Vumbi kesi ya Dk. Slaa

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,011
Vumbi kesi ya Dk. Slaa

na Mustafa Leu
Tanzania Daima

UTATA unaotokana na tofauti za takwimu umeibuka mahakamani wakati kesi ya kupinga ushindi wa Mbunge wa Karatu, Dk. Willbrod Slaa (CHADEMA) ilipokuwa ikiendelea kusikilizwa jana.
Kuibuka kwa utata huo kulikuja baada ya aliyekuwa wakala wa jimbo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Joseph Hayim, kuwasilisha takwimu alizodai kuwa ni za matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005 zinazotofautiana na zile za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Katika kesi hiyo ambayo wanachama watatu wa CCM wanapinga ushindi wa Dk. Slaa, wakala huyo anadaiwa kuwasilisha majina ya baadhi ya vituo vya kupigia kura ambavyo havimo katika orodha ya vituo rasmi vya NEC.

Wakala huyo ambaye ni shahidi wa walalamikaji, aliiambia Mahakama Kuu Kanda ya Arusha inayosikiliza kesi hiyo kwamba, matokeo katika kituo cha Shangit B yaliyoandaliwa na CCM yalikuwa hayafanani na matokeo sahihi ya NEC.

Hayim alidai mahakamani hapo kuwa kutokana na tofauti hiyo ya matokeo kati ya yale ya NEC na aliyoletewa na mawakala wa chama hicho kutoka vituoni ni vigumu kujua ni mgombea gani wa ubunge kati ya yule wa CCM au CHADEMA (Slaa) alishinda.

Shahidi huyo alidai pia kuwa, katika kituo kingine cha Mamsai kulikuwa na tofauti katika fomu za CCM na zile za NEC na hivyo kuleta utata wa kutojulikana mshindi halisi.

Katika kituo kingine cha Njia Panda, Hayim alidai hakukuwa na kituo kama hicho, ingawa katika fomu za CCM zimeonyeshwa kilikuwepo na karatasi zake za malalamiko ziliwasilishwa kwa bahati mbaya mahakamani kama kielelezo.

Aliiambia mahakama hiyo kuwa yeye alipokea karatasi za matokeo kutoka kwa mawakala wa Chama chake Cha Mapinduzi ambazo zilionyesha kuwepo kwa kituo cha Njia Panda, lakini ukweli ni kuwa kituo hicho hakikuwepo.

Alipoulizwa na Wakili Tundu Lissu, anayemtetea Dk. Slaa kuhusu taarifa za kituo kimoja kuwa na fomu mbili za matokeo, shahidi huyo alisema kuwa swali hilo hawezi kulijibu na alikuwa anaiachia mahakama, kwani kila kituo kilikuwa na fomu moja ya matokeo na fomu 20 za CCM zilizoongezeka zilipelekwa mahakamani kwa bahati mbaya.

Akiendelea kutoa ushahidi, alisema kuwa katika kituo cha Getamol, matokeo yalibadilishwa na yale ya CCM yakawekwa kama ya CHADEMA na ya CHADEMA yakaandikwa kama ya CCM, na taarifa ya msimamizi wa uchaguzi inaonyesha kuwa CHADEMA ilishinda kwa kura 79 katika kituo hicho.

Alipotakiwa kutoa ufafanuzi ni fomu zipi basi za matokeo zipokelewe na mahakama kama kielelezo, alisema yeye amezileta mahakamani ili mahakama ndiyo iangalie.

Shahidi huyo alikiri kuwapo kwa fomu ambazo ziliandaliwa na CCM zinazoonyesh matokeo, ingawa hazina majina na sahihi za mawakala, na nyingine zilizowasilishwa mahakamani hapo kwa makosa ambayo yalitokea katika vituo vya kupigia kura wakati wa kuzijaza.

Hayim aliiambia mahakama hiyo kuwa mawakala wote 253 wa CCM hawakujaza fomu za malalamiko ya matokeo, ingawa walikuwa na haki ya kufanya hivyo kupitia fomu namba 16 inayotolewa na msimamizi wa uchaguzi kwa madai kuwa walinyimwa.

Alidai pia kuwa katika matokeo hayo, CCM iliandaa taarifa yenye kuchanganya kura za madiwani na kuzifanya kuwa ndizo za wabunge.

Kuhusu hilo, alieleza kuwa, walalamikaji wenzake walibadilisha herufi moja katika fomu kwenye kituo cha Mango'ra kwa kuongeza herufi A, badala ya ile ya awali, ambapo hakuna herufi hiyo, na taarifa yake aliyoiandaa ilikuwa haina muhuri wa msimamizi na akaiomba mahakama iikubali.

Aliiambia mahakama kuwa alipokea fomu hizo Novemba 25 mwaka 2006, na siku iliyofuata wakafungua kesi. Shahidi huyo ataendelea kutoa ushahidi wake leo.
 
