Vodacom yaongoza kwa kutoza gharama kubwa za intaneti kwa wateja

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,499
9,279
Kwa mujibu wa taarifa ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ya robo ya mwaka inayoishia Septemba 2019 zinaonesha kuwa kampuni ya Vodacom Tanzania ndiyo inayoongoza kwa kutoza gharama kubwa zaidi ambapo hutoza TZS 205 kwa megabyte (MB) mteja anayotumia.

Wakati Vodacom ikitoza kiwango hicho, nafasi ya pili inashikwa na Zantel ambayo hutoza TZS 93 kwa kila MB, huku wateja wa Airtel na Tigo wanalipa sawa ambao gharama ya MB moja ni TZS 29.

Wateja wa Halotel wanalipa TZS 22 kwa MB, huku wateja wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) wanalipa TZS 10, wakati wateja wa Smile ndio wanaotozwa gharama ndogo zaidi ya TZS 5 kwa kila MB moja. Gharama zote hizi ni bila kodi, na zinazotwa endapo mteja hajajiunga kifurushi.

TCRA imeeleza kuwa gharama za vifurushi mitandao ya simu nchini haitofautiani sana, na kwamba vifurushi hivyo ambavyo vimekuwa vikitumiwa sana vimeleta unafuu wa gharama za matumizi ya simu kwa wananchi.

Taarifa hiyo ya TCRA inaonesha kuwa mteja anaweza kupata dakika moja ya kupiga simu, MB moja, na ujumbe mmoja kwa gharama kati ya TZS 21 hadi TZS 62 endapo atajiunga kifurushi.

Chanzo: TBC
 
Kuna mfanyakazi mmoja wa Vodacom aliwahi kuniambia kuwa wanatoza bei kubwa kufidia gharama za faini wanazotozwa.
 
hakuna kitu kinanikera kwenye voda kama ukitaka kuaccess account yako ya benk na kufanya miamala kama line ya simu haina salio huwezi kuingia, wakati mitandao mingine hata kama huna salio unaweza ku access account yako bila shida na kufanya miamala yako bure kabisa
 
Kuna mdau aliwahi kuleta uzi humu akielezea kuwa Tanzania inaongoza kwa bei kubwa ya internet (alisema GB 1 Ni 12000 kama sikosei) alishambuliwa vibaya mno. Ila leo TCRA wamethibitisha. Mfano hiyo 205/Mb ukizidisha mara 1024 ni sawa na 209,920/GB.
 
TCRA huwa nasema ni taasisi mbovu, wanatoa hizo Takwimu utafikiri raia wamewahi kulalamikia Bei kubwa za MB bila kujiunga na Kifurushi... Hivi watanzania wangapi hutumia internet bila kujiunga na Kifurushi , Hilo limekuwa tatizo tangu lini?


Tatizo la watanzania Ni Bei za vifurushi na vifurushi kuisha haraka na sio hizo Takwimu walizotuletea... TCRA fanyeni kazi inayogusa wananchi mnalipwa Kodi zetu Kama mishahara ,tutumikieni kadri ya kero tulizo nazo .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
TCRA huwa nasema ni taasisi mbovu, wanatoa hizo Takwimu utafikiri raia wamewahi kulalamikia Bei kubwa za MB bila kujiunga na Kifurushi... Hivi watanzania wangapi hutumia internet bila kujiunga na Kifurushi , Hilo limekuwa tatizo tangu lini?


Tatizo la watanzania Ni Bei za vifurushi na vifurushi kuisha haraka na sio hizo Takwimu walizotuletea... TCRA fanyeni kazi inayogusa wananchi mnalipwa Kodi zetu Kama mishahara ,tutumikieni kadri ya kero tulizo nazo .

Sent using Jamii Forums mobile app
Kumbe wametoa kabla ya kujiunga? Kweli hawa hamnazo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huu ndio mtandao ambao kw mujibu wa tcra ni wa gharama nafuu zaidi, do i need to believe TCRA?


