Vurugu za Xenophobia Afrika ya Kusini: Upande wa Pili wa Sarafu

Stuxnet

JF-Expert Member
Feb 12, 2011
10,335
17,850
Vitendo vinavyofanywa na raia wa Afrika Kusini dhidi ya maisha na mali za Wahamiaji ni vitendo viovu ambavyo vinapaswa kulaaniwa na Waafrika wote.

Bara la Afrika ni moja na mipaka iliwekwa mwishoni mwa karne ya 18 na Wakoloni ili waweze kututawala kiurahisi na kupora mali asili yetu.

Pamoja na hizo vurugu zinazofanywa dhidi ya wahamiaji kuna mambo kama 6 yanayopelekea vurugu hizo zitokee;

1. Wahamiaji kutoka Zimbabwe wanakimbia uchumi mbovu ambao umeharibiwa na viongozi wao (Robert Mugabe 1980-17 na sasa Mnanhagwa). Laiti Robert Muhabe asingeleta sera ya kugawa ardhi ya Masetla kwa Maveterani wa vita vya ukombozi wa Zimbabwe mwaka 2000, uchumi wa Zimnabwe usingevurugika na Wazimbabwe wasingekimbikia South Africa kutafuta vibarua.

2. Wahamiaji wanaoshambuliwa ni haramu (undocumented). Wameingia kwa njia za panya. Wameroroka nchini kwao na kutopita kwenye mifumo ya Uhamiaji. Kwa mfano vijana wa Tanzania wengi hawana hata uwezo wa kuishi nyumba za kupanga. Aidha wanalala kwenye korido za majumba makubwa au kwenye magari mabovu maeneo ya garage. Wengine hulala kwenye meli mbovu katika majiji yaliyoko pembezoni mwa bahari.

3. Wahamiaji haramu hawana sifa (skills) za kuwawezesha kufanya kazi za kitaalamu kule hivyo huishia kufanya biashara haramu kama ; kuuza mihadarati, kufanya ukahaba, kuuza silaha na ujambazi wa kutumia silaha.
Watanzania hufanya biashara za uganga wa kienyeji, kuuza karanga na nyanya, kuuza kete za bangi nk

4. Katika kitovu cha Johannesburg maarufu kama Hilbrough, Wanaigeria ndiyo wamiliki wa majumba makubwa baada ya Wazungu kukimbia uharamia unaofanyika. Katika eneo hili ndiyo biashara ya silaha, mihadarati na ukahaba umekithiri

5. Wahamiaji haramu wako tayari kufanya kazi yeyote kwa mshahara wowote watakaopewa na Kaburu. Kitendo hiki kinawakwaza Wenyeji kwa vile wanataka kulipwa kadri ya bei ya soko. Wenyeji wana vyama vya wafanyakazi vilivyo imara, hivyo basi mara nyingi hufanya mgomo. Wakati wa mgomo Kaburu huwaajiri Wahamiaji, na hapo ndipo chuki kutoka kwa Wenyeji inapoanzia.

Wito Wangu;
Nchi zote zilizo kaskazini mwa Afrika ya Kusini ziweke mazingira wezeshi kwa vijana kupata ajira ikiwa ni pamoja na matumizi ya Raslimali zao za asili vizuri. Botswana iko karibu sana na South Africa lakini tatizo la wahamiaji si kubwa kama Tanzania Mozambique na Malawi
 
Tatizo sijaona hata Mchina mmoja wakati wapo wengi sana yaani hawa wanatafuta Waafrika tu. US pamoja na matatizo yake ukiacha wanasiasa watu wako poa na tunachapa kazi. Ushindani unaleta maendeleo angalia hata China maendeleo yamekuja baada ya kuruhusu watu kuingia. Wanaogopa wahamiaji ni wavivu maana mwenyeji kila siku ana adavantages wahamiaji ni visingizio tu
 
Tatizo sijaona hata Mchina mmoja wakati wapo wengi sana yaani hawa wanatafuta Waafrika tu. US pamoja na matatizo yake ukiacha wanasiasa watu wako poa na tunachapa kazi. Ushindani unaleta maendeleo angalia hata China maendeleo yamekuja baada ya kuruhusu watu kuingia. Wanaogopa wahamiaji ni wavivu maana mwenyeji kila siku ana adavantages wahamiaji ni visingizio tu
Yes uko sawa, wale wenzetu makovu ya ubaguzi wa rangi bado yapo kwa vile yamehamia kwa karne 5. Pili hata elimu waliyopewa haikuwa na tija sana.
 
