Mwan mpambanaji
JF-Expert Member
- Apr 3, 2008
- 482
- 131
Katika hali ya kushangaza Dunia, mahakama ya hakimu mkazi Arusha,imesema haina mamlaka ya kutoa dhamana kwa Washtakiwa 20 ambao ni wanachama na viongozi wa CHADEMA wanaokabiliwa na Kesi no 72,75 na 76 zote za Uhujumu Uchumi zinazokabili wanachama 20 wa Arusha Mjini na Arumeru Magharibi
Hakimu Mfawidhi Bi.Mahumbugwa alikuwa anawasiliana na wakili wa serikali kabla ya kusoma hukumu hii ambayo imefanya ndugu wa washtakiwa kubaki midomo wazi, kabla ya hukumu ya leo Hakimu huyu huyu na mahakama hii ilitoa uamuzi Novemba 9 kuwa ina mamlaka ya kutoa dhamana kwa kuwa shtaka lenyewe halina zaidi ya 10mil.Ni mara ya kwanza kwa hakimu wa mahakama kutoa hukumu mbili tofauti kwenye shauri moja
Kisheria baada ya hukumu ya kwanza upande wa Jamhuri ulipaswa kukata rufaa kupinga uamuzi wa mahakama lakini badala yake hakimu amewekewa shinikizo na Serikali kufuta hukumu ya awali
Baada ya ndugu kusikia hivo walizingira mahakama wakitaka haki itendeke kwa ndugu zao ambao ndio watafuta mkate wa kila siku wa familia,baadhi ya washtakiwa wana watoto wachanga!
Mawakili wa upande wa Wafuasi wameeleza kuwa wataenda mahakama kuu kuomba dhamana kwa ajili ya wateja wao! Jopo hili linaongozwa na Wakili maarufu Jijini Arusha Sheck Mfinanga,pamoja na wakili Jebra Kambole na Winnie
Ndugu wa washtakiwa walionekana mahakamani hapa wakiwa na jaziba kali kiasi cha kutishia usalama wa mahakama,na wamesema siku ya shauri watakuja kwa wingi kuonyesha mshikamano,aidha wametaka Mahakama itende haki kwa kuwa ndugu zao wamebambikiziwa kesi za kisiasa
My take,
Mahakama inapaswa kutoa haki mapema maana haki iliyocheleweshwa ni haki iliyonyimwa.
Huyu hakimu aache ubabaishaji atende haki maana kuna siku uvumilivu utawashinda watu
Hakimu Mfawidhi Bi.Mahumbugwa alikuwa anawasiliana na wakili wa serikali kabla ya kusoma hukumu hii ambayo imefanya ndugu wa washtakiwa kubaki midomo wazi, kabla ya hukumu ya leo Hakimu huyu huyu na mahakama hii ilitoa uamuzi Novemba 9 kuwa ina mamlaka ya kutoa dhamana kwa kuwa shtaka lenyewe halina zaidi ya 10mil.Ni mara ya kwanza kwa hakimu wa mahakama kutoa hukumu mbili tofauti kwenye shauri moja
Kisheria baada ya hukumu ya kwanza upande wa Jamhuri ulipaswa kukata rufaa kupinga uamuzi wa mahakama lakini badala yake hakimu amewekewa shinikizo na Serikali kufuta hukumu ya awali
Baada ya ndugu kusikia hivo walizingira mahakama wakitaka haki itendeke kwa ndugu zao ambao ndio watafuta mkate wa kila siku wa familia,baadhi ya washtakiwa wana watoto wachanga!
Mawakili wa upande wa Wafuasi wameeleza kuwa wataenda mahakama kuu kuomba dhamana kwa ajili ya wateja wao! Jopo hili linaongozwa na Wakili maarufu Jijini Arusha Sheck Mfinanga,pamoja na wakili Jebra Kambole na Winnie
Ndugu wa washtakiwa walionekana mahakamani hapa wakiwa na jaziba kali kiasi cha kutishia usalama wa mahakama,na wamesema siku ya shauri watakuja kwa wingi kuonyesha mshikamano,aidha wametaka Mahakama itende haki kwa kuwa ndugu zao wamebambikiziwa kesi za kisiasa
My take,
Mahakama inapaswa kutoa haki mapema maana haki iliyocheleweshwa ni haki iliyonyimwa.
Huyu hakimu aache ubabaishaji atende haki maana kuna siku uvumilivu utawashinda watu