Vodacom Tanzania yapata CEO Mpya, Hisham Hendi raia wa Misri

Mukulu wa Bakulu

JF-Expert Member
Aug 12, 2014
4,052
12,904
IMG_20190327_072254.jpg

Waafrika alieturoga alituweza sana.

Mwaka jana Vodacom ikateua raia mwanamama mmoja kutoka Kenya kuja kua mkurugenzi wake, maneno yakawa maneno kua kwani tumekosa mtanzania wa kushika hizo nafasi na mambo kede kede, serikali ikamnyima kibali cha kazi. Dada wa watu akaendelea na maisha yake huko kwao Kenya.

Sasa Vodacom wameteua mwarabu kutoka Misri kua mkurugenzi wake, zile kelele za mwaka jana hazisikiki tena, maana yake hatutaki waafrika wenzetu ila tunataka watu wenye ngozi nyeupe. Kwanza tunaweza kumnyima mkenya kibali cha kufanya kazi Tanzania ila tukampa mwarabu wa Misri, sijui akili za wapi hizi.

Kwa hiyo ikifika kwa ngozi nyeupe hadithi za wazawa zinakufa, ila ikiwa ni mweusi mwenzetu hadithi za wazawa wapewe fursa ndio zinaibuka.

Binafsi hua sikubaliani na hoja ya uzawa, kwenye ulimwengu ulioendelea watu wenye uwezo binafsi wanataftwa kutoka kila mahali wakafanye mabadiliko na kuongoza taasisi za nchi nyingine. Uingereza ilimkodi Gavana wa benki ya Canada ili awe Gavana wao awasaidie kurekebisha uchumi, mkuu wa Google ni mhindi na mifano iko mingi.

Hoja yangu ni kwamba, kwa nini mkenya tulimkatalia kwa hoja ya uzawa alafu tumekubali mwarabu wa Misri?
 
Huyo unayemuita "Mwarabu" ni raia wa nchi gani? coz ukisema yule mama alikua ni "Mkenya" ina maana ni raia wa Kenya,tatizo lako ni uraia wa mtu au rangi ya ngozi? nadhani kuna vitu viwili unachanganya aidha kwa kutokujua au kwa msukumo wa chuki ya ubaguzi wa rangi.
Aisee ni kwamba umeruka mistari ya uo uzi ama unakingine cha zaidi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo unayemuita "Mwarabu" ni raia wa nchi gani? coz ukisema yule mama alikua ni "Mkenya" ina maana ni raia wa Kenya,tatizo lako ni uraia wa mtu au rangi ya ngozi? nadhani kuna vitu viwili unachanganya aidha kwa kutokujua au kwa msukumo wa chuki ya ubaguzi wa rangi.
Sio raia wa tanzania. Ni raia wa egypt. Sasa umefaham. Ngoz nyeusi haswa waswahili tunawashobokea waarab sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hongera kwa bwana mdogo Hisham Hendi. Ila huo ndio utakuwa mwisho wa career yake after three years.
Voda com dont believe that an MD will still perform after three yrs. So he shouldnt expect a contract renewal after three yrs.
Historically, the recent past two Vodacom MDs are on retirement leave.
Huwezi toka Voda ukaenda tena uswahilini kuajiriwa kama sijui meneja wa nini! Huu ndio mwisho wa career. Akitoka hapo akawe mkulima tu.
 
View attachment 1054930
Waafrika alieturoga alituweza sana.

Mwaka jana Vodacom ikateua raia mwanamama mmoja kutoka Kenya kuja kua mkurugenzi wake, maneno yakawa maneno kua kwani tumekosa mtanzania wa kushika hizo nafasi na mambo kede kede, serikali ikamnyima kibali cha kazi. Dada wa watu akaendelea na maisha yake huko kwao Kenya.

Sasa Vodacom wameteua mwarabu kutoka Misri kua mkurugenzi wake, zile kelele za mwaka jana hazisikiki tena, maana yake hatutaki waafrika wenzetu ila tunataka watu wenye ngozi nyeupe. Kwanza tunaweza kumnyima mkenya kibali cha kufanya kazi Tanzania ila tukampa mwarabu wa Misri, sijui akili za wapi hizi.

Kwa hiyo ikifika kwa ngozi nyeupe hadithi za wazawa zinakufa, ila ikiwa ni mweusi mwenzetu hadithi za wazawa wapewe fursa ndio zinaibuka.

Binafsi hua sikubaliani na hoja ya uzawa, kwenye ulimwengu ulioendelea watu wenye uwezo binafsi wanataftwa kutoka kila mahali wakafanye mabadiliko na kuongoza taasisi za nchi nyingine. Uingereza ilimkodi Gavana wa benki ya Canada ili awe Gavana wao awasaidie kurekebisha uchumi, mkuu wa Google ni mhindi na mifano iko mingi.