Haiwezi justify mauaji wanayofanya, ni upuuzi kiwango cha juu sana kuuwa weusi wenzao eti kwa kisingizio cha makovu ya ubaguzi waliofanyiwa, nachelea kusema walistahili ule ubaguzi kama mindset zao ziko hivyo.
Zimbabwe umaskini wa RAIA kwakuwa wazungu walinyang'anywa mashamba, na hao makaburu waliachiwa mashamba mbona wasauzi still maskini kiasi cha kuwa na wivu dhidi ya weusi wenzao na mpaka inawafanyia ukatili na kuwaua?
Afrika kuna shida zaidi ya mashamba tunayodhani tumewaachia wazungu au tumewapora japo ardhi ni yetu..kuna muafrika ana miliki ardhi kubwa kama wazungu wafanyavyo Africa?
Tanzania nako mpaka tunakamatiwa ndege si ni ardhi chanzo?
Alieturoga Afrika hakika anatushangaa tena maana hakutegemea kama tungerogeka kiasi hiki...
Wapuuzi wa south afrika watafutiwe dawa ya kudumu maana sasa hakuna namna.
Yes uko sawa, wale wenzetu makovu ya ubaguzi wa rangi bado yapo kwa vile yamehamia kwa karne 5. Pili hata elimu waliyopewa haikuwa na tija sana.
 
Haiwezi justify mauaji wanayofanya, ni upuuzi kiwango cha juu sana kuuwa weusi wenzao eti kwa kisingizio cha makovu ya ubaguzi waliofanyiwa, nachelea kusema walistahili ule ubaguzi kama mindset zao ziko hivyo.
Zimbabwe umaskini wa RAIA kwakuwa wazungu walinyang'anywa mashamba, na hao makaburu waliachiwa mashamba mbona wasauzi still maskini kiasi cha kuwa na wivu dhidi ya weusi wenzao na mpaka inawafanyia ukatili na kuwaua?
Afrika kuna shida zaidi ya mashamba tunayodhani tumewaachia wazungu au tumewapora japo ardhi ni yetu..kuna muafrika ana miliki ardhi kubwa kama wazungu wafanyavyo Africa?
Tanzania nako mpaka tunakamatiwa ndege si ni ardhi chanzo?
Alieturoga Afrika hakika anatushangaa tena maana hakutegemea kama tungerogeka kiasi hiki...
Wapuuzi wa south afrika watafutiwe dawa ya kudumu maana sasa hakuna namna.
Kweli hizo sababu hazina justification, pengine ni laana tu
 
Tatizo kubwa la huo uhuni huko Afrika kusaini ni ajira. Huko Afrika kusini kuna maendeleo ya vitu kuliko ya watu, hali hiyo ndio inaleta msongo wa mawazo kwa wale wanaoishi kwa ufukara mkubwa. Hatari hiyo iliyo Afrika kusaini huenda ikatokea hapa nchi hata kwa namna tofauti, wananchi hawana ajira wakati pesa nyingi inapelekwa kwenye miradi ya maendeleo na wenye ajira mishahara yao haipandi, hivyo maisha kuzidi kuwa magumu, huku viongozi hawajali kwani wao wana mishahara mikubwa.
 
Tatizo la SA ni kubwa sana na wasipolitatua litawapeleka pabaya zaidi.

Rais wetu naye anapaswa sana kujifunza kwa hili la Afrika kusini kwamba, mabarabara, maflyover, mandege nk sio sehemu pekee ya kupeleka hela kwani wananchi watakapokuwa na maisha magumu hayo maendeleo pekee hayatakuwa suluhu, inapaswa kubalance maisha ya watu na miradi ya maendeleo hasa kutoa ajira na mishahara kuboreshwa.
 
