wazazi waache ubinafsi waone ukweli watoto wao nao wanahitaj kufurahia maisha kama wao. wakubali matokeo jaman wawapeleke watoto Kliniki wakapimwe na wawe tayari kuwapa dawa. Naumia sana nionapo msururu mrefuuu wa watu wazima wakichukua dawa huku wakiwa wamewafunga watoto ndani eti wanakwepa aibu.

Wasalaam
gfsonwin




 
Dah!! kweli nimeamini yaani hata uzi tu unaohusu VVU watu wanakwepa kuchangia....................
ningekuwa nimeweka mambo ya mavibration hapa toka usiku wa jana saa hii uzi ungekuwa page ya 10+
haya mambo yapo na gonjwa hili lipo cha muhimu ni watu wajifunze jins ya kuish na kuwakinga wapendwa wao, na kukubali kuwahudumia kwa upendo.

tunataka kuestablish home based standard ya kutunza wagonjwa kiasi kwamba sio wagonjwa wote wawe wanalazwa hosp kama ilivyosasa na kuona ni kwa kiasi gani home care inaweza kumuongezea mtu maisha na kumpa unafuu zaid.
 
Dah!! kweli nimeamini yaani hata uzi tu unaohusu VVU watu wanakwepa kuchangia....................
ningekuwa nimeweka mambo ya mavibration hapa toka usiku wa jana saa hii uzi ungekuwa page ya 10+
haya mambo yapo na gonjwa hili lipo cha muhimu ni watu wajifunze jins ya kuish na kuwakinga wapendwa wao, na kukubali kuwahudumia kwa upendo.

tunataka kuestablish home based standard ya kutunza wagonjwa kiasi kwamba sio wagonjwa wote wawe wanalazwa hosp kama ilivyosasa na kuona ni kwa kiasi gani home care inaweza kumuongezea mtu maisha na kumpa unafuu zaid.

Nini kimekusukuma kutuandikia hii makitu ya kutisha. Wenzio tunaogopa.
 
Nini kimekusukuma kutuandikia hii makitu ya kutisha. Wenzio tunaogopa.

unaogopa nini??
nimesukumwa na nilichokiona huko kijiwen nilipopewa kazi ya kuhesabu magari yaingiayo gereji kwa kosa la mafuta yake kuchakachuliwa
 
how do you tell your child he/she has terminal illness??

ni 'mtihani mgumu sana' kwa wazazi. wanajihisi 'wamefail' kuwalinda wanao na wanashindwa how to proceed. it need counselling and i doubt kama psychologists wetu wako equiped to do this. 'inaumiza sana' hasa ukifahamu kwamba mtoto 'hana hatia'
 
how do you tell your child he/she has terminal illness??

ni 'mtihani mgumu sana' kwa wazazi. wanajihisi 'wamefail' kuwalinda wanao na wanashindwa how to proceed. it need counselling and i doubt kama psychologists wetu wako equiped to do this. 'inaumiza sana' hasa ukifahamu kwamba mtoto 'hana hatia'
Blaine kuna jambo moja ambalo watu tunapswa kulijua kwaba kama kweli tatizo lipo basi tufikiri namna ya kupunguza madhara na sio kufikiri kilichotokea.

watoaushauri nasaha katika CTC klinic wako equipped na skills muhimu ili kuweza kumsaidia mzazi ingawa pia huwa hatushauri sana mtoto kuambiwa jambo hili na mzazi wake as wazazi wengi hushindwa na hisia za mapenzi juu ya watoto wao. Anayetakiwa kumwambia mtoto ni mshauri nasaha na atamwambia mtoto baada ya kumfanyia cancelling ya kutosha hadi akaridhika.

sio kazi ya mzazi kumwambia mtoto anaumwa nini..............

tatizo linakuja kwamba wazazi wengi huhofia hili kwamba mtoto akijua basi mm ndio chanzo...................lkn wakasahahu kwamba woga wao hauna msaada kwa kipindi hiki manake ni heri uwe jasiri umtibie uendelee kuish nae kuliko kuwa mwoga halafu umpoteze uanze kujuta kama wengi wafanyavyo sasa.............

yaani unakuta mama kila ukimsihi tumpime mtoto anagoma kabisa anadai siko tayari bado, ila mtoto akishafariki anaaza sijui nini kilinifunga nikashindwa kumpima mwanangu maskini...........mwanangu asingalikufa kama sio mimi............
maneno haya huumiza sana kwa wengine manake wanajua walikuwa kwenye position ya kuzuia haya kutokea.
 