Hoja yangu ni kwamba, kwa nini mkenya tulimkatalia kwa hoja ya uzawa alafu tumekubali mwarabu wa Misri?
Suala LA Dada wa Kenya,na msuguano wa Kenya na TZ,ni kubwa kuliko unavyolifahamu,
Kwanza hatuna Vita ya kiuchumi kati yetu na Misri,tuna vita ya kiuchumi kati yetu na Kenya,unajua kilichotokea kwenye kiwanda cha General Tyre?watu waliingia pale kijasusi,wakashika uongozi,wakahujumu kiwanda,kikafa,mitambo ikahamishiwa Kenya,sasa HV ni Yana,sio General tyre tena,
Ukiruhusu kampuni kubwa kama Vodacom,iwe na CEO kutoka nchi,ambayo,MNA ugomvi nayo wa kiuchumi,ikihujumiwa uchumi wa nchi utayumba balaa,
Hivi vitu ni vikubwa sana.Kuna CEO wa Huawei,mchina,kashikwa kule CANADA,na USA inataka apelekwe USA,akashitakiwe kwa wizi wa tekinolojia,China na USA ni wapinzani kwenye uchumi,ukilala umeliwa.
Uwezi kusikia USA,imegombana na India,wakati wahandisi na madakitari kibao kutoka India wanafsnya kazi kwenye vitengo nyeti pale USA.
Hatuna shida na Zambia,watu wake wamejaa Tazara,hatuna shida na SA,wala Uganda,lakini Kenya,tuna shida nao sana,wakipata nafasi,wanaweza kuifanya nchi hii soko LA bidhaa zao.
Unakumbuka ishu ya vifaranga?
Nashukuru Maghufuri kwenye vita ya kiuchumi,ameiwezea sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hoja iliyotolewa kwa wakenya Ni kua eti wana mtindo wa kuhujumu kampuni na brand za Tanzania...mfano bia ya ndovu na tusker...
Kwakweli hizo tuhuma ni za muda mrefu. But then vodacom si ya tanzania.. ni ya south africa.
Wether angekuja mkenya au lah still tupo pale pale.
Okay mkenya amekataliwa.. kaajiriwa mwarab.. wha next. Lini tutashika nafasi hizo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Suala LA Dada wa Kenya,na msuguano wa Kenya na TZ,ni kubwa kuliko unavyolifahamu,
Kwanza hatuna Vita ya kiuchumi kati yetu na Misri,tuna vita ya kiuchumi kati yetu na Kenya,unajua kilichotokea kwenye kiwanda cha General Tyre?watu waliingia pale kijasusi,wakashika uongozi,wakahujumu kiwanda,kikafa,mitambo ikahamishiwa Kenya,sasa HV ni Yana,sio General tyre tena,
Ukiruhusu kampuni kubwa kama Vodacom,iwe na CEO kutoka nchi,ambayo,MNA ugomvi nayo wa kiuchumi,ikihujumiwa uchumi wa nchi utayumba balaa,
Hivi vitu ni vikubwa sana.Kuna CEO wa Huawei,mchina,kashikwa kule CANADA,na USA inataka apelekwe USA,akashitakiwe kwa wizi wa tekinolojia,China na USA ni wapinzani kwenye uchumi,ukilala umeliwa.
Uwezi kusikia USA,imegombana na India,wakati wahandisi na madakitari kibao kutoka India wanafsnya kazi kwenye vitengo nyeti pale USA.
Hatuna shida na Zambia,watu wake wamejaa Tazara,hatuna shida na SA,wala Uganda,lakini Kenya,tuna shida nao sana,wakipata nafasi,wanaweza kuifanya nchi hii soko LA bidhaa zao.
Unakumbuka ishu ya vifaranga?
Nashukuru Maghufuri kwenye vita ya kiuchumi,ameiwezea sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hiyo habari ya kwamba Kenya waliiba mitambo General Tyre ni story story za vijiwe vya kahawa na mtu makini hutakiwa hata kuongelea hilo. Mitambo yenu ipo pale Arusha imetulia kama vitu vilivyoko museum usiwasingizie Wakenya.
 
