Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Ninakerwa na message nyingi nazopata baada ya kununua bundle zangu via MPESA. Ukinunua bundle tu message si chini ya 6, kuna ya M-PESA, MPESA, VODACOM, TUZO POINT blah blah...... tafadhali sana itafutwe njia mbadala sio fair kutushambulia inbox na message zote hizi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanini mnacharge Ussd code kama za NMB, NBC, CRDB, AZAM NK? , isipokuwa zinazotumika kwenye mitandao wenu, mbona hizo code wenzenu Hawa charge kama tigo na airtel?

Sent from my Infinix-X551 using Tapatalk
 
Okey Here it It. Mwaka jana Vodacom waliniunganisha na huduma yao ya Game Lounge ambayo wala sikuwahi kujiunga nilipolalamika kwenye Twitter account yao wakasema kwamba nijitue, kumbuka kwamba kujitoa unalipia, nikajiuliza how comes kwamba waniunge wao bila mimi kutaka alafu kujitoa nijitoe mimi kwa hela? kujituoa ni TZS 150/= hii ni pesa ndogo kwa kuiangalia ila ni ujinga wa hali ya juu kuingia Gharama ambayo haina msingi.

MWAKA JANA:
Wakanitumia ujumbe kwamba huduma ya Game Imewekwa upya!. Nikaisoma sms nikatulia maana najua kujitoa ni hela.

Siku ya jumapili tarehe 3/02/2019 wakanitumia sms kwamba nimekatwa TZS kwa kujiunga kwenye Gemlounge ambayo sijawahi kujiunga. Sasa hapa Voda wameshasepa na TZS 500/=.

HAPA KUNA WIZI!. Kwenye tangazo la kwanza wanasema watakata tzs 50/= kwa wiki lakini kwenye sms ya makato naona hela iliyokatwa ni TZS 500/=.

This is unethical and unprofessional, Return my money.

Screenshot_20190203-161814.png

Screenshot_20190203-161814.png


LEO TENA wamelamba 150 Kwa ajili ya Hilohilo Game.
Screenshot_20190204-073717.png


VODACOM TANZANIA nahitaji Pesa zangu zirudi Haraka sina mchezo wa kujiunga na huduma ambazo situmii.
 
kuna mtu amenunua till ya mpesa kwa mtu na baadae imezingua na kuonyesha emmegence muda wote na hana detail za hyo lain ..pia kuna hela sijui mnaweza kumsaidia je ?
 
Hawa viumbe hawafai hata kidogo mimi nishatupa line kitaambo....ukiweka mb500 ukiingia jf tu nusu saa imekwisha,nipo airtel natanua hao voda wapuuzi
Supa uni,siku ambayo niliweka buku mbili(2000) nikajiunga na bando la chuo ndani yake unapata muda wa maongezi ya voda to voda na dakika chache mitandao mingine shindani na gb 1(mb 1000) za my surf internet lkn kilichonikuta siku within a few hours nikapewa sms notification kuwa mb zimekwisha.Sikuamini lkn ndio hvyo ilikuwa zimekwisha.
From that day no long Vodacom member period!,ilikuwa ni ujuzi wa kiwango cha juu sana .
Nilijaribu kuwapigia customer care huwezi amini nilikutana na utaratibu mreefu hadi kumfikia muhudumu alikuwa zamu, maelezo hayakujitosheleza kuhusu matumizi yngu au ni nni kilitokea hadi kufilisiwa mb zangu.
Vodacom asanteni kwa huduma zenu lkn mmi tena basi


Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
VODACOM M - PESA.
Hivi ni vigezo gani ninastahili ili kuanzisha Vodashop?
Naomba mnijibie hapa sio mnidirect Vodashop tena.


Nahitaji sana kufikia lengo hili.
 
Kuna wizi mkubwa kwa fedha za salio za wateja unaoendelea sasa hivi katika mtandao wa Vodacom.
Kwa vile hili si jungu bali ukweli nimisha report wizi huo katika kitengo cha malalamiko TCRA kwa hatua zaidi.

Nimeweka salio la Tsha 10,000 mchana wa leo kwa Mpesa ref Y23SY687 na baada ya muda mfupi nikakuta salio langu la maongezi ni sifuri.

Nikanunua vocha na kutumiwa tshs 10,000 na hela yote imekatwa tena.

Wateja wa Vodacom jihadharini, kuna mwizi kaingia mtandaoni Vodacom

UPDATE
=====
VODACOM wamefanya ustaarabu wa kunipigia baada ya kuona detail ya transaction hapo juu, na kuiona kwenye mtandao wa Jamiiforums.
Kimsingi wameapologise kwa mtafaruku uliotokea lakini wamenieleza nifike ofisini kwao kuona aian ya simu ninyotumia isije ikawa data apps ziko wazi.
Na kweli baada ya maongezi ya kuchunguza, mobile data setting ilikuwa ON, na mimeizima sasa.