5. Wahamiaji haramu wako tayari kufanya kazi yeyote kwa mshahara wowote watakaopewa na Kaburu. Kitendo hiki kinawakwaza Wenyeji kwa vile wanataka kulipwa kadri ya bei ya soko. Wenyeji wana vyama vya wafanyakazi vilivyo imara, hivyo basi mara nyingi hufanya mgomo. Wakati wa mgomo Kaburu huwaajiri Wahamiaji, na hapo ndipo chuki kutoka kwa Wenyeji inapoanzia.
Kwahiyo kabla hawajafanya ule udhalimu huwa wanaanza kukuuliza uoneshe passport yako ilipogongwa ili kujiridhisha kwamba uliingia kwa njia za halali, au?
 
Wanapossma wanaigeria wanafanya biashara haramu maana yake hiyo nchi ina madhaifu kwenye mfumo wa sheria na ulinzi na usalama, kwanini wasishtakiwe hao wafanya biashara haramu badala yake mahakama ziwe wananchi?
 
Kwahiyo kabla hawajafanya ule udhalimu huwa wanaanza kukuuliza uoneshe passport yako ilipogongwa ili kujiridhisha kwamba uliingia kwa njia za halali, au?
Hapo amejigonga. Hawana cha halali wala hawana cha haramu. Ukionekana wewe ni mgeni mweusi machoni mwao na ukashindwa vigezo vyao vya uenyeji wanaanzana na wewe..... Halafu kuna hao wenye biashara kama maduka, wamefungua kihalali na wanalipa kodi... mbona na wao maduka yao yanafanyiwa ushenzi? Tatizo la Afrika Kusini liko zaidi kwenye uvivu na kupenda starehe kwa raia wake. Waliwavurumusha makaburu bure tu lakini hawana uwezo wa kuendesha nchi. Nina uhakika hata wageni wote wakiondoka bado wataendelea kuwa na maisha mabaya tu.
 
Vitendo vinavyofanywa na raia wa Afrika Kusini dhidi ya maisha na mali za Wahamiaji ni vitendo viovu ambavyo vinapaswa kulaaniwa na Waafrika wote.

Bara la Afrika ni moja na mipaka iliwekwa mwishoni mwa karne ya 18 na Wakoloni ili waweze kututawala kiurahisi na kupora mali asili yetu.

Pamoja na hizo vurugu zinazofanywa dhidi ya wahamiaji kuna mambo kama 6 yanayopelekea vurugu hizo zitokee;

1. Wahamiaji kutoka Zimbabwe wanakimbia uchumi mbovu ambao umeharibiwa na viongozi wao (Robert Mugabe 1980-17 na sasa Mnanhagwa). Laiti Robert Muhabe asingeleta sera ya kugawa ardhi ya Masetla kwa Maveterani wa vita vya ukombozi wa Zimbabwe mwaka 2000, uchumi wa Zimnabwe usingevurugika na Wazimbabwe wasingekimbikia South Africa kutafuta vibarua.

2. Wahamiaji wanaoshambuliwa ni haramu (undocumented). Wameingia kwa njia za panya. Wameroroka nchini kwao na kutopita kwenye mifumo ya Uhamiaji. Kwa mfano vijana wa Tanzania wengi hawana hata uwezo wa kuishi nyumba za kupanga. Aidha wanalala kwenye korido za majumba makubwa au kwenye magari mabovu maeneo ya garage. Wengine hulala kwenye meli mbovu katika majiji yaliyoko pembezoni mwa bahari.

3. Wahamiaji haramu hawana sifa (skills) za kuwawezesha kufanya kazi za kitaalamu kule hivyo huishia kufanya biashara haramu kama ; kuuza mihadarati, kufanya ukahaba, kuuza silaha na ujambazi wa kutumia silaha.
Watanzania hufanya biashara za uganga wa kienyeji, kuuza karanga na nyanya, kuuza kete za bangi nk

4. Katika kitovu cha Johannesburg maarufu kama Hilbrough, Wanaigeria ndiyo wamiliki wa majumba makubwa baada ya Wazungu kukimbia uharamia unaofanyika. Katika eneo hili ndiyo biashara ya silaha, mihadarati na ukahaba umekithiri

5. Wahamiaji haramu wako tayari kufanya kazi yeyote kwa mshahara wowote watakaopewa na Kaburu. Kitendo hiki kinawakwaza Wenyeji kwa vile wanataka kulipwa kadri ya bei ya soko. Wenyeji wana vyama vya wafanyakazi vilivyo imara, hivyo basi mara nyingi hufanya mgomo. Wakati wa mgomo Kaburu huwaajiri Wahamiaji, na hapo ndipo chuki kutoka kwa Wenyeji inapoanzia.

