Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Voda ni wezi sana nyie... Yaani unit zipo 125 lakini mnaniambia kuwa zipo 50..

ACHENI WIZI
IMG_20181007_082507.jpeg
IMG_20181007_082543.jpeg
 
Vodacom. your services around Kibaha are very erratic. have you sunk that low. Please confirm you have received this and you are working on it.
 
Ndugu mteja,

Una tatizo lolote unapotumia mtandao wetu? Una ushauri wowote ili tuiboreshe huduma yetu?

Tafadhali itumie mada (thread) hii ili tukusaidie kwa urahisi.

Unapokuwa na tatizo, ili tukusaidie kirahisi zingatia haya:

- Ni tatizo gani? (M-PESA, SMS, Calls, Internet, usajili, kukatika kwa mawasiliano n.k)
- Maeneo gani? (Tukifahamu location, inakuwa rahisi kukuelekeza wapi uende ili upate physical assitance toka kwa vendor wetu aliye karibu nawe)
- Tatizo limeanza lini na limejirudia au kuendelea kuwa kero kwako kwa muda gani?
- Kama ni ushauri, zingatia ya juu lakini tutafurahi tukijua kwanini unapendekeza unachopendekeza
- Kama ni pongezi, zingatia ya juu na tungependa pia upendekeze lipi tufanye kuzidi kuiboresha huduma kwako.

Karibu

Vodacom Tanzania
Nyie voda mitambo yenu mnayo funga maeneo ya mpakani ni mibovu au??? Maana unakuta mitambo yenu ipo mipakani na ukiwa na cmu hapo inasoma mitandao ya nchi nyingine
 
Huduma zenu za m pesa zina harufu ya wizi unatuma pesa baada ya hapo sms inayorudi ya muamala haionyeshi gharama ulizokatwa kwa huduma hiyo ukiangalia salio unakuta umekatwa pesa nyingi huo ni wizi hebu rekebisheni hilo tigo kwenye hili wao wako vizuri sana
 
Kwa ujumla hao jamaa lazima huwa wanashirikiana TCRA haiwezekani chombo kinachosimamia walaji kikawa kimya. Kwa maoni yangu tuiunge mkono TTCL maana ni shirika la serikali hata kama tukadhulumiwa ni kama pesa ilitoka mfuko wa kulia kwenda kushoto.
 
Mmebadilisha menu,toka juzi najaribu kuwapigia ili niongee na huduma kwa wateja,lakini inashindika kuunganishwa, tatizo ninini au mmeamua msiwe mnaongea na wateja?

Matatizo ambayo yanahitaji maongezi ya moja kwa moja kati ya mteja na wahudumu mmeona hayana maana au?
 
NILINUNUA KIFURUSHI CHA CONTINENTAL DECORDER KWA M-PESA TOKA 03 OKTOBA 2018 KWANINI HAMJATUMA HIYO HELA KWA CONTINENTAL?

USHAHIDI WA FEFHA NILOTUMA NI HII SMS YENU:

5J321PDPA0S 03-10-2018 10:21:38 Pay Bill to 333355 - CONTINENTAL DIGITAL Acc. 8123403687351180 333355 - CONTINENTAL DIGITAL Completed TZS Tsh-11,999.00

Acheni ubabaishaji bwana pelekeni hiyo fedha CONTINENTAL au irudisheni kwangu....
.
 
wadau naombeni msaada jinsi ya kununua bando kwenye modem ya vodacom nimejaribu kuweka *149*01# pale vodacom service kwenye kipengere cha activate bundle lakini natumiwa SMS kuwa alama niliyotumia siyo sahihi
 
Kwa ujumla hao jamaa lazima huwa wanashirikiana TCRA haiwezekani chombo kinachosimamia walaji kikawa kimya. Kwa maoni yangu tuiunge mkono TTCL maana ni shirika la serikali hata kama tukadhulumiwa ni kama pesa ilitoka mfuko wa kulia kwenda kushoto.
ni bora aisee kuliko kuwapa hawa matapeli me wananikera kinoma serikal imetulia tu tcra ndo hawana hta mpango
 
Vodacom wizi wa kutuibia salio wananchi wanyonge kwa ujanja ujanja usio na maana utaisha lini?, au hadi tuwashtaki kwa Rais?. Kila nikiweka vocha na kubakiza salio kwenye line yangu vodacom mnaiba izo pesa. Utakuta umefanikiwa kujiunga games longe afu salio linakatwa, najitoa kwenye hiyo games longe lakini wapi...hamchoki kuniibia. Zile mia tano zangu mnazoniibia kila siku, mkiiba kwa wateja wenu milioni moja inamaana kwa siku mnajiingizia shilingi milioni mia tano kiujanja ujanja na kwa mwezi ni bilioni kumi na tano. Hizi pesa hizi sizinajenga hospitali huko vijijini?. (Huu mfano tu ila ni kweli hua naibiwa mia tano kila nikibakiza salio. Namba yangu ni 0769515507)

Nilifikiri ni mimi tu, nishawachoka hawa jamaa, niliweka salio lazima wakate, ukiwapigia wanakwambia eti ulijiunga na huduma fulani wakati si kweli, wananielekeza kuitoa, nikiwema tena inakuwa hivo hivo.

