Moderator tafadhali usibadilishe heading nimemaanisha iwe hivyo kwani Vodacom ni wezi kweli kweli sio masihara. Nimekuwa najiunga na cheka time yao ambayo wanadai ni 24 hours japo si kweli. Lakini cha ajabu hata hayo masaa ambayo bado ni less than 24 hawatoi hiyo huduma inavyotakiwa matokeo yake wanaiba kwa ku-double charge. Wanadai muda wa cheka time ni ni saa 12-11 jioni na saa 3-6 usiku lakini mara nyingi hiyo saa saa 3 mpaka 6 usiku hata kama una dakika 60 za cheka time hawatumiii hiyo balance badala yake wanakucharge kawaida. Huu kama sio wizi ni nini? Hiyo double charge jamani inakuwaje? Hakuna apology wala refunds kama tulivyozoea mitandao mingine wao wanauchuna, wakikucharge wrongly ndio imetoka hiyo. Its true kwamba computers huwa zinafail lakini basi muwe mnarefund kama wanavyofanya wengine? Huu kama si ufisadi nao tuuiteje? Otherwise badilisheni jina la hii huduma yenu badala ya CHEKA TIME iwe NUNA TIME maana huwezi kucheka kwa kuwa double charged sana sana utaishia kununa tu.