Vodacom kifurushi cha siku Sh. 500,000/= wizi mtupu

salimkabora

JF-Expert Member
Nov 10, 2012
2,441
651
Jana nimenunua kifurushi cha vodacom internet kinachosomeka 9,000/= kwa mwezi; kabla sijaanza kusoma emails zangu umeme ukakatika na haukurudi hadi saa 12 jioni. Nilipowasha computer nilipokea ujumbe wa kifurushi kimeisha ili hali ni muda mfupi tu tangu nifungue internet hata nusu saa bado; sasa swali, hivi huu wizi wa aina hii ni nani anaudhibiti katika taifa hili? je hii fedha ya wizi wa jinsi hii toka kwa mteja maskini haiwezi kuibiwa fedha kubwa faidi kwenye kodi ya nchi? kwanini hivi vifurushi makampuni wanayojitangazia kitapeli havisajiliwi ili viweze kufatiliwa na mamlaka husika? elfu tisa kuunguzwa kwa nusu saa ni karibia laki tano kwa masaa 24; hivi kweli upo uhalali gani hapo? unaibiwa huku huwezi kujilinda?
 
Nenda police katoe malalamiko yako pia mamlaka husika itafikishiwa na kulishughulikia pengne na kweli lakn cc hatujui kwan ulipotaka kujiunga hukutuambia ila tuu umeona tofauti ndo ukatuambia so hatuwez sema chochote na vodacom nawapenda sana tu hawana shida hata
 
Account yako ina salio LA shilingi 1000 unajaribu kujiunga kifurushi cha data cha mb 500 kwa siku ambacho kimsingi kinauzwa sh 1000 unaambiwa hauna salio LA kutosha kila ukicheck balance haijatoka hata senti moja matokeo yake unalazimika kununua kifurushi cha mia tano ambacho kwa technologia hii ya 4G LTe mb 150 zinaisha fasta,sasa je kwanini ukiwa na 1000 inazingua kununua kifurushi mpaka simu iwe na 1000 na shilingi kadhaa.
 
Hakikisha unatumia browser ambayo inazuia ads(yenye adblocker extension). Tumia Yandex inapokea extensions nyingi za adblocker .Hii Inapunguza upotevu wa MBs
 
Account yako ina salio LA shilingi 1000 unajaribu kujiunga kifurushi cha data cha mb 500 kwa siku ambacho kimsingi kinauzwa sh 1000 unaambiwa hauna salio LA kutosha kila ukicheck balance haijatoka hata senti moja matokeo yake unalazimika kununua kifurushi cha mia tano ambacho kwa technologia hii ya 4G LTe mb 150 zinaisha fasta,sasa je kwanini ukiwa na 1000 inazingua kununua kifurushi mpaka simu iwe na 1000 na shilingi kadhaa.
Namba yangu ni 0754 84 33 88 nina balance ya airtime ths 1,520,882/= na ujumbe wa jana kwamba nimepatiwa kifurushi cha elfu tisa bado ninao; msiwe na mawazo ya kimasikini kila siku, angalia hoja na misingi yake sio kukurupuka
 
Nenda police katoe malalamiko yako pia mamlaka husika itafikishiwa na kulishughulikia pengne na kweli lakn cc hatujui kwan ulipotaka kujiunga hukutuambia ila tuu umeona tofauti ndo ukatuambia so hatuwez sema chochote na vodacom nawapenda sana tu hawana shida hata

Kama hawanashida kwako mkuu, haina maana hawana shida kwa kila mtu, Vodacom wanashida sana tu kwa kulamba vifurushi. Mimi walishalamba elfu 20 zangu kwa masaa matatu tu. nilijiunga bundle la wiki kwa elfu 5, wakalamba ndani ya saa moja, nikajiunga tena bundle la mwezi kwa elfu 15, wakalamba ndani ya masaa 2, na hapo sijadownload chochote zaidi ya kusoma message tu, niliwapigia wakanizungusha tu hawakunisaidia chochote.
 
Kama hawanashida kwako mkuu, haina maana hawana shida kwa kila mtu, Vodacom wanashida sana tu kwa kulamba vifurushi. Mimi walishalamba elfu 20 zangu kwa masaa matatu tu. nilijiunga bundle la wiki kwa elfu 5, wakalamba ndani ya saa moja, nikajiunga tena bundle la mwezi kwa elfu 15, wakalamba ndani ya masaa 2, na hapo sijadownload chochote zaidi ya kusoma message tu, niliwapigia wakanizungusha tu hawakunisaidia chochote.
Yani huo ndio mwendo wao ni mambo ya kiwiziwizi tuuuu; sasa kwa kuwa watanzania wengi ni mazezeta kazi ni kushabikia na kutetea wakati kuna wizi wa hali ya juu sana unafanyika dhidi ya wateja
 
Voda wezi sana, jana mimi nimejiunga kifurushi cha sh 5.000 nikaongea cm kama 3 za dakika tatu hadi nne, leo asubuhi nimeongea dakika 18 simu imekata kifurushi kimeisha
 