2020-01-17.png
 
Sasa kinachoshangaza vodacom ni ingiza vocha sahau kujiunga ndani ya masaa 2 utakuta kihela kimechotwa kiko pungufu kikikaa siku nzima utakuta sh 23 tu uliza sasa jinu utakolo pewa utatafuta mtaalamu wa kutafsili maelezo wote mtashindwa
Halafu linakuja swala la gawio aisee utacheka sana , ni sh 50 hiyo sh 50 ukisema ukatoe kwa wakala utajibiwa huna kiasi vhochoye cha chochote cha kuweza kutoa .
VODACOM myandao unaongoza kwa uizi TANZANIA.
 
Gharama hizo ni endepo hujajiunga na kifurushi,ila wajue kwamba hata ukijiunga na kifurushi cha GB 10 unashangaa unaambiwa kifurushi chako kimeisha,utaona msg MB za kifurushi chako ziko chini ya 15MB mara paap zimeisha hata kama hujawasha data,swali najiuliza huwa wanazikusanyiwa wapi hz MB zetu hazijai tu siku wakatoa hata offer..
 
Kwa mujibu wa taarifa ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ya robo ya mwaka inayoishia Septemba 2019 zinaonesha kuwa kampuni ya Vodacom Tanzania ndiyo inayoongoza kwa kutoza gharama kubwa zaidi ambapo hutoza TZS 205 kwa megabyte (MB) mteja anayotumia.

Wakati Vodacom ikitoza kiwango hicho, nafasi ya pili inashikwa na Zantel ambayo hutoza TZS 93 kwa kila MB, huku wateja wa Airtel na Tigo wanalipa sawa ambao gharama ya MB moja ni TZS 29.

Wateja wa Halotel wanalipa TZS 22 kwa MB, huku wateja wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) wanalipa TZS 10, wakati wateja wa Smile ndio wanaotozwa gharama ndogo zaidi ya TZS 5 kwa kila MB moja. Gharama zote hizi ni bila kodi, na zinazotwa endapo mteja hajajiunga kifurushi.

TCRA imeeleza kuwa gharama za vifurushi mitandao ya simu nchini haitofautiani sana, na kwamba vifurushi hivyo ambavyo vimekuwa vikitumiwa sana vimeleta unafuu wa gharama za matumizi ya simu kwa wananchi.

Taarifa hiyo ya TCRA inaonesha kuwa mteja anaweza kupata dakika moja ya kupiga simu, MB moja, na ujumbe mmoja kwa gharama kati ya TZS 21 hadi TZS 62 endapo atajiunga kifurushi.

Chanzo: TBC
Duu! Ni muhimu kwa vyombo vya habari kuwahabarisha wananchi zaidi ili wengi waufahamu utapeli unaofanywa na VODA! Ni wakati sasa wa kuwalazmisha voda kutambua kuwa wameshawakamua wateja wao vya kutosha! Utakuta unanunua kifurushi cha Internet ambacho unaambiwa ni cha masaa 24, lakini baada ya nususaa tu unaanza kutumiwa vijimeseji ....Oh! Ndugu mteja umetumia 90% ya kifurushi chako , kununua kifurushi kingine piga.....!???? Wizi Mtupu! Si huko tuu, bali pia ni voda hawahawa ndio waliojaza wezi mtandaoni kupitia utitiri wa vimichezo vya kamari vya kubeti! Nashauri serikali kupitia mamlaka husika ingeichunguza kampuni hii kwani imeshapiga pesa za wananchi vya kutosha!
 
hakuna kitu kinanikera kwenye voda kama ukitaka kuaccess account yako ya benk na kufanya miamala kama line ya simu haina salio huwezi kuingia, wakati mitandao mingine hata kama huna salio unaweza ku access account yako bila shida na kufanya miamala yako bure kabisa
Sio wewe tu Mkuu ,Mimi ndo maana natumia airtel Ku access menu za bank . Voda bila credit haingii kabisa .
 
Back
Top Bottom