wakuu nimepita wilaya nyingi kutafuta maisha nimekutana na kitu adimu sana nchini humu. Nilifika wilaya ya kilindi mkoa wa tanga wilaya hii ni mpya imezaliwa kutoka wilaya ya handeni, nilifika nikakutana na maafisa ardhi ambao niliwashangaa. Kwani nilipewa fomu ya maombi nikalipia benki tsh 5000 halafu wakanipa ramani na bei ya kila kiwanja ipo kwenye kitabu cha bei nkachagua kiwanja wakanipa invoice nikalipa benki kwenye akaunti mbili za serikali nikarudi kwao wakanielekeza kwenda ofisi ya fedha nikakatiwe risiti.nikakatiwa risit nilichoshangaa nikaandaliwa offer yangu ya kiwanja sikuhiyohiyo. Wadau ardhi kuna urasimu lakini kama ofisi zote zingekuwa hivi mambo yangekuwa mstari.wakaniambia wanawakaribisha watanzania wote na wametangaza viwanja hivyo kwenye magazeti.kwa anayetaka fursa hii wasiliana na hao maofisa o787737616 au 0653792114 kazi kwenu wajasiliamali