Hii,
Ni vyema iunganishwe na ile ilo tangulia, 'kessi ya Slaaa ushahidi ni wa kutungwa' ili tusipoteze uelekeo.. Admin. please!
 
Posted Date::12/11/2007
Shahidi kumpinga Slaa akiri fomu za madai zina utata

Na Mussa Juma, Arusha.
Mwananchi

KESI ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa Jimbo la Kararu, iliendelea jana ambapo shahidi wa kwanza wa upande mashitaka, Joseph Haimu aliimbia mahakama kuwa ni baadhi tu ya waliokuwa mawakala wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) walalamikia matokeo hayo. CCM ilikuwa na mawalaka 253.

Katika uchaguzi huo, Mgombe wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Wilibrod Slaa alimshinda mgombea wa CCM Patrick Tsere.

Akihojiwa na Wakili wa Utetezi, Tundu Lissu Shahidi huyo pia alikiri kuwa fomu za matokeo ambazo wamewasilisha mahakamani hapo baadhi matokeo yake �yamegushiwa�.

Sehemu ya mahojiano baina ya Lissu na shahidi huyo ambaye ni mmoja ya waliofungua kesi ya kupinga matokeo hayo yalikuwa hivi.

Wakili: katika uchaguzi wa Karatu ni kweli CCM ilikuwa na mawakala katika vituo vyote.

Shahidi: Ndio

Wakili: Je ni kweli kuwa CCM ilikuwa na mawakala 253 na kati yao ni Emanuel Bura ambaye ni mmoja wa walalamikaji katika kesi hii.

Shahidi: Ni kweli.

Wakili: Je, katika uchaguzi wa Karatu kuna wakala ambaye alijaza fomu za kulalamikia matokeo kwenye fomu ya Tume ya Uchaguzi namba 16.

Shahidi: Hakuna ila nina sababu kwani walinyimwa fomu.

Wakili: Katika malalamiko yenu ya kupinga matokeo mbona hili halipo kama mawakala wote walinyimwa fomu na msimamizi wa uchaguzi.

Shahidi: Kimya

Awali Lissu aliwasilisha mahakamani hapo vielelezo vya fomu za matokeo ambazo zimewasilishwa mahakamani hapo ambazo zinabadilishwa matokeo.

Wakili: Naomba utusomee vielelezo P255 na D257 ambazo ni fomu za matokeo na je ni za kituo kimoja au la.

Shahidi. Ni za kituo kimoja cha Mang�ola NTC, P2555 CCM kura 172, CHADEMA kura 122 na D 257 CCM kura 122 na CHADEMA kura 172.

Wakili: Je, ni kweli matokeo yamepinduliwa.

Shahidi: Ndio

Wakili: Je, haya ni matokeo ya kituo kimoja

Shahidi: Ndio

Wakili: Matokeo ya fomu P255 yamesainiwa na yana jina la wakala wa Chadema na jina lake

Shahidi: Hayajasainiwa na wakala na jina halionekani vizuri.

Jaji: Robert Makaramba anayesikiliza kesi anachukuwa fomu na kuitazama anaguna

kisha anamrudishia Lissu.

Wakili: Je matokeo ya D257 ambayo ndio ya tume ya uchaguzi yamesainiwa na mawakala

Shahidi Ndio.

Wakili: Jina lake ni nani?

Shahidi: Abasi Maoi

Wakili: Sasa mlipoleta fomu mbili za kituo kimoja mnataka jaji afuate ipi.

Shahidi: Ni uamuzi wa mahakama

Wakili: Msomee jaji fomu hizi, P 254 na D 258 ambazo ni za kituo kimoja cha Kandel C, Barai

Shahidi: P 254 CCM kura 136 na CHADEMA kura 115 na D254, CCM 115 na CHADEMA 136.

Wakili: Ebu tusomee orodha ya matokeo yenu ya kifupi ya kata zote katika kielelezo chenu namba P 256 kwa kituo hicho hicho.

Shahidi: CCM kura 115 na CHADEMA kura 36.

Wakili: Je, hapa tena jaji afuate fomu ipi na inaonekana tena mmepunguza kura 100

za CHADEMA na katika malalamiko yenu mnadai mlishinda kwa tofauti ya kura 177?

Shahidi: Mahakama itaamuwa.

Wakili: ni nani ambaye amepindua matokeo haya?

Shahidi :Sijui.

Wakili: Msomee jaji fomu D261 , D 256 na P 253. Je, matokeo yanafanana?

Shahidi: Ndio, isipokuwa kwenye p253 neno A limeongezwa.

Jaji: Wewe jibu swali unaloulizwa, unajua hapa ni sawa na polisi lazima uwe makini na maelezo yako.

Wakili: Ni nani kaongeza?