Jana nimenunua kifurushi cha vodacom internet kinachosomeka 9,000/= kwa mwezi; kabla sijaanza kusoma emails zangu umeme ukakatika na haukurudi hadi saa 12 jioni. Nilipowasha computer nilipokea ujumbe wa kifurushi kimeisha ili hali ni muda mfupi tu tangu nifungue internet hata nusu saa bado; sasa swali, hivi huu wizi wa aina hii ni nani anaudhibiti katika taifa hili? je hii fedha ya wizi wa jinsi hii toka kwa mteja maskini haiwezi kuibiwa fedha kubwa faidi kwenye kodi ya nchi? kwanini hivi vifurushi makampuni wanayojitangazia kitapeli havisajiliwi ili viweze kufatiliwa na mamlaka husika? elfu tisa kuunguzwa kwa nusu saa ni karibia laki tano kwa masaa 24; hivi kweli upo uhalali gani hapo? unaibiwa huku huwezi kujilinda?
hatari sana mkuu,na inauma sana,wanajua ila ndio vile hakuna wa kututetea,nchi ngumu hii..
 
DILI LA TCRA imenitokea kupitia Tigo+ voda nilipiga Cm Tcra Wakaniunga Tigo elf2 yangu hadi waleo! majibu c TCRA au Tigo kote alikuwa hovyo! nilienda kulalamika Bukoba ofisi hakuna msaada. mdhibiti ni TCRA wana 10% hata J. Makamba anajua utasemea wapi?
 
hatari sana mkuu,na inauma sana,wanajua ila ndio vile hakuna wa kututetea,nchi ngumu hii..
Mkuu labda wazee wa matamko wataangalia na pande hizi pia; tuombe mungu manake kwa sasa wanabip tu wakiona hakuna ufatiliaji au mamlaka inayoinua mdomo kukemea ndio wateja watatolewa chozi la damu
 
Kumekuwa na malalamiko mengi kuhusu hivi vifurushi, nafikiri ni wakati wa mamlaka hisika TCRA kutoa mwongozo. Sasa hivi ni wizi mtupu
 
Nani unadhani atakuwa msaada kwako! Wenye hisa kubwa huko vodacom unawajua? Usijisumbue kupeleka kesi ya swala kwa simba! Ww sikilizia maumivu yakiisha nunua tena. Pole, haya ndiyo maisha ya Tanzania. Mimi nimesha zoea.
 
me nlijiunga dabo bando ya 1500 had xaiv sjaletewa kifuruxhi na pesa waxhachukua,nkiwapigia wanasema pesa bado ipo hewani,vodacom n wasumbufu xana
 
DILI LA TCRA imenitokea kupitia Tigo+ voda nilipiga Cm Tcra Wakaniunga Tigo elf2 yangu hadi waleo! majibu c TCRA au Tigo kote alikuwa hovyo! nilienda kulalamika Bukoba ofisi hakuna msaada. mdhibiti ni TCRA wana 10% hata J. Makamba anajua utasemea wapi?
Na sasa ndio wameibuka na dili jipya la kuscrap salio ambalo halijamalizwa ndani ya siku 60; yani hapo si kwamba tu utaibiwa vifurushi ulivyonunua bali hata masalio ya wateja yatakuwa yanayeyuka kiaina kwa ridhaa ya wamiliki wa vodacom na hapo ndio sijui salio langu la tshs 1,520,882/= nitalifanyaje kabla halijapigwa kinyama ilihali nimelikusanya kwa muda mrefu ajili ya ku launch website yangu mpya. Yani mimi sijui hata ni uharamia wa aina gani hii unaendelea ndani ya makampuni ya simu na sijui nani kawapa matapeli leseni za biashara hii
 
Nani unadhani atakuwa msaada kwako! Wenye hisa kubwa huko vodacom unawajua? Usijisumbue kupeleka kesi ya swala kwa simba! Ww sikilizia maumivu yakiisha nunua tena. Pole, haya ndiyo maisha ya Tanzania. Mimi nimesha zoea.
Na sasa ndio wameibuka na dili jipya la kuscrap salio ambalo halijamalizwa ndani ya siku 60; yani hapo si kwamba tu utaibiwa vifurushi ulivyonunua bali hata masalio ya wateja yatakuwa yanayeyuka kiaina kwa ridhaa ya wamiliki wa vodacom na hapo ndio sijui salio langu la tshs 1,520,882/= nitalifanyaje kabla halijapigwa kinyama ilihali nimelikusanya kwa muda mrefu ajili ya ku launch website yangu mpya. Yani mimi sijui hata ni uharamia wa aina gani hii unaendelea ndani ya makampuni ya simu na sijui nani kawapa matapeli leseni za biashara hii
 
VODACOM ni wezi hakuna mfano, haijapata kutokea kampuni ya MAJIZI nchi huu wanauweza kuikaribia VODACOM.
 
Mkuu labda wazee wa matamko wataangalia na pande hizi pia; tuombe mungu manake kwa sasa wanabip tu wakiona hakuna ufatiliaji au mamlaka inayoinua mdomo kukemea ndio wateja watatolewa chozi la damu
kibaya zaidi wanaotukamua hivi ukute ni waafrika wenzetu...dunia haina utu tena,hata kama ndio survive of the fittest lkn bado tuendako hatukujui....
 
Back
Top Bottom