Vodacom msijisahau, kuweni washindani

SuperImpressor

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
1,504
646
Kama mnavyojua watoa huduma mbalimbali wanavyoendelea kuboresha biashara zao ili kuwavutia wateja, ambapo sasa naongelea virtual card zinazotusaidia kufanya manunuzi mtandaoni.

Airtel Money Mastercard yaweza kuwa salama zaidi kuliko M-Pesa Mastercard, hii ni kutokana na upatikanaji wa taarifa za Airtel Money Mastercard kuwa mgumu mpaka uingie kwa passcode kuliko M-Pesa Master card ambayo taarifa zake ziko nje nje na mtu akichukua simu yako akaenda kwenye USSD ya *150*00# hadi ilipo M-Pesa Mastercard, ataingia pyuuu! hadi ndani.

Vodacom angalieni hicho kitu. Hilo linawatia doa.

Nakumbuka hata zamani walikuwa wanatoa huduma ya email account kwa wateja wao (076.....58@vodamail.co.tz au pia uliweza kuset alias something@vodamail.co.tz) na mimi ni mmoja wa waliokuwa wanaitumia lakini baadaye walisitisha huduma hiyo bila notice yoyote. Hilo nalo ni doa ingawaje bado tumeendelea kuwang'angania. Kilichoniuma zaidi kuna wapsite nilitengeneza enzi hizo na nikaregister kwa kutumia hiyo ......@vodamail.co.tz, na sasa sina access kwenye hiyo wap na hakuna update yoyote nawezafanya huko, hivyo imekaa kizamanizamani tu.
 
Itabdi waifanyie kazi aisee maana mtu mwingine anakuwa na uwezo wa kufanya hatar kweny cm yangu
 
Ulishaletwa uzi kama huu humu, issue ni kwamba hata kadi za benki zipo hivyo hivyo uchi, ni sera yao hawa mastercard/visa na wala sio tatizo la Voda.
Hapo bado sijaafiki, kwani hiyo ya Airtel Money Mastercard mbona yenyewe haifikiki kizembe hivyo? Kwa nini lisiwepo kufuli kwenye menu ya M-Pesa kama lilivyo kwenye Airtel? Kwani wameshindwa nini? Je, mtu akiingia akakufutia hiyo virtual card yako na tayari umeshafanya manunuzi na kwa bahati mbaya seller asifikishe mzigo wako si hapo itakuwa shida na wakati huo ukahitaji refund je, si itakuwa shida hapo?

Sikupingi mkuu ila naomba ufanye comparison kati ya menu ya M-Pesa na Airtel Money.
Nimeipenda ya Airtel kwa upande wa Card.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo bado sijaafiki, kwani hiyo ya Airtel Money Mastercard mbona yenyewe haifikiki kizembe hivyo? Kwa nini lisiwepo kufuli kwenye menu ya M-Pesa kama lilivyo kwenye Airtel? Kwani wameshindwa nini? Je, mtu akiingia akakufutia hiyo virtual card yako na tayari umeshafanya manunuzi na kwa bahati mbaya seller asifikishe mzigo wako si hapo itakuwa shida na wakati huo ukahitaji refund je, si itakuwa shida hapo?

Sikupingi mkuu ila naomba ufanye comparison kati ya menu ya M-Pesa na Airtel Money.
Nimeipenda ya Airtel kwa upande wa Card.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sijatumia bado hio ya Airtel money hivyo ni ngumu kwangu kufanya comparison, nazungumzia tu hilo suala la details kuwa uchi.
 
Kiongozi kuna mahali nakwama, nimetengeneza kadi ya airtel mastercard, naletewa namba za kadi zikiwa hazijatimia yaani kuna namba mwanzo na mwisho ila katikati ni xxxxx Tu. Nafanyaje kupata full details za kadi yangu ? Kwa chini waniambia nibonyeze sijui ki link gani kupata taarifa za kadi yangu.
Ninaporudi kwenye menyu yao ili niingie taarifa za kadi bado mambo ni yale yale nafanyaje.
Nimepiga customer care ushirikiano ni xito kabisa hawapokei.
Mwisho kabisa nani mwenye makato makubwa kati ya mpesa mastercard na airtel master card ufanyapo manunuzi online
 
Hizo namba ulizoletewa zikiwa hazijatimia utaziona zikiwa full utakapo click kwenye hiyo link waliyokutumia, na hiyo link itakapokuwa imefunguka utaiona kadi yako ikiwa na taarifa zote hadi jina lako. Na wewe pia waweza kuidownload kama tunavyodownload online copy ya kitambulisho cha kitaifa. Na hiyo link ukichelewa kuifungua inaExpire hadi uende tena kwenye menu ya Airtel Money Mastercard kuomba taarifa za Card na hapo utatumiwa tena link yenye code tofauti na ulizotumiwa mwanzoni.
Na hiyo link ili utumiwe mpaka uingize namba za siri za Airtel Money na hapo ndipo nimepapenda.

