Vitz vs starlet

riba

Member
Dec 30, 2016
23
13
Wakuu naomba kujua kati ya izo gari mbili ipi ina ubora zaidi? Kwa upande wa kula mafuta na usafiri wa umbali mrefu. Vilevile ni gari ipi inayo weza kudumu kwa mda mrefu.


Ni hayo tyu Wakuu, wenye kujua wanijuvyeee
 
Ratio ya mafuta ni liter 1/100km sasa kinacho ongezeka ni nguvu yani Horsepower Vits inaanzia cc 1000 mpaka 1300 kwa vits toleo la zamani wakati toleo jipya ni 1500 Stalets zipo za kama aina 4 lakini cc inaanzia 1300 mpaka 1800 kwa stalet granza hii ni kama sport car stalet hawana new model kwani wameanza kuzitengeneza mwaka 1973 to 1999
 
Ratio ya mafuta ni liter 1/100km sasa kinacho ongezeka ni nguvu yani Horsepower Vits inaanzia cc 1000 mpaka 1300 kwa vits toleo la zamani wakati toleo jipya ni 1500 Stalets zipo za kama aina 4 lakini cc inaanzia 1300 mpaka 1800 kwa stalet granza hii ni kama sport car stalet hawana new model kwani wameanza kuzitengeneza mwaka 1973 to 1999
Mkuu asante sana ...ila hujazungumzia suala la kudumu kwa haya magari na upatikanaji wa spear zake uko vipi?

Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app
 
Mkuuu asante sana ...ila hujazungumzia .....suala la kudumu KWa haya magari na upatikanaji wa spear zakeee uko vipi

Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app
Nataka kukwambia kitu ambacho Watanganyika wengi tunachanganya au hatuna taarifa sahihi juu ya vitu nataka kukwambia mpaka gari linaingia sokoni linapitia katika vigezo mbalimbali na viwango mbalimbali lazima ipate kibali cha International Vehicle Standards (IVS) na kama itatoka na kuthibitika aijakidhi vigezo ni lazima zirudishwe kiwandani na kuondolewa sokoni so kati ya vitu ving ambavyo IVS.

Wanasimamia moja wapo ni ubora wa gari husika sasa bhasi gari zote ni bora tatizo kwa kwetu ni Utunzaji na barabara za Africa ni mbovu ujiulizi kwa nini Tunanunua magari ya miaka ya 1980 au 90 lakini yanaonekana bado mapya yakija huku ndo yanachakaa?

Mimi nakushauli nunua Stalet pia gari baada ya km fulani peleka gereji kuhusu Spare dunia ya sasa usiogope kununua gari kwa kuogopa hakuna spare siku hz watu wanaagiza tu ndani ya cku 4 imefika na bei ni nafuu tu
 
Nataka kukwambia kitu ambacho Watanganyika wengi tunachanganya au hatuna taarifa sahihi juu ya vitu nataka kukwambia mpaka gari linaingia sokoni linapitia katika vigezo mbalimbali na viwango mbalimbali lazima ipate kibali cha International..
Asante mkuu.
 
Ratio ya mafuta ni liter 1/100km sasa kinacho ongezeka ni nguvu yani Horsepower Vits inaanzia cc 1000 mpaka 1300 kwa vits toleo la zamani wakati toleo jipya ni 1500 Stalets zipo za kama aina 4 lakini cc inaanzia 1300 mpaka 1800 kwa stalet granza hii ni kama sport car stalet hawana new model kwani wameanza kuzitengeneza mwaka 1973 to 1999
Mkuu kwaiyo mafuta yanalika sawa na pikipiki? i.e 1/100km
 
Mkuu kwaiyo mafuta yanalika sawa na pikipiki? i.e 1/100km
Mkuu unapozungumzia pikipiki kuna mapikipiki makubwa na mengine yanampaka rejeta na yanakunywa mafuta kuliko hata GX 110 Ratio ya 1/100 km ni ratio ya kimataifa ya ulaji wa mafuta kwa gari sasa bhasi.

Suala la gari itumie mafuta kiasi gani kwa mzunguko gani wa engine linabaki kwa mtengenezaji wa gari mfano magari mengi ya ulaya hayatumii mafuta mengi pamoja na kuwa na Cc kubwa na watengenezaji wa magari kwa sasa wanatengeneza magari ya kutumia umeme sana mafuta kidogo
 
It looks like this will be your first car. Huwezi kuwauliza watu wenye akili timamu kwamba vitz na starlet lipi ni gari zuri kununua. Wote waliokujibu wamejibu pumba.

