Bigirita
Platinum Member
- Feb 12, 2007
- 15,986
- 7,366
Nikiwa mdogo, mjomba wangu aliwahi kuniuliza, ninapenda kifaa gani kizuri cha muziki? mimi kwa kuwa nilipenda filimbi nikasema filimbi ndo kifaa kizuri, akaniuliza kwa nini? nikasema kwakuwa kinatoa milio tofauti kwa nyimbo tofauti.
Mjomba akaniangalia usoni, akaniambia, hiyo ni milio tofauti au mlio ule ule katika ala tofauti?
Akasema, kama ni mlio tofauti, basi filimbi ingeweza kutoa mlio wa ngoma. Nikagundua busara ya mjomba. Nikanyamaza.
Haya ya JK na milio ule ule kutoka kwenye VUVUZELA linalotoa mlio wa kati yanakubalika kwa wananchi? Kama VUVUZELA alilotumia 2005 halikuweza kuwaburudisha watanzania, anauhakika gani kwamba, wimbo ule ule kwa kuongeza neno zaidi kutoka katika VUVUZELA lile lile, utawaburudisha watanzania wasio na maji, uhakika wa chakula, uhakika wa matibabu, elimu bora, barabara, pembejeo za kilimo n.k.??
Tutafakari!!
Mjomba akaniangalia usoni, akaniambia, hiyo ni milio tofauti au mlio ule ule katika ala tofauti?
Akasema, kama ni mlio tofauti, basi filimbi ingeweza kutoa mlio wa ngoma. Nikagundua busara ya mjomba. Nikanyamaza.
Haya ya JK na milio ule ule kutoka kwenye VUVUZELA linalotoa mlio wa kati yanakubalika kwa wananchi? Kama VUVUZELA alilotumia 2005 halikuweza kuwaburudisha watanzania, anauhakika gani kwamba, wimbo ule ule kwa kuongeza neno zaidi kutoka katika VUVUZELA lile lile, utawaburudisha watanzania wasio na maji, uhakika wa chakula, uhakika wa matibabu, elimu bora, barabara, pembejeo za kilimo n.k.??
Tutafakari!!