Dah mpaka nimeamua kuwacha wakate tu
 
Mimi ni mwanahisa wa kampuni yenu na hivi karibuni mmetangaza kuwa mmetoa gawio. Swali langu ni muda gani unapita baada ya kutangaza wanahisa wanapata gawio? Swali la pili je vodacom wana dividend policy?
 
Ndugu mteja,

Una tatizo lolote unapotumia mtandao wetu? Una ushauri wowote ili tuiboreshe huduma yetu?

Tafadhali itumie mada (thread) hii ili tukusaidie kwa urahisi.

Unapokuwa na tatizo, ili tukusaidie kirahisi zingatia haya:

  • Ni tatizo gani? (M-PESA, SMS, Calls, Internet, usajili, kukatika kwa mawasiliano n.k)
  • Maeneo gani? (Tukifahamu location, inakuwa rahisi kukuelekeza wapi uende ili upate physical assitance toka kwa vendor wetu aliye karibu nawe)
  • Tatizo limeanza lini na limejirudia au kuendelea kuwa kero kwako kwa muda gani?
  • Kama ni ushauri, zingatia ya juu lakini tutafurahi tukijua kwanini unapendekeza unachopendekeza
  • Kama ni pongezi, zingatia ya juu na tungependa pia upendekeze lipi tufanye kuzidi kuiboresha huduma kwako.

Karibu

Vodacom Tanzania

Kiukweli mnaboa Sana hasa kuiba muda wa maongezi unaobakia kwenye Simu, yaani ukibakiza hata shilingi 100 baadae ukiangalia huikuti yaani mpaka inalazimu kuwa unajiunga vifurushi vyenu bila kupenda, Kiukweli huo wizi sio mzuri ila za mwizi 40, ipo Siku tutashtaki na hapo mtaona watanzania watakavyo funguka msifikiri hatuoni mnavyotuibia.

Kingine Sms zenu za matangazo imekuwa nyingi mpaka kero yaani kwa siku mtu unapata sms zaidi ya 50 mi sipendi Mara Tatumzuka, Bico, Sportpesa, Dakapesa, Mojabet, Bado bado zakwenu Kiukweli imekuwa kero Sana, sasa uwe na mitandao miwili hapo ndiyo zinatawala zenyewe tu mxiuuuuuueeei
 
Hata mimi mkuu kama tumefanana maana nlisafir kama miez miwil nikasahau sim moja ya voda hom kurud nikakuta dogo kaitia jino haisomi nikaenda voda na lain mkononi wakanambia namba tano nikataja wananiambia hazikubal mwishoe et nisajil nyingine na akat ile nlikuwa naitegemea kupigiwa tena wengi namba zao nlikuwa sina wao ndio walisev zangu namba 0744470135 .ilivyoshindikana nikamaind had leo situmiag voda
Mimi mmeniudhi kitu kimoja nimepoteza laini yangu kuirudisha naambiwa namba tano nilizokuwa nazipigia Mara kwa Mara sasa Mimi nazipata wapi wakati nimepoteza simu kitambulisho ninacho lakini mmeshindwa kunirudishia nimeamua kuachana na voda kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu mteja,

Una tatizo lolote unapotumia mtandao wetu? Una ushauri wowote ili tuiboreshe huduma yetu?

Tafadhali itumie mada (thread) hii ili tukusaidie kwa urahisi.

Unapokuwa na tatizo, ili tukusaidie kirahisi zingatia haya:

- Ni tatizo gani? (M-PESA, SMS, Calls, Internet, usajili, kukatika kwa mawasiliano n.k)
- Maeneo gani? (Tukifahamu location, inakuwa rahisi kukuelekeza wapi uende ili upate physical assitance toka kwa vendor wetu aliye karibu nawe)
- Tatizo limeanza lini na limejirudia au kuendelea kuwa kero kwako kwa muda gani?
- Kama ni ushauri, zingatia ya juu lakini tutafurahi tukijua kwanini unapendekeza unachopendekeza
- Kama ni pongezi, zingatia ya juu na tungependa pia upendekeze lipi tufanye kuzidi kuiboresha huduma kwako.

Karibu

Vodacom Tanzania
Samahani. Nataka kujua taarifa zangu za hisa. Sikuhudhuria mkutano wa wanakosa.
 
Back
Top Bottom