Kuhusu nani ana makato makubwa kati ya M-Pesa Mastercard na Airtel Money Mastercard, ndo sasa najipanga kuanza kuitumia Card ya Airtel tuone utofauti uko wapi. Ila kuhusu usiri nimeipenda Airtel. Na kitu kingine nitakachotafiti ni kuhusu card iliyokwisha muda wake kama ukiiendeleza itarudi tena kama ilivyokuwa au ndo kwisha kazi yake. Maana kule voda nilijaribu kuiendeleza lakini niliona matokeo hasi baada ya kuletewa namba za card tofauti na za card niliyoiendeleza.

Hapa chini ni screenshot ya hiyo card ya Airtel.
IMG_20191022_125158.jpeg
 
Hizo namba ulizoletewa zikiwa hazijatimia utaziona zikiwa full utakapo click kwenye hiyo link waliyokutumia, na hiyo link itakapokuwa imefunguka utaiona kadi yako ikiwa na taarifa zote hadi jina lako. Na wewe pia waweza kuidownload kama tunavyodownload online copy ya kitambulisho cha kitaifa. Na hiyo link ukichelewa kuifungua inaExpire hadi uende tena kwenye menu ya Airtel Money Mastercard kuomba taarifa za Card na hapo utatumiwa tena link yenye code tofauti na ulizotumiwa mwanzoni.
Na hiyo link ili utumiwe mpaka uingize namba za siri za Airtel Money na hapo ndipo nimepapenda.

Kuhusu nani ana makato makubwa kati ya M-Pesa Mastercard na Airtel Money Mastercard, ndo sasa najipanga kuanza kuitumia Card ya Airtel tuone utofauti uko wapi. Ila kuhusu usiri nimeipenda Airtel. Na kitu kingine nitakachotafiti ni kuhusu card iliyokwisha muda wake kama ukiiendeleza itarudi tena kama ilivyokuwa au ndo kwisha kazi yake. Maana kule voda nilijaribu kuiendeleza lakini niliona matokeo hasi baada ya kuletewa namba za card tofauti na za card niliyoiendeleza.

Hapa chini ni screenshot ya hiyo card ya Airtel.View attachment 1240874
Nimeipata kadi jinsi ya kuweka mtonyo kwa kadi ndio mtihani nielekez natka niitumie nw tu nijue wema wake
 
Nimeipata kadi jinsi ya kuweka mtonyo kwa kadi ndio mtihani nielekez natka niitumie nw tu nijue wema wake
kiasi ulichonacho kwenye akaunti ya Airtel Money ndicho sawa na kiasi cha Master card. Ukitaka kufanya malipo yatakatwa kwenye akaunti ya Airtel Money. Kazi kwenu.
 
Iko hivyo mkuu kwa hiyo hapo ni kuwa makini kwa wale wanaofanya majaribio, ukijichanganya kidogo hela zinafyekwa. Ila nitaendelea kuifuatilia nione.
Mkuu mimi bancAbc waliadd hidden fees bila kutuambia, kila website inapo attempt kufanya transaction wanakata 2000, na kitu hichi ni kawaida online hasa website za domain, kama kadi haina hela kila baada ya masaa kadhaa wanajaribu tena.

Siku nakuja kuweka hela kama 80,000 wakaramba yote hapo hapo balance ikabaki zero, nilipowafata bank ndio wakanionesha deni langu negative za kutosha.

Na ninavyofahamu hizi master card zipo powered na hao BancAbc hivyo kama hela wanatoa moja kwa moja kwenye Airtel money ipo siku watu watakuja kulia, account inakaa bila hela muda mrefu siku unatumiwa hela wanakata zote.
 
Mkuu mimi bancAbc waliadd hidden fees bila kutuambia, kila website inapo attempt kufanya transaction wanakata 2000, na kitu hichi ni kawaida online hasa website za domain, kama kadi haina hela kila baada ya masaa kadhaa wanajaribu tena.

Siku nakuja kuweka hela kama 80,000 wakaramba yote hapo hapo balance ikabaki zero, nilipowafata bank ndio wakanionesha deni langu negative za kutosha.

Na ninavyofahamu hizi master card zipo powered na hao BancAbc hivyo kama hela wanatoa moja kwa moja kwenye Airtel money ipo siku watu watakuja kulia, account inakaa bila hela muda mrefu siku unatumiwa hela wanakata zote.
Ngoja tuendelee nao tuone labda na wao watawaka tamaa watufanyie hivyo. Bado wanatuvuta vuta.
 
Kiongozi kuna mahali nakwama, nimetengeneza kadi ya airtel mastercard, naletewa namba za kadi zikiwa hazijatimia yaani kuna namba mwanzo na mwisho ila katikati ni xxxxx Tu. Nafanyaje kupata full details za kadi yangu ? Kwa chini waniambia nibonyeze sijui ki link gani kupata taarifa za kadi yangu.
Ninaporudi kwenye menyu yao ili niingie taarifa za kadi bado mambo ni yale yale nafanyaje.
Nimepiga customer care ushirikiano ni xito kabisa hawapokei.
Mwisho kabisa nani mwenye makato makubwa kati ya mpesa mastercard na airtel master card ufanyapo manunuzi online

ingia google search engine...ukiwa unaingia kwenye simu kuna meseji huwa inakuja pale na kitu kama link....sasa paste ile link hapo na usearch...utaona moja kwa moja details za kadi yako zinatokea...save na hakikisha humuoneshi mtu kwa usalama zaidi.
 

Similar Discussions

3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom