Charity24
Senior Member
- Jan 31, 2014
- 124
- 153
Ni wazi kwamba linapokuja suala la kupata huduma nzuri hasa zile za kulipia kila mtu angependa huduma bora. Hoja yangu ipo kwenye watoa huduma za mawasiliano kupitia simu za mkononi. Awali nilikuwa mnazi wa tigo lakini kila siku zinavyosona hawa jamaa wanazidi kuwa wababaishaji hasa kukatwa gharama zisizoeleweka. Nikaamua kuegemea zaidi voda na japokuwa hawakosi mapunguf yao lakini naona wao wako smart zaidi. Ukipiga simu kitengo chao cha huduma kw wateja inapokelewa instantly na unapewa majibu ya ukweli bila kusingizia hata kama kuna tatizo hawafichi. Hii imenikuna sana nikaona siyo vibaya kutoa pongez pale zinapostahili kutolewa. Sijui wadau nyie mnaonaje. Airtel sina uzoefu nao.