Hili suala la mlima Kilimanjaro limeendeshwa kitapeli zaidi. Kwanza watu tunaambiwa tuupigie mlima kura bila kuelimishwa ni kwa nini tunafikiri unapaswa kuwamo katika maajabu 7. Pili, sh. 300 zinazokatwa zinaenda kwa nani na kwa nini zinakatwa kimyakimya? Na je, hawajui kwa kutoza hela wanapunguza kura?
Ikiwa mwisho ni Tarehe 11 Novemba basi Mlima wetu umweshindwa, badala yake mlima Meza umeingia kwenye maajabu saba. Swali ni je ikiwa zoezi hili liliaza tangu mwaka 2009 mbona ni juzi tu ndio uhamasishaji umefanyika? zima moto itatutesa.
Mi nadhani huu ni uchakachuaji wa akili za watu, mlima kilimanjaro huwezi kuufananisha na mlima meza, hivi meza unasifa zipi? Hivi watu hawajui sifa za kilimanjaro mpaka ipigiwe kura? Tafuteni jinsi ya kutafuta fedha hapo mimi sidanganyiki.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.