Shahidi:sijui

Kesi hiyo ambayo inavuta umati wa watu inaendelea leo na shahidi huyo ataendelea kuhojiwa na wakili Lissu.

Katika kesi hiyo, Haimu na wenzake wanadai kuwa uchaguzi haukuwa wa haki kwani taratibu kadhaa zilikiukwa ikiwepo kuwepo fomu feki na pia kama matokeo yangehesabiwa vizuri CCM ilishinda ubunge kwa tofauti ya kura 177.
 
Kumbe wakati mwingine wezi ni wau butu kabisa!

Wakili Lisu ni shujaa wa kujenga demokrasia. Aibu kuu kwa wezi wa kura. Naona wataumbuliwa sana kwenye kesi hii.
 

Naona media inashirikiana vizuri na Tindu Lissu kama walivyokuwa wanafanya kwa Dr M. Lamwai.

Tukumbuke tu kuwa haya magazeti yanaandika wanachotaka kutuonyesha...ningependa kujua pia wakili wa walalamikaji naye anauliza na kujibiwa majibu...ila kwa mambo yaliyoandikwa mpaka sasa nashindwa kujua ni juha gani ndani au nje ya CCM aliyeona hii kesi ina maslahi mazuri kwa CCM.

Ila kesi inaendelea tungoje tuone uamuzi wa mahakama.
 
Yebo*2 wakili wa walalamikaji hawezi kuhoji sasa kwani mashahidi ndio wameletwa ili kutetea upande wa ulalamikaji.

Mwanasheria wa upande wa utetezi ndio anahoji mashahidi sasa , nami nasubiri kuona kinachoendelea mkuuu.
 
I am beginning to wonder whether Dr. Slaa is not the smoothest political operator in the whole country at this material time. The man is shrewd, very shrewd, lucky, and above all, bold. Having reduced Sumaye to the a mere amateur, he now has the whole upper echelon of the CCM leadership firmly in his sights. I sympathize with these CCM guys for it is indeed very bad news to have Wilbrod Slaa coming after you.

Slaa was infinitely wise in his choice of advocate. In Tundu Lisu, he has found "a man after his own heart". By the time Lissu and Slaa are through with this case, CCM will have been bloodied and humiliated beyond belief.

Now I can see, at last, why those like Chenge and Balali who know better have not dared to take Slaa to court. Those who were foolish enough to proceed with litigation against Slaa will pay a heavy price for their ill conceived action.
 
Mwalimu, hakuna aliyeenda mahakamani! Bomani na wenzake waliwashauri wasifanye hivyo bora waishi na hiyo aibu tu kwa sasa.
 
Sasa kwanini tunakula pumba wakati mchele upo? Kwa nini nchi yenye Slaa itawaliwe na Lowasa?

Ili tuendelee, tunahitaji viongozi wazuri. Kuna wakati Kawawa alisema "Watanzania uchumi mnao lakini mmeukalia". Naona hata viongozi tunao lakini tumebaki tunakumbatia wezi na wanyanganyi. Mimi naona kama Slaa angekuwa Rais basi hili taifa lingeacha kuporomoka na kuanza kusimama.

Kwanini Slaa asiwe Rais wa Tanzania?
 
.....................Naona hata viongozi tunao lakini tumebaki tunakumbatia wezi na wanyanganyi. Mimi naona kama Slaa angekuwa Rais basi hili taifa lingeacha kuporomoka na kuanza kusimama.

Kwanini Slaa asiwe Rais wa Tanzania?

Yes viongozi mbadala tunao ila wamegawanyika...........ni vyema kwao (Upinzani) wakajipanga kwa pamoja na kuwa wata-form Government ya ushirikiano ya vyama vya Upinzani

Yes
Rais: Dr. Slaa
Makamu: Maalim Seif
PM .........(hapo jazeni wenyewe)......Mbatia possible candidate
1.Naibu PM na Waziri wa mambo ya Ndani: Mrema
2.Fedha, Mipango, Uwekezaji na Uchumi: Ibrahim Lipumba
3.Waziri wa Sheria na Mwanasheria Mkuu: Prof Issa Shivji
4.Waziri wa Nishati na Madini: Tundu Lissu
5.Afya na Maendeleo ya Jamii:
6.Utalii na Maliasili na Mazingira: Zitto Kabwe
7.Local Governemnt: Freeman Mbowe
8.Viwanda Biashara Kilimo na Masoko:
9.Kazi na Utumishi:
10.Vijana na Michezo na Utamaduni:
11.Elimu:
12.Ulinzi na Usalama:
13. Mawasiliano na Miundombinu:
14. Ardhi na Maendeleo ya Makazi:

nafikiri hizo ndio wizara zinazotakiwa ila watu wa upinzani wengine siwajui
 
Back
Top Bottom