The Businessman
JF-Expert Member
- Jan 9, 2014
- 7,404
- 9,234
Habari wakuu,
Wengi wetu bado tunatumia mtandao wa Vodacom kwa kazi maalumu japo hatuweki vocha, Wazazi wetu wengi pia wanatumia huu mtandao hasa wazee.
Sasa jana jioni nimenunua vocha ya vodacom ya shilingi 5000, tukaweka kwenye kwenye simu ya bibi baada ya kama dakika 20 tukasema ngoja tumrushie na mamkubwa shilingi 2000 tunaambiwa salio lako halitoshi yaani tunakuta imo shilingi 78.3 na wakati hatujaitumia na bibi hajawahi kukopa na hajui hata kukopa ni nini, yeye ni kupiga na kupokea. Tukawapigia voda wakaishia kutuwekea matangazo na kukata simu.
Sasa vodacom pesa yetu imeenda wapi?
Wengi wetu bado tunatumia mtandao wa Vodacom kwa kazi maalumu japo hatuweki vocha, Wazazi wetu wengi pia wanatumia huu mtandao hasa wazee.
Sasa jana jioni nimenunua vocha ya vodacom ya shilingi 5000, tukaweka kwenye kwenye simu ya bibi baada ya kama dakika 20 tukasema ngoja tumrushie na mamkubwa shilingi 2000 tunaambiwa salio lako halitoshi yaani tunakuta imo shilingi 78.3 na wakati hatujaitumia na bibi hajawahi kukopa na hajui hata kukopa ni nini, yeye ni kupiga na kupokea. Tukawapigia voda wakaishia kutuwekea matangazo na kukata simu.
Sasa vodacom pesa yetu imeenda wapi?