Viwanda vya Sukari kufungwa, Serikali yajiandaa kuagiza tani 100,000 za Sukari nje

FikraPevu

JF-Expert Member
Jan 2, 2010
303
236
Waziri-copy-750x350.jpg

Serikali ya Tanzania inakusudia kuagiza tani 100,000 za sukari kutoka nje ili kukabiliana na uhaba wa sukari nchini utakaosababishwa na kufungwa kwa muda kwa viwanda vyote vinavyozalisha sukari nchini, hali ambayo tayari imesababisha uhaba mkubwa wa bidhaa hiyo, huku katika baadhi ya maeneo nchi ikianza kuuzwa kwa bei ya kuruka.

Taarifa zilizoifikia
FikraPevu zinasema viwanda vyote vikubwa vya sukari nchini vitasitisha uzalishaji wa bidhaa hiyo muda wowote kuanzia sasa, wakati kwa ujumla, vyote vikiwa na shehena ya akiba ya sukari inayofikia tani 40,000 tu wakati mahitaji halisi ya nchi kwa mwezi ni tani 35,000.


Kwa mujibu wa taarifa hiyo, hali hiyo ya kuadimika kwa sukari katika baadhi ya maeneo nchini hata kabla viwanda hivyo havijasitisha uzalishaji, kumeelezwa kusababishwa na baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu, ambao wanadaiwa kuhodhi bidhaa hizo wakisubiri bei ya bidhaa hiyo iadimike zaidi baada ya viwanda vilivyopo nchini kusitisha uzalishaji hali itakayosababisha kupanda kwa bei zaidi kwa bidhaa hiyo na kuwawezesha kuvuna faida kubwa.

Hadi sasa katika baadhi ya maeneo nchini, sukari imeanza kuuzwa kwa mwendo wa kuruka wa kati ya Sh 2,500 na 3,000 badala ya bei iliyozoeleka ya kati ya Sh 1,800 na 2,000 kwa kilo.

Kwa sasa viwanda vya sukari vilivyopo nchini vilivyokuwa vikizalisha sukari na ambavyo vinakusudia kusitisha uzalishaji kwa muda kwa ajili ya kufanyiwa ukarabati, ni pamoja na kiwanda cha Kilombero na Mtibwa vilivyopo mkoani Morogoro, TPC kilichoko mkoani Kilimanjaro na Kagera sugar kilichoko mkoani Kagera

Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira, amethibitisha kuwepo kwa mpango huo wa Serikali wa kuagiza tani 100,000 za sukari nje ili....

Habari zaidi, soma=>
Viwanda vya sukari kufungwa, Serikali yajiandaa kuagiza tani 100,000 za sukari nje.
 
Hivi lile sakata la ufisadi wa sukari lilokuwa linamkabili Mizengo liliishia wapi???
 
Hawa nao wanatuzingua juzi sukari ilipokuwa nyingi nchini walikuwa wanapiga kelele kuwa wanashindwa kuuza sukari mwani muna sukari inaingizwa nchini ki magendo leo serikali imezuia uingizaji wa sukari, wao tena wanasema wanataka kukarabati viwanda!! Hivyo kupelekea tena vibali vitolewe tena!! Na bei ya sukari kupanda.
 
Kwa mwonekano wa wasira, kuwa kiongozi naona kama mnapotezwa maksudi hivi, mkija kushtuka mko katikati gombe.
 
Serikali dhaifu tu hii, unabinafsisha kila kitu mpaka baadae wafanyabiashara wanajipangia wanavyotaka.
Tutaburuzwa haswa coz serikali imeshatiwa mfukoni.
Wabinafsishe mpaka magereza.

Lkn ukija ukifikiria nje ya box unaona huu ni usanii wa serikali, hivi kweli viwanda vyote vinaweza fanya ukarabati at the sametime?

Na isitoshe eti serikali inanunua sukari nje ya nchi wakati viwanda inavyo na vinafanya kazi , hapa hunidanganyi.

Serikali inafanya biashara ya kulazimisha ili wapate hela ya uchaguzi coz wahisani wamebana wafanyabiashara wamebana wapi serikali itoe hela? Hawana pa kwenda so Inabidi serikali ndiyo iwe mfanyabiashara tena wa kulazimisha.
 
Wafunge tu na sukari iagizwe nje mpaka watakapojifunza na watakapoweza kushindana na wazalishaji wa nje. Wanataka kutuuzia sukari bei waitakayo wao, ukiwauliza kisa nini? eti ajira.

Sasa hivi habembelezwi mtu ni soko huria.

Sijawahi ona sloth kama wewe duniani,kama hujui kitu bora ukapike au kaa kimya
 
Wafunge tu na sukari iagizwe nje mpaka watakapojifunza na watakapoweza kushindana na wazalishaji wa nje. Wanataka kutuuzia sukari bei waitakayo wao, ukiwauliza kisa nini? eti ajira.

Sasa hivi habembelezwi mtu ni soko huria.

Endeleeni tu kusifia kila kitu, tukisema mnatuita Chadema. . . .mambo ya muhimu kama haya serikali iwe na shares sio kuuza kila kitu!!!!
 
Wacha wafanye wanavyodikria wenyewe bwana, nilishajua nchi hii haina uongozi nilishajinyamazia shauri yenu nyie mnaofikria kwamba bado kuna Rais nchi hii!! Hata ikiwezekana wafunge milele hivyo viwanda tutahamia kwenye utamu Wa nyuki Pam.baff na karais kenu!!
 