Hata hivyo ni vema nitaenda kupata maelezo ya kuyeyuka kwa salio langu , karibu 20,000, kwa siku moja.
Wanabodi mtajulishwa inawezekana kuna wenye tatizo kama langu.

UPDATE
=====
Nimeonana na waheshimiwa sana wa Customer Care pale Block 4 Mlimani City.
Cha kusikitisha ni wao kushindwa kuchukua malalamiko yangu na kuyafanyia kazi, na hii ni licha ya kuwaelewesha kuwa hili tukio nalijawahi kunitokea na hii kuwa ni mara ya kwanza.

Hawa jamaa wa Customer Care ni kama mabalozi waliopewa jukumu la kusafisha kampuni ya VODACOM hata kama inanuka kwa wizi uliodhahiri.
Kitu ambacho hawajui ni kuwa nilifanya due diligence kupitia wafanyakazi ndani ya VODACOM walionidhihirishia kuwa kuna wafanyakazi wasio waaminifu ambao wana access na personal security settings za wateja.

Na wafanyakazi hao huwa "wapiga kishenzi" fedha za wateja.

Kwa kifupi mtu wa Customer Care ameshindwa kuniconvince na maelezo yake ya upotevu wa Tshs 20,000 katika mtandao wa VODACOM.
hureeeeeèeeeee nice one,wakiendelea kuzingua
tunahamia TTCL rudi nyumbani kumenoga.
 
vodacom Tanzania naomba kufahamishwa,hii offer ya DAR SUPA UNI Tsh2,500/= per week imesitishwa ktk line yangu au vipi maana siipati!
IMG_20190214_142509.jpeg


Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
 
vodacom Tanzania naomba kufahamishwa,hii offer ya DAR SUPA UNI Tsh2,500/= per week imesitishwa ktk line yangu au vipi maana siipati!View attachment 1022357

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
mkuu hata mimi nangojea wakujibu, kwasasa nimeiweka pembeni laini yao maana sasa huu ni upuuzi! wasiporudisha basi nahamia mtandao mwingine mazima uzuri ninazo laini za mitandao yote.
 
habari mimi nina shida na meseji niliyotuma 2018 tar 6 mwezi wa 10 siku ya jmos mida kama ya saa8 mchana nikiwa maeneo ya chang'ombe kwenda kwa General Manager wa kampuni fulani ya kutengeneza rangi iliyopo maeneo ya maduka mawili chang'ombe kama ushahidi wa kesi mahakamani
mimi nimeipoteza kwenye jumbe zilizotumwa( sent message)
nifanyeje ili nipate hiyo jumbe
 
Voda com ni wezi mno tena mno,leo nimejiunga mb500 nimeingia jamii forum ndani ya dk 6 wananiambia bando langu limekata nilikasirika mno .hivi mnachukulia pesa tunaokota sio??na sio mara ya kwanza kunifanyia huu uhuni...nimewachoka kesho nahamia airtel kwenye afadhali.
pumbavu sana
 
halafu hampo serious na kazi yenu, totally inaonesha nyinyi ni wababaishaji mara ya mwisho kuingia humu ilikuwa mwaka jana last seen ni 3 dec 2018..mnatatuaje malalamiko ya watu humu?? kulikuwa kuna umuhimu gani wa kuanzisha thread ya malalamiko na maswali??
mitandao ya bongo upigaji tu :mad::mad::mad::confused::confused::confused:
 
Ndugu mteja,

Una tatizo lolote unapotumia mtandao wetu? Una ushauri wowote ili tuiboreshe huduma yetu?

Tafadhali itumie mada (thread) hii ili tukusaidie kwa urahisi.

Unapokuwa na tatizo, ili tukusaidie kirahisi zingatia haya:

- Ni tatizo gani? (M-PESA, SMS, Calls, Internet, usajili, kukatika kwa mawasiliano n.k)
- Maeneo gani? (Tukifahamu location, inakuwa rahisi kukuelekeza wapi uende ili upate physical assitance toka kwa vendor wetu aliye karibu nawe)
- Tatizo limeanza lini na limejirudia au kuendelea kuwa kero kwako kwa muda gani?
- Kama ni ushauri, zingatia ya juu lakini tutafurahi tukijua kwanini unapendekeza unachopendekeza
- Kama ni pongezi, zingatia ya juu na tungependa pia upendekeze lipi tufanye kuzidi kuiboresha huduma kwako.

Karibu

Vodacom Tanzania
1550504745758.png

MNAZINGUA
 
Leo vodacom mnashida gani ukipiga simu zinakata tu ukiweka salio haliingi ukiangalia salio hamna tatizo ni nini tupeni hata taarifa basi siyo kuja kuomba samahani baadaye

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Voda kunatatizo gani arusha?.Hatuwezi kuongeza salio, kujiunga na vifurushi wala kuangalia Salio.
 
Back
Top Bottom