Vituo vya mafuta katikati ya mji na makazi ya watu Dar: Bomu linalosubiri maafa makubwa

Tujiulize maswali haya
Je mipango miji inaruhusu vituo vya mafuta katikati ya miji na makazi ya watu?
Je sera ya mamlaka ya viwango na ubora inaruhusu vituo vya mafuta katikati ya miji na makazi ya watu?
Vipi wizara ya miundombinu?
Vipi wizara ya mazingira?
Jeshi la zimamoto je nalo haliwezi kuhusika hapa?

Kimsingi pamoja na tahadhari zote za usalama zinazochukuliwa lakini bado haishauriwi kuwa na vituo vya mafuta katikati ya miji na makazi ya watu... Na sheria ya vituo vya mafuta inasema kuwe na umbali USIOPUNGUA kilometer 5 kati ya kituo kimoja hadi kingine
Mafuta ni kitu kinachoweza kulipuka kwa haraka sana na kusababisha maafa makubwa ya watu na vitu kwa muda mfupi mno.. Hata magari yake na sehemu za kuhifadhia hayo mafuta zina alama kubwa za tahadhari ya hatari INFLAMMABLE (VILIPUZI)
Ni taasisi gani imeruhusu hili jambo la hatari kiasi hiki katikati ya mji na makazi ya watu na bila kuzingatia umbali kama sheria inavyotaka?
Kuna kampuni imeotesha vituo vya mafuta kila kona ya jiji ndani na nje, kwenye makazi ya watu, kwenye misongamano, kwenye maofisi na hata karibia kabisa na ofisi za mamlaka ya juu ama nyeti... Mtandao wa hivyo vituo unaleta mashaka na kutia hofu kubwa hasa katika kipindi hiki dunia inapopambana na ugaidi wa kila aina
Imagine itakuwaje kikatokea kikundi cha magaidi (Eeh Mungu tuepushe) kikakamata vituo vinne tu katikati ya jiji na kuvilipua... !? Ninini kitatokea?

Miundombinu yetu na vifaa vyetu kwenye kupambana na majanga makubwa ya moto bado sana... Tumewekeza kwa nguvu sana kwingine kote lakini sio kwenye kikosi cha zima moto... Tunaishi tu kwa kudra za mwenyezi Mungu...!

Kampuni husika iliyootesha vituo husika ndani katikati ya jiji la Dar imeishia kupigwa faini ya Tsh bilion tatu... Achilia mbali kama zitalipwa ama la ... Swali la kujiuliza je tuko tayari kuhatarisha maisha ya mamalioni ya watu na mali zao kwa ajili ya bilion 3? Maana baada ya kupigwa faini pengine ataruhusiwa aendelee na biashara.. NADHANI...!
Ni ngumu kumwambia abomoe kwakuwa pengine ana nyaraka zote muhimu za kumruhusu kufanya ujenzi na kufanya biashara..! Akizuiwa ndio mwanzo wa kushikana uchawi na pengine hakuna aliye tayari kufanya hivyo! Kwakuwa pengjne kila mmoja kala kwa urefu wa kamba yake!

Ni mpaka pale tutakapopigwa tukio moja baya kubwa na la kustukiza ndio akili zitatukaa sawa! Lakini tutaunda na tume? Jibu ni ndio kwakuwa huo sasa umekuwa utamaduni wetu...!
Jiandaeni na wanasheria pamoja na wanamazingira na wataalamu wamipango miji nguli, thats money throughout and through... Sue .. sue ..sue
 
Hakuna kampuni inayokopesha mafuta kaka! BP, Oryx's,Total na mengineyo hawapo! Ni cash by cash unapewa mafuta!

Jambo jingine,sio wote wenye vituo vya mafuta ni vyao,watu hua wanakodisha hilo eneo,unakua unanunua mafuta kwenye kampuni husika tu! Mfano unakodi kituo cha Total Energies, wao ndiyo wanakua wanakuletea mafuta,kwa mashariti yao,ukienda kinyume na mashariti yao,wanachukua kituo chao!
Nadhani zipo zinazotoa kwa mali kauli lakini kwa mikataba maalum..huwezi kuchukua mzigo wa pili kabla hujalipia wa kwanza
 
Tujiulize maswali haya
Je mipango miji inaruhusu vituo vya mafuta katikati ya miji na makazi ya watu?
Je sera ya mamlaka ya viwango na ubora inaruhusu vituo vya mafuta katikati ya miji na makazi ya watu?
Vipi wizara ya miundombinu?
Vipi wizara ya mazingira?
Jeshi la zimamoto je nalo haliwezi kuhusika hapa?

Kimsingi pamoja na tahadhari zote za usalama zinazochukuliwa lakini bado haishauriwi kuwa na vituo vya mafuta katikati ya miji na makazi ya watu... Na sheria ya vituo vya mafuta inasema kuwe na umbali USIOPUNGUA kilometer 5 nadhani kati ya kituo kimoja hadi kingine
Mafuta ni kitu kinachoweza kulipuka kwa haraka sana na kusababisha maafa makubwa ya watu na vitu kwa muda mfupi mno.. Hata magari yake na sehemu za kuhifadhia hayo mafuta zina alama kubwa za tahadhari ya hatari INFLAMMABLE (VILIPUZI)
Ni taasisi gani imeruhusu hili jambo la hatari kiasi hiki katikati ya mji na makazi ya watu na bila kuzingatia umbali kama sheria inavyotaka?
Kuna kampuni imeotesha vituo vya mafuta kila kona ya jiji ndani na nje, kwenye makazi ya watu, kwenye misongamano, kwenye maofisi na hata karibia kabisa na ofisi za mamlaka ya juu ama nyeti... Mtandao wa hivyo vituo unaleta mashaka na kutia hofu kubwa hasa katika kipindi hiki dunia inapopambana na ugaidi wa kila aina
Imagine itakuwaje kikatokea kikundi cha magaidi (Eeh Mungu tuepushe) kikakamata vituo vinne tu katikati ya jiji na kuvilipua... !? Ninini kitatokea?