Ili upate jibu la uhakika lazima u-specify model ya gari na pengine engine size. Vitz ana models nyingi so is starlet. Kwa wanaojua magari vizuri, hata ukieleza year of manufacture anajua ni model ipi.

Sasa ukiwa specific to that extent, kwa wajuzi wa magari utakuwa umewatengenezea premises nzuri za kukushauri.
Samahani kwa kutumia lugha yenye ukakasi.
 
Sahihisha hii ratio mkuu...
Mkuu ratio ni hyo hyo kwa magari madogo gari ikiwa ainatatizo lolote kwenye mifumo ya engine au mafuta kwa Heavy Duty Trucks ni 13.3/100 km na magari ya kati ni 10.7/100km tatizo 90% ya magari yanayotembea Tanganyika mifumo yao ya engine na mifumo ya uchomaji mafuta ni mibovu pia unatakiwa kujua ukibadilisha mataili au kuweka rims kubwa ili gari ipendeze tayali unakuwa umeshatibua ulaji wa mafuta kwenye gari
 
Ratio ya mafuta ni liter 1/100km sasa kinacho ongezeka ni nguvu yani Horsepower Vits inaanzia cc 1000 mpaka 1300 kwa vits toleo la zamani wakati toleo jipya ni 1500 Stalets zipo za kama aina 4 lakini cc inaanzia 1300 mpaka 1800 kwa stalet granza hii ni kama sport car stalet hawana new model kwani wameanza kuzitengeneza mwaka 1973 to 1999
Mkuu naomba ufafanuzi hiyo ratio ya 1lt/100km au unamaanisha 1lt/10km maana hata pikipiki si hivyo!
 
Mkuu naomba ufafanuzi hiyo ratio ya 1lt/100km au unamaanisha 1lt/10km maana hata pikipiki si hivyo!
Mkuu ratio ni hyo hyo International Vehicle Standards (IVS) ndio wana recommend ratio hyo kwa magari madogo 1/100Km huku Heavy Duty Trucks ni 13.3/100Km na magari ya kati ni 10.7/100Km kama nilivyosema hapo mwanzo ulaji wa mafuta kwa gari unatokana na mapendekezo ya mtengenezaji kutokana na speed au nguvu inayotumika kwenye engine na ndo maana ulaji wa mafuta gari iliyotupu ni tofauti na gari yenye mizigo

Mfano ukiwa unaendesha baiskeli ukiwa peke yako nguvu utakayo tumia ni tofauti na ukiwa umepakiza mizigo au mtu mwingine pia ulaji wa mafuta auna mahusiano na Cc na Cylinders (horsepower) mfano kuna gari linaitwa Mazda rx8 ina Cc 1300 na 4 Cylinder lakini ulaji wake wa mafuta ni kama ina engine ya V8 lakini inakimbia zaidi ya Alteeza ikiwa na speed ya 239 km/h na inauwezo wa zero to 96.56 km/h in 6.3 seconds pamoja kuwa na Cc ndogo na horsepower au Cylinders 4


Magari mengi sana yanatumia mafuta mengi kutokana na watu kutokujua tu mfano magari ya ulaya yanatumia mafuta kidogo sana pamoja na kuwa na Cc kubwa watengenezaji wameweka matumizi ya umeme kuliko mafuta kwenye magari zipo sababu znazofanya magari kunywa mafuta sana ila watu wengi wakiona gari inakwenda bhasi wanaona ni sawa tu lakini zipo sababu nying sana nitakutolea chache

1 bad timing
2 bad sparkplugs
3 low octane fuel
4 malfunctioning coolant temperature sensor
5 blocked catalytic converter(s)
6 malfunctioning MAP/MAF sensors
7 driving with the parking brake engaged
8 having aftermarket wings on the car.
9 tyres not inflated to the recommended pressure

Kitu kingine ambacho nimekiona kwa wabongo wengi ni uendeshaji mbaya wa magari watu wengi si madereva wazuri hata ktk ubadilishaji wa gia tu utajua huyu si dereva hata gari ya automatic nayo inauendeshaji wake si ukiweka D basi
 
Back
Top Bottom