Congo
JF-Expert Member
- Mar 13, 2008
- 2,064
- 2,301
Mwishoni mwa wiki iliyopita kulitokea vurugu kubwa shule ya Sekondari St. Mathew's kule Kongowe. shule hii inamilikiwa na bwana Mtembei. Sababu ya vurugu hizi ni vijana waliomaliza kidato cha sita waliokuwa wanadai fedha zao za "caution money".
Kiasi cha shilingi 30,000 kila mmoja. Walipoufuata uongozi wa shule (na hatimae mwenye shule) wakanyimwa fedha hizo. Vurugu hizo zilisababisha Polisi kupelekwa pale shuleni na mpaka leo wako pale. Pia masomo ya shule nzima yamesimama kwa maelezo kuwa walimu walichomewa vifaa, vitabu na madaftari yao ya kufundishia.
Baadhi ya wanafunzi wamechukuliwa na wazazi wao kwa kuwa hakuna maji na chakula kinachelewa kupikwa.
Cha, ajabu, sikuona chombo chochote cha habari kikiripoti habari hiyo. Habari leo waliripoti Jumatano ukurasa wa tatu. Najiuliza, ilikuwaje vyombo vingine vya habari visiripoti habari hiyo?
Suala la kurudishiwa "caution money" kwa mwanafunzi aliyemaliza shule ni haki yake ili mradi tu awe hakufanya uharibifu wowote wa vifaa vya shule kabla. Vipi hawa wanyimwe mpaka kutokee mzozo uliosababisha vurugu?
Labda kuna mwenye habari zaidi na majibu mwafaka.
Kiasi cha shilingi 30,000 kila mmoja. Walipoufuata uongozi wa shule (na hatimae mwenye shule) wakanyimwa fedha hizo. Vurugu hizo zilisababisha Polisi kupelekwa pale shuleni na mpaka leo wako pale. Pia masomo ya shule nzima yamesimama kwa maelezo kuwa walimu walichomewa vifaa, vitabu na madaftari yao ya kufundishia.
Baadhi ya wanafunzi wamechukuliwa na wazazi wao kwa kuwa hakuna maji na chakula kinachelewa kupikwa.
Cha, ajabu, sikuona chombo chochote cha habari kikiripoti habari hiyo. Habari leo waliripoti Jumatano ukurasa wa tatu. Najiuliza, ilikuwaje vyombo vingine vya habari visiripoti habari hiyo?
Suala la kurudishiwa "caution money" kwa mwanafunzi aliyemaliza shule ni haki yake ili mradi tu awe hakufanya uharibifu wowote wa vifaa vya shule kabla. Vipi hawa wanyimwe mpaka kutokee mzozo uliosababisha vurugu?
Labda kuna mwenye habari zaidi na majibu mwafaka.