Miundombinu yetu na vifaa vyetu kwenye kupambana na majanga makubwa ya moto bado sana... Tumewekeza kwa nguvu sana kwingine kote lakini sio kwenye kikosi cha zima moto... Tunaishi tu kwa kudra za mwenyezi Mungu...!

Kampuni husika iliyootesha vituo husika ndani katikati ya jiji la Dar imeishia kupigwa faini ya Tsh bilion tatu... Achilia mbali kama zitalipwa ama la ... Swali la kujiuliza je tuko tayari kuhatarisha maisha ya mamalioni ya watu na mali zao kwa ajili ya bilion 3? Maana baada ya kupigwa faini pengine ataruhusiwa aendelee na biashara.. NADHANI...!
Ni ngumu kumwambia abomoe kwakuwa pengine ana nyaraka zote muhimu za kumruhusu kufanya ujenzi na kufanya biashara..! Akizuiwa ndio mwanzo wa kushikana uchawi na pengine hakuna aliye tayari kufanya hivyo! Kwakuwa pengjne kila mmoja kala kwa urefu wa kamba yake!

Ni mpaka pale tutakapopigwa tukio moja baya kubwa na la kustukiza ndio akili zitatukaa sawa! Lakini tutaunda na tume? Jibu ni ndio kwakuwa huo sasa umekuwa utamaduni wetu...!
Nieshangaa kuna mjini Songea kuna jamaa kanunua nyumba 5 katikati ya makazi ya watu na kuzivunja anajenga kituo cha mafuta, hii ni sawa kweli?
 
Nieshangaa kuna mjini Songea kuna jamaa kanunua nyumba 5 katikati ya makazi ya watu na kuzivunja anajenga kituo cha mafuta, hii ni sawa kweli?
Je eneo limepata kibali cha kubadili matumizi?
 
Uzuri wa bongo hata hayo tunayoita makazi ya watu utakuta hayako kisheria....
 
Labda uwe mteja mkubwa sana! Au uwe na collateral kutoka bank flan kaka!

Hii biashara,nilitamani kuifanya toka mwaka 2017,lakini shida ni hapo tu,hua nakwama kwenye collateral! Nishaenda sana onana na MDs wa Orxy, BP na Total Energies,lakini majibu yao ni kwamba uwe na mtaji,au upewe loan from Bank! Bank wanasema hawatoi start up loan,hua wanatoa loan kwenye business inayo run!
Duh je ukiweka advance let's say ya 20M?
 
Mshana tafuta pesa nduguyangu hayo mambo waachie wenyewe , yatakusumbua tu , we huoni mama yao kasema tozo zifutwe lakini jana tu mafuta yamepandishwa bei? nchi hii ngumu sana ndugu kuna mambo ukihangaika nayo yatakuletea taabu sana
 
Mshana tafuta pesa nduguyangu hayo mambo waachie wenyewe , yatakusumbua tu , we huoni mama yao kasema tozo zifutwe lakini jana tu mafuta yamepandishwa bei? nchi hii ngumu sana ndugu kuna mambo ukihangaika nayo yatakuletea taabu sana
Nimetimiza wajibu wangu... Maandishi hayafutiki
 
Hawakubali kaka! 20M ni mzigo kidogo sana! Wao wataka walau 500M huko! Maana lazima ulipie kwanza Kodi ya pango la kituo Chao! Mfano kwa dsm 5M kwa mwezi! Au 10M kwa mwezi! Maana yake hiyo ishafika 120M kwa mwaka!

Halafu uwe na uwezo wakuchukua mengi,kituo kisije kaukiwa mafuta hata kidogo! Nina jamaa yangu alikua pale Total Afirikana,akawazingua wenye kituo chao,wakamnyang'anya! Alikua ana make sana pesa pale! Jioni ukiwa unarudi home,unakuta folen kabisa ya magari pale,na kuna vituo vingine opposite,lakini watu hawaendi
Kumbe hii biashara ina huo umafia ndani yake!
Na hii biashara ina upigaji mkubwa ndani yake.. Kuna mhudumu mmoja pale Msata aliwahi kunimegea siri
Kuna mafuta ya dili ni ya transit lakini hayatoki nje ya nchi
Kuna mafuta ya wizi direct toka port
Kuna pump zinaibia wateja kwa settings za mmiliki
Kuna pump zinaibia wahudumu kwa settings za mmiliki
Kuna pump zinaibia wateja na mmiliki kwa ujanja wa wahudumu
 
Duh je ukiweka advance let's say ya 20M?
Kaka hebu soma kidogo mashariti yao hapo! Hizo gazeti nilitembea nalo sana kwenye banks za dsm! Sikuweza kupata msaadaView attachment 1966435
Screenshot_20211007-090107.jpg
 
Back
Top Bottom