Hongera kwa bwana mdogo Hisham Hendi. Ila huo ndio utakuwa mwisho wa career yake after three years.
Voda com dont believe that an MD will still perform after three yrs. So he shouldnt expect a contract renewal after three yrs.
Historically, the recent past two Vodacom MDs are on retirement leave.
Huwezi toka Voda ukaenda tena uswahilini kuajiriwa kama sijui meneja wa nini! Huu ndio mwisho wa career. Akitoka hapo akawe mkulima tu.
Ni kama sijakuelewa!
Kwa nini unasema ndio unakuwa mwisho wa career yake?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Suala LA Dada wa Kenya,na msuguano wa Kenya na TZ,ni kubwa kuliko unavyolifahamu,
Kwanza hatuna Vita ya kiuchumi kati yetu na Misri,tuna vita ya kiuchumi kati yetu na Kenya,unajua kilichotokea kwenye kiwanda cha General Tyre?watu waliingia pale kijasusi,wakashika uongozi,wakahujumu kiwanda,kikafa,mitambo ikahamishiwa Kenya,sasa HV ni Yana,sio General tyre tena,
Ukiruhusu kampuni kubwa kama Vodacom,iwe na CEO kutoka nchi,ambayo,MNA ugomvi nayo wa kiuchumi,ikihujumiwa uchumi wa nchi utayumba balaa,
Hivi vitu ni vikubwa sana.Kuna CEO wa Huawei,mchina,kashikwa kule CANADA,na USA inataka apelekwe USA,akashitakiwe kwa wizi wa tekinolojia,China na USA ni wapinzani kwenye uchumi,ukilala umeliwa.
Uwezi kusikia USA,imegombana na India,wakati wahandisi na madakitari kibao kutoka India wanafsnya kazi kwenye vitengo nyeti pale USA.
Hatuna shida na Zambia,watu wake wamejaa Tazara,hatuna shida na SA,wala Uganda,lakini Kenya,tuna shida nao sana,wakipata nafasi,wanaweza kuifanya nchi hii soko LA bidhaa zao.
Unakumbuka ishu ya vifaranga?
Nashukuru Maghufuri kwenye vita ya kiuchumi,ameiwezea sana.
Sent using Jamii Forums mobile app
1. Rudi shule uongeze maarifa. Huo ugomvi wa kiuchumi na Kenya ulianza lini?mawazo ya kimaskini na kijinga kama haya ndio yanaturudisha nyuma. Sasa kama waliiba GT ni kosa la wezi au uzembe wa serikali, kwani walikua wanapitia wapi walipokua wanaiba kwenda Kenya? Unalaum wezi au unalaum serikali kushindwa kulinda rasilimali zake? Mbona ilipovunjika EAC na wakenya kuchukua ndege zote hakukua na vita ya kiuchumi? Eti vita ya kiuchumi. Ndio yale yale tuna vita ya kiuchumi na mabeberu alafu tunaenda kuwaomba misaada.

2. Kwani Vodacom ni kampuni na mali ya Tanzania? Ikiibiwa Vodacom wewe inakuhusu nini?

3. Kuhusu Huawei hujui chochote, tafta vyanzo vingine vya taarifa vikujuze kuhusu mhasibu wa Huawei, Meng anaeshikiliwa Canada. Mambo ya kuiba teknolojia umeyatoa wapi?
 
Kama wanalipa vizuri katika miaka hiyo 3, hakuna haja ya ajira tena. Ajira ya nini wakati una mabilioni benki?

Hongera kwa bwana mdogo Hisham Hendi. Ila huo ndio utakuwa mwisho wa career yake after three years.
Voda com dont believe that an MD will still perform after three yrs. So he shouldnt expect a contract renewal after three yrs.
Historically, the recent past two Vodacom MDs are on retirement leave.
Huwezi toka Voda ukaenda tena uswahilini kuajiriwa kama sijui meneja wa nini! Huu ndio mwisho wa career. Akitoka hapo akawe mkulima tu.
 
1. Rudi shule uongeze maarifa. Huo ugomvi wa kiuchumi na Kenya ulianza lini?mawazo ya kimaskini na kijinga kama haya ndio yanaturudisha nyuma. Sasa kama waliiba GT ni kosa la wezi au uzembe wa serikali, kwani walikua wanapitia wapi walipokua wanaiba kwenda Kenya? Unalaum wezi au unalaum serikali kushindwa kulinda rasilimali zake? Mbona ilipovunjika EAC na wakenya kuchukua ndege zote hakukua na vita ya kiuchumi? Eti vita ya kiuchumi. Ndio yale yale tuna vita ya kiuchumi na mabeberu alafu tunaenda kuwaomba misaada.

2. Kwani Vodacom ni kampuni na mali ya Tanzania? Ikiibiwa Vodacom wewe inakuhusu nini?

3. Kuhusu Huawei hujui chochote, tafta vyanzo vingine vya taarifa vikujuze kuhusu mhasibu wa Huawei, Meng anaeshikiliwa Canada. Mambo ya kuiba teknolojia umeyatoa wapi?
Mkuu hivi EAC imevunjika eeh???

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom