Vodacom watazidi kuanguka kwa sababu ya kiburi chao

Nimeona wameshindwa kuendelea kudhamini premier league,sababu kubwa ikiwa ni hali mbaya ya kampuni.

Mkataba uliwataka wawe wanatoa bilioni 3 kila mwaka.Hata hivyo kwa msimu huu waliomba eti watoe milioni 500 tu kisha zilizobaki zingetolewa msimu ujao.

Kwa mawazo yangu hawa jamaa kiburi na janja janja yao ndivyo vimewadidimiza sana.Mimi ni mmoja wa niliokuwa wateja wao wakubwa nikitumia zaidi ya laki 3 ya kununua vifurushi mbali mbali kwa mwaka.Mimi ni mtu wa hali ya kawaida sana unaweza kusema ya chini au kati.Lakini mara nyingi hata ukinunua kifurushi cha saa 24 huwa hazifiki.Unakuta bado una dakika,lakini unaambiwa muda wa kifurushi umeisha nunua kifurushi kingine.

Hali hiyo imetukimbiza wengi kwani utapeli huu ulikuwa umekithiri sana kwenye hii kampuni.Wasitarajie msimu ujao watafanya vizuri kwani kipindi cha mpito wa kubadilika huchukua muda mrefu.Hadi wateja wavumilivu waanze kuisemea vizuri tena kampuni.

Binafsi nilitaka kuifufua line yangu ya Voda kwa kununua simu ndogo mwezi ujao ila kwa taarifa hizi inaonekana wateja wengi wanawakimbia.Inawezekana hawajajifunza.Bado wana mambo ya ukaburu hata kwenye biashara
Walionunua hisa mwaka wa 5 huu hakuna gawio zaidi ya elfu kumi tu, na hisa zao haziuziki.
VODA imeuliwa na Rosta
 
Laini inayotumika mara kwa mara ina vifurushi vya kiutopolo kuliko isiyotumika mara kwa mara. Sijui voda walifikiri vipi hapa yaani mteja wa muda mrefu anapandishiwa vifurushi wakiamini hawezi kuhama halafu eti laini mpya au isiyotumika mara kwa mara vifurushi bei chee.

Huo ndio utopolo wa voda wa kutomthamini mteja wa muda mrefu wakiamini hawezi kuhama lakini kiuhalisia kuhama ni rahisi tu.
Ndo maana nimetupa laini yao
 
Nilinunua 9gb kwa 20,000 ya mwezi. Nilijiunga na meseji ikaingia kua nishajiunga. Simu iko idle ndani ya masaa matatu ( three hrs) ikaingia meseji bando langu limeisha!
Una Moyo sana, zantel unapewa GB 20 Kwa hiyo hela
 
Voda hawafai,
tigo wanajiuza so wanataka pesa hata kwa dhulma,
halotel speed kinyonga,
zantel imekaa kimwinyi sana
Ttcl hawaeleweki nini wanafanya
Airtel nao hawana ubunifu

Sijui twende wapi au Bahkresa aanzishe kampuni ya mawasiliano?
 
aisee msihamishie machungu yenu ya vifurusi vya jero kwenye hili.

Biashara ya mawasiliano sio bishara ya biriani.
 
Back
Top Bottom