Last edited by a moderator:
Blaine kuna jambo moja ambalo watu tunapswa kulijua kwaba kama kweli tatizo lipo basi tufikiri namna ya kupunguza madhara na sio kufikiri kilichotokea.

watoaushauri nasaha katika CTC klinic wako equipped na skills muhimu ili kuweza kumsaidia mzazi ingawa pia huwa hatushauri sana mtoto kuambiwa jambo hili na mzazi wake as wazazi wengi hushindwa na hisia za mapenzi juu ya watoto wao. Anayetakiwa kumwambia mtoto ni mshauri nasaha na atamwambia mtoto baada ya kumfanyia cancelling ya kutosha hadi akaridhika.

sio kazi ya mzazi kumwambia mtoto anaumwa nini..............

tatizo linakuja kwamba wazazi wengi huhofia hili kwamba mtoto akijua basi mm ndio chanzo...................lkn wakasahahu kwamba woga wao hauna msaada kwa kipindi hiki manake ni heri uwe jasiri umtibie uendelee kuish nae kuliko kuwa mwoga halafu umpoteze uanze kujuta kama wengi wafanyavyo sasa.............

yaani unakuta mama kila ukimsihi tumpime mtoto anagoma kabisa anadai siko tayari bado, ila mtoto akishafariki anaaza sijui nini kilinifunga nikashindwa kumpima mwanangu maskini...........mwanangu asingalikufa kama sio mimi............
maneno haya huumiza sana kwa wengine manake wanajua walikuwa kwenye position ya kuzuia haya kutokea.

CTC clinic iko wapi?
 
Last edited by a moderator:
CTC clinic iko wapi?

kwanza kabisa ngoja nikupe long form yake CTC ni abb ya Care and Treatment Clinic.
clinic hizi zipo katika kila kituo cha afya na hosp kwaajili ya watu wenye TB na HIV.
 
Blaine kuna jambo moja ambalo watu tunapswa kulijua kwaba kama kweli tatizo lipo basi tufikiri namna ya kupunguza madhara na sio kufikiri kilichotokea.

watoaushauri nasaha katika CTC klinic wako equipped na skills muhimu ili kuweza kumsaidia mzazi ingawa pia huwa hatushauri sana mtoto kuambiwa jambo hili na mzazi wake as wazazi wengi hushindwa na hisia za mapenzi juu ya watoto wao. Anayetakiwa kumwambia mtoto ni mshauri nasaha na atamwambia mtoto baada ya kumfanyia cancelling ya kutosha hadi akaridhika.

sio kazi ya mzazi kumwambia mtoto anaumwa nini..............

tatizo linakuja kwamba wazazi wengi huhofia hili kwamba mtoto akijua basi mm ndio chanzo...................lkn wakasahahu kwamba woga wao hauna msaada kwa kipindi hiki manake ni heri uwe jasiri umtibie uendelee kuish nae kuliko kuwa mwoga halafu umpoteze uanze kujuta kama wengi wafanyavyo sasa.............

yaani unakuta mama kila ukimsihi tumpime mtoto anagoma kabisa anadai siko tayari bado, ila mtoto akishafariki anaaza sijui nini kilinifunga nikashindwa kumpima mwanangu maskini...........mwanangu asingalikufa kama sio mimi............
maneno haya huumiza sana kwa wengine manake wanajua walikuwa kwenye position ya kuzuia haya kutokea
.
guilty conscience.

kama CTC wako equiped then keep trying. mwanzo mgumu but eventually it will get better. wazazi wapewe ushauri how to reduce their guilty feeling, hii itasaidia sana
 
Last edited by a moderator:
kwanza kabisa ngoja nikupe long form yake CTC ni abb ya Care and Treatment Clinic.
clinic hizi zipo katika kila kituo cha afya na hosp kwaajili ya watu wenye TB na HIV.

Oh, siku nyingine usiwe unatuacha kwenye mataa washika vyuma.

&#304;la mi kupima ngoma mi mtanisamehe bure.
 
guilty conscience.

kama CTC wako equiped then keep trying. mwanzo mgumu but eventually it will get better. wazazi wapewe ushauri how to reduce their guilty feeling, hii itasaidia sana
binafsi nalazimika kuona kwamba wazazi wengi ni selfish. Blaine imagine mzazi anapanga folen kupata dawa na haoni aibu wala shida, lkn lijapo swala la mtoto wake anajionea tabu na woga huu je sio ubinafsi??
 
