ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Sauti ya Msimamizi wa Uchaguzi inaonekana kuwa CCM wanaleta vurugu katika eneo la Embaseni baada kuona vijana wa CDM wapo ngangari kulinda kura... Imelazimu polisi kuingilia kati.
Alikuja mama ambae alieleza kuwa anakuja kumlipa wakala wa SAU, lakini akaelezwa kuwa hapo kituo cha Uchaguzi hakukuwa na wakala huyo..akatakiwa kuondoka. Jioni hii akaja tena akiwa na Vijana wa Kimasai kwenye gari,akamwita msimamizi wa CCM pembeni na kuongea nae kwa muda. Msimamizi wa Uchaguzi akamtaka aondoke, mara vijana aliokuwa nao kwenye gari wakaanza kuwarushia mawe wenzao wa CDM ambao walikuwa mita mia zaidi toka eneo la kupiga kura..ndipo vurugu za kufa mtu zikaibuka, vijana wale wakakimbia na gari wakamwancha yule mama ambae baadae aliwekwa chini ya ulinzi na polisi..Vijana wa CDM wakamdhibiti vurugu zikaendelea mpaka imelazimika Msimamizi wa Uchaguzi wa Kituo kutoa taarifa kwa OCD kwa msaada.
Kwa mujibu wa ITV (Sauti ya Renatus Mtabuzi)
Alikuja mama ambae alieleza kuwa anakuja kumlipa wakala wa SAU, lakini akaelezwa kuwa hapo kituo cha Uchaguzi hakukuwa na wakala huyo..akatakiwa kuondoka. Jioni hii akaja tena akiwa na Vijana wa Kimasai kwenye gari,akamwita msimamizi wa CCM pembeni na kuongea nae kwa muda. Msimamizi wa Uchaguzi akamtaka aondoke, mara vijana aliokuwa nao kwenye gari wakaanza kuwarushia mawe wenzao wa CDM ambao walikuwa mita mia zaidi toka eneo la kupiga kura..ndipo vurugu za kufa mtu zikaibuka, vijana wale wakakimbia na gari wakamwancha yule mama ambae baadae aliwekwa chini ya ulinzi na polisi..Vijana wa CDM wakamdhibiti vurugu zikaendelea mpaka imelazimika Msimamizi wa Uchaguzi wa Kituo kutoa taarifa kwa OCD kwa msaada.
Kwa mujibu wa ITV (Sauti ya Renatus Mtabuzi)
Ngilisho Sunrise Radio anaripoti:
Kituo Embasema kata Kikatiti:
Hali ni tete kabisa, gari lilokuwa na katibu mkuu wa ccm mkoa wa arusha Rosemery Chatanda lashambuliwa na wafuasi wa cdm gari hilo lilikuwa linalazimisha kuingia ndani ya kituo hicho.