SAYVILLE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 5,104
- 7,857
Kutokana na uhuni ambao VODACOM wamekuwa wananifanyia, mfano bando zangu zinaisha haraka sana katika mazingira ya wazi ya wizi na udanganyifu, nimepunguza sana kutumia vifurushi vyenu. Sasa bado nahifadhi hela yangu kwenye M-PESA na nikiwa na mahitaji nayo ya kununua bando najitumia kwenye namba nyingine.
Hivi karibuni nimegundua kumbe unaweza kununua airtime moja kwa moja kutoka M-PESA kwenda mtandao mwingine bila kuingia gharama za kutuma hela kwanza, nikasema, this is even better! Sidhani kama utaratibu huo mnaupenda.
Sasa jana nilinunua airtime kwenye namba yangu nyingine kutoka M-PESA, nikakaa kidogo kimya, sioni message imeingia wala nini. Nikakumbuka last time ilitokea hivi hivi na nilipoamua kucheki balance ya M-PESA, haikupita dakika 3 message ikaingia kuwa hela niliyotumia imekwenda.
Akili ikanijia kuwa kumbe mnanitegea mpaka nicheki balance yangu ndiyo mnakamilisha muamala (ukicheki balance utaratibu unajulikana kuwa mnakata hela kwenye M-PESA). Nikasema sitafanya hivyo, badala yake nikajitumia kiasi kidogo cha pesa kutoka M-PESA kwenda M-PAWA, nikajua ukifanya hivyo message itakuja ikionyesha balance ya M-PAWA na M-PESA. Na kweli, message imekuja hapo hapo na inaonyesha hela niliyotuma imekwenda na hata ile niliyotuma kununua airtime mtandao mwingine pia inaonyesha ilishatoka ila kule kwingine haijafika.
Customer service nimewapigia jana wananiambia nisubiri masaa 24 kama itashindikana nitarudishiwa. Nimesubiri sasa ni masaa zaidi ya 28 yamepita, hela yangu haijarudi M-PESA na huko nilikotuma haijafika.
Najua mnanitega mpaka nicheki balance yangu ya M-PESA ili mnikate hela ndiyo mkamilishe muamala na nimeamua sifanyi hivyo.
Msiponirudishia hela yangu nitachukua hatua zaidi.
Hivi karibuni nimegundua kumbe unaweza kununua airtime moja kwa moja kutoka M-PESA kwenda mtandao mwingine bila kuingia gharama za kutuma hela kwanza, nikasema, this is even better! Sidhani kama utaratibu huo mnaupenda.
Sasa jana nilinunua airtime kwenye namba yangu nyingine kutoka M-PESA, nikakaa kidogo kimya, sioni message imeingia wala nini. Nikakumbuka last time ilitokea hivi hivi na nilipoamua kucheki balance ya M-PESA, haikupita dakika 3 message ikaingia kuwa hela niliyotumia imekwenda.
Akili ikanijia kuwa kumbe mnanitegea mpaka nicheki balance yangu ndiyo mnakamilisha muamala (ukicheki balance utaratibu unajulikana kuwa mnakata hela kwenye M-PESA). Nikasema sitafanya hivyo, badala yake nikajitumia kiasi kidogo cha pesa kutoka M-PESA kwenda M-PAWA, nikajua ukifanya hivyo message itakuja ikionyesha balance ya M-PAWA na M-PESA. Na kweli, message imekuja hapo hapo na inaonyesha hela niliyotuma imekwenda na hata ile niliyotuma kununua airtime mtandao mwingine pia inaonyesha ilishatoka ila kule kwingine haijafika.
Customer service nimewapigia jana wananiambia nisubiri masaa 24 kama itashindikana nitarudishiwa. Nimesubiri sasa ni masaa zaidi ya 28 yamepita, hela yangu haijarudi M-PESA na huko nilikotuma haijafika.
Najua mnanitega mpaka nicheki balance yangu ya M-PESA ili mnikate hela ndiyo mkamilishe muamala na nimeamua sifanyi hivyo.
Msiponirudishia hela yangu nitachukua hatua zaidi.