Zitto hana ushauri wowote wa maana aliutoa. Wenye viwanda vya uzalishaji wameshampa chake,sukari ya nje imezuiwa,sasa wenye viwanda wanaleta mizengwe ili bei ipande halafu ndio inakuwa bei halali. Tanzania inaliwa na nani? Kasungura Zitto na jamaa zake
Zitto katoa ushauri mzuri juu ya kuepukana na uhuni huu wa kuagiza sukari
 
Wafunge tu na sukari iagizwe nje mpaka watakapojifunza na watakapoweza kushindana na wazalishaji wa nje. Wanataka kutuuzia sukari bei waitakayo wao, ukiwauliza kisa nini? eti ajira.

Sasa hivi habembelezwi mtu ni soko huria.

Ni kweli lakini bado si soko huria kama serikali ndiyo inayoingiza sukari badala ya wafanyabiashara wa kawaida. Cha ajabu ni kwamba vibali vya kuingiza sukari wamepewa wachache tu! na hii ni rushwa kama ni soko huria bali kibali apewe yeyote na serikali itoke kwenye biashara ya sukari. Uhaba wa sukari ni kwasababu serikali ina wata vibali wachache tu wanaotoa chochote
 
Wafunge tu na sukari iagizwe nje mpaka watakapojifunza na watakapoweza kushindana na wazalishaji wa nje. Wanataka kutuuzia sukari bei waitakayo wao, ukiwauliza kisa nini? eti ajira.

Sasa hivi habembelezwi mtu ni soko huria.

serikali au wakinan watajifunza??
 
Kweli nimeshaona kiza kinene mbele. Mpaka kuelekea Oktoba 2015, kila rangi tutaiona. Tangu enzi za chama kimoja, ccm walijua mahali pekee pa kuchota fedha haraka kufanya uchaguzi bila kutegemea wahisani ilikuwa Sukari.
Juzi kati, tukaambiwa viwanda vitafungwa kama sukari ikizidi kuletwa kutoka nje ya nchi. Ameingia mkuu wa mipango mzee Wasira. Cha kwanza tu kama salamu wizarani, akafuta vibali vyooote ati Vibali Fake. Akaahidi kutatua tatizo la kulundikana kwa sukari kwenye godawni zetu.
Leo; mmekuja na neno kuwa sasa viwanda vyote vinafungwa hivyo sukari iagizwe tena kutoka nje. Nasema, kuna kumchezo hapo. Na hako kamchezo si kazuri hata kidogo.
Ile sukari iliyokuwa ina lalamikiwa na viwanda vyetu kuwa inaua ajira imepelekwa wapi au ilikuwa inapelekwa Pemba ikamezwa na mkondo wa Nungwi? Nawaza tuu jamani.
Iweje, serekali yetu hii sikivu yenye kufanya na kuwaza mengi sana mpaka BRN isiwaze kuhusu wakati viwanda hivyo vinafungwa kupisha matengenezo ya kila mwaka, kwa nini wasiweke uzalishaji wa kutosha kufidia hiyo kipindi?
Vibali hivyo, watapewa nani?? Watz au wageni toka China na kwingineko? Nasema, ni mazingira ya 10% hayo. Hosea yanakuhusu hapo. Usingojee kikao cha bajeti PAC ikuruhusu. Pinda yanakuhusu, usidhani utatoka kiurahisi ka ile ye Escrow.
Jamani, kuleni 10% lakini msile kwa kutuumiza, tumebamizwa mno jamani tuhurumieni kabisaaaaaa
 
Endeleeni tu kusifia kila kitu, tukisema mnatuita Chadema. . . .mambo ya muhimu kama haya serikali iwe na shares sio kuuza kila kitu!!!!

Nendeni nyinyi mkachukuwe shares muendeshe mjuavyo, mnangoja nini?

Serikali ilijitoa zamani sana kuwa ni wafanya biashara, mambo yalikuwa mabaya zaidi wakati serikali ilipokuwa inajishughulisha na hizi biashara. Hukumbuki? hata sukari ilikuwa kilo moja kwa wiki kwa kaya moja, au ulikuwa bado hujazaliwa? unataka turudi tena huko? Maawe!
 
serikali au wakinan watajifunza??

Watajifunza wenye viwanda vya sukari namna ya kuzalisha sukari inayoweza kuhimili ushindani na wazalishaji wa nje. Si kutuuzia mibei ya kiajabu ajabu. Juzi juzi walia Sukari ya nje inauwa viwanda, leo imesitishwa wao hawana ya kuuza, sasa Serikali itowe tena vibali vya kuagiza sukari mambo yaishe.
 
Ni kweli lakini bado si soko huria kama serikali ndiyo inayoingiza sukari badala ya wafanyabiashara wa kawaida. Cha ajabu ni kwamba vibali vya kuingiza sukari wamepewa wachache tu! na hii ni rushwa kama ni soko huria bali kibali apewe yeyote na serikali itoke kwenye biashara ya sukari. Uhaba wa sukari ni kwasababu serikali ina wata vibali wachache tu wanaotoa chochote

Serikali amma itatoa vibali amma itaagiza kwa emergency na uharaka wa kutatua tatizo liliopo.
 
Wafunge tu na sukari iagizwe nje mpaka watakapojifunza na watakapoweza kushindana na wazalishaji wa nje. Wanataka kutuuzia sukari bei waitakayo wao, ukiwauliza kisa nini? eti ajira.

Sasa hivi habembelezwi mtu ni soko huria.


Usikurupuke hawafungi kwaajili ya mgomo au mashindano wanafunga kwaajili ya ukarabati mkubwa.....
 
Back
Top Bottom