Wito Wangu;
Nchi zote zilizo kaskazini mwa Afrika ya Kusini ziweke mazingira wezeshi kwa vijana kupata ajira ikiwa ni pamoja na matumizi ya Raslimali zao za asili vizuri. Botswana iko karibu sana na South Africa lakini tatizo la wahamiaji si kubwa kama Tanzania Mozambique na Malawi

Me huwa nashindwa kabisa kuelewa hii tabia ya mtu kutaka kulizungumzia suala au jambo ambalo hana ufahamu nalo kabisa,ni vyema ukahakikisha kuwa unazo habari sahihi juu ya kitu/jambo lolote kabla ya kuamua kulizungumzia hilo jambo.
 
Tatizo kubwa la huo uhuni huko Afrika kusaini ni ajira. Huko Afrika kusini kuna maendeleo ya vitu kuliko ya watu, hali hiyo ndio inaleta msongo wa mawazo kwa wale wanaoishi kwa ufukara mkubwa. Hatari hiyo iliyo Afrika kusaini huenda ikatokea hapa nchi hata kwa namna tofauti, wananchi hawana ajira wakati pesa nyingi inapelekwa kwenye miradi ya maendeleo na wenye ajira mishahara yao haipandi, hivyo maisha kuzidi kuwa magumu, huku viongozi hawajali kwani wao wana mishahara mikubwa.
Ni kweli ajira tatizo kubwa na ndio chanzo cha vurugu za SA.
Cha kushangaza kule ubepari umejichimbia mizizi, sekta binafsi ndio imeshika uchumi huku ikitegemewa kuzalisha ajira nyingi.
Huku kwetu tunaambiwa sera za kijamaa ndio zina dhorotesha sekta binafsi na kusababisha ukosefu wa ajira kuwa mkubwa.
Sasa kama ni hivyo tatizo la ajira hasa ni nini?
 
Tatizo kubwa la huo uhuni huko Afrika kusaini ni ajira. Huko Afrika kusini kuna maendeleo ya vitu kuliko ya watu, hali hiyo ndio inaleta msongo wa mawazo kwa wale wanaoishi kwa ufukara mkubwa. Hatari hiyo iliyo Afrika kusaini huenda ikatokea hapa nchi hata kwa namna tofauti, wananchi hawana ajira wakati pesa nyingi inapelekwa kwenye miradi ya maendeleo na wenye ajira mishahara yao haipandi, hivyo maisha kuzidi kuwa magumu, huku viongozi hawajali kwani wao wana mishahara mikubwa.
Ningeshangaa usingelinganisha na TZ . Hasira zako na Magufuli nadhani hata kivuli chake unatakani ukichape fimbo
 
Ni kweli ajira tatizo kubwa na ndio chanzo cha vurugu za SA.
Cha kushangaza kule ubepari umejichimbia mizizi, sekta binafsi ndio imeshika uchumi huku ikitegemewa kuzalisha ajira nyingi.
Huku kwetu tunaambiwa sera za kijamaa ndio zina dhorotesha sekta binafsi na kusababisha ukosefu wa ajira kuwa mkubwa.
Sasa kama ni hivyo tatizo la ajira hasa ni nini?

Hata hapa ajira ndio mbaya zaidi isipokuwa watu wana uoga wa kipaji na ni kama wamekubaliana na umasikini, ila kwakuwa kuna elimu duni ndio maana unaona watu hawafunguki. Hao watu wa Afrika kusini wengi wana elimu bora ndio maana wanaonyesha hisia zao mara kwa mara. Hapa watu bei za bidhaa zinapanda maradufu tena kwa kiki za kisiasa na watu hawachukui hatua zaidi ya kulalamika, huko Afrika kusini huo ujinga hamna.
 
Kwahiyo kabla hawajafanya ule udhalimu huwa wanaanza kukuuliza uoneshe passport yako ilipogongwa ili kujiridhisha kwamba uliingia kwa njia za halali, au?
Ukisoma kwa munkari utakuja na conclusions kama hizo. Huu ni utafiti wangu kwa niliyojionea wenye visits kadhaa nilizofanya.
 
Back
Top Bottom