Last edited by a moderator:
binafsi nalazimika kuona kwamba wazazi wengi ni selfish. Blaine imagine mzazi anapanga folen kupata dawa na haoni aibu wala shida, lkn lijapo swala la mtoto wake anajionea tabu na woga huu je sio ubinafsi??

Na roho mbaya tu anaona mtoto hastaili kuishi ila
Kuna mtoto namfahamu nae wazazi wake walimcheleweshea dawa yaani ameanza dawa akiwa weak sana ila now anaendelea vizuri sasa ina mcost sana anatumia nutrition za GNLD na ARV wakati angemwanzshia dose mapema wala asingetumia gharama nyingi

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Dah!! kweli nimeamini yaani hata uzi tu unaohusu VVU watu wanakwepa kuchangia....................
ningekuwa nimeweka mambo ya mavibration hapa toka usiku wa jana saa hii uzi ungekuwa page ya 10+
haya mambo yapo na gonjwa hili lipo cha muhimu ni watu wajifunze jins ya kuish na kuwakinga wapendwa wao, na kukubali kuwahudumia kwa upendo.

tunataka kuestablish home based standard ya kutunza wagonjwa kiasi kwamba sio wagonjwa wote wawe wanalazwa hosp kama ilivyosasa na kuona ni kwa kiasi gani home care inaweza kumuongezea mtu maisha na kumpa unafuu zaid.

Mi nachoelewa kuna ile huduma ya HBC ambapo ni Home Based Care watu wanahudumiwa majumbani mwao na hao hbc care givers na vilevile wanahamasisha upimaji kwa wanafamilia wengine ambao hawajapima ikiwa ni pamoja na watoto.Lakini changamoto ipo pale ambapo unakuta mgonjwa huyu hajaishirikisha familia yake hali ya maambukizi aliokua nayo...bado kuna kazi kubwa ya kuuondoa unyanyapaa kwa mgonjwa mwenyewe na kwa jamii yote.Pili ni kweli kabisa watoto wanapata shida sana kutokupimwa na kupata matibabu sahihi...
 
na roho mbaya tu anaona mtoto hastaili kuishi ila
kuna mtoto namfahamu nae wazazi wake walimcheleweshea dawa yaani ameanza dawa akiwa weak sana ila now anaendelea vizuri sasa ina mcost sana anatumia nutrition za gnld na arv wakati angemwanzshia dose mapema wala asingetumia gharama nyingi

sent from my blackberry 9220 using jamiiforums

sasa mkuu umeona huyo anauwezo wa kupata hata hizo nutrition suppliment
imagine mtu hana uwezo halafu bado anasema naogopa kweli mtu huyu utasema hajafanyiwa kanseling ama ni ujinga tu??
 
mi nachoelewa kuna ile huduma ya hbc ambapo ni home based care watu wanahudumiwa majumbani mwao na hao hbc care givers na vilevile wanahamasisha upimaji kwa wanafamilia wengine ambao hawajapima ikiwa ni pamoja na watoto.lakini changamoto ipo pale ambapo unakuta mgonjwa huyu hajaishirikisha familia yake hali ya maambukizi aliokua nayo...bado kuna kazi kubwa ya kuuondoa unyanyapaa kwa mgonjwa mwenyewe na kwa jamii yote.pili ni kweli kabisa watoto wanapata shida sana kutokupimwa na kupata matibabu sahihi...

unachokisema sipingani nacho ila hbc nayo bado haijawekewa standards ambazo ziko valid.
Swala ninaloumizwa nalo ni kwann watoto wame ndio wahanga wa unyanyapaa?? Yaani wazazi wao wenyewe wanaaza kuwanyanyapaa kwa kuwaficha na kutokuwapa huduma husika mwishowe watoto wanakufa mzazi anabaki kuponda raha jambo hili linaumaiza sana
 
Kumuanzisha dozi ya VIDONGE mtoto wa miaka 3 wakati akiumwa ugonjwa wowote hunywa dawa ya syrup (tena tamu), ni shuguli pevu sana. Inahuzunisha sana kuumwa kwa mtoto mdogo kama huyo na inatia uwoga sana kumpima mtoto kwani akigundulika ameathirika, mzazi anaweza kurukwa na akili ama kufa kwa presha bure. Ndio maana wengi wanaogopa kuwapima watoto wao hadi afya zao zinapokuwa mbaya kabisa. Ni mtihani mkubwa sana kwa mzazi...sio uamuzi rahisi kuuchukua huu.
 
Back
Top Bottom