Vituo vya kuchezea PlayStation na hatima ya kizazi cha sasa

Mphamvu

JF-Expert Member
Jan 28, 2011
10,702
3,288
Haya mabanda yanayotumika kuchezesha game kwa kulipia yamekuwa mengi jiji hili na hata mikoani. Si mbaya kwani ni burudani kama zilivyo burudani zingine lakini ningeomba tuangalie suala hili kwa mtazamo tofauti.

Michezo ya kompyuta, au gemu kama wanavyoita ni kitu chene uraibu (addiction) karibu sawa na vitu vingine hatari kama kamari na pombe. Wachezaji wa michezo hii wanaweza kutoa shuhuda zao jinsi mtu mzima na akili zake anaposhindwa kukakamilisha mambo yake ya msingi kwa kuwa alikuwa anacheza game.

Sasa hali inakuwa tishio zaidi kwani wanaopatwa na uraibu wa hii michezo ya kompyuta ni watoto hasa chini ya umri wa miaka 15 ambao wengi bado wangali shule na bongo zao zina mengi ya kujifunza. Michezo hii ikitawala sana akili ya mtu hujenga uvivu wa kimwili, kitu ambacho kinaweka msingi mbaya sana kwa mtoto na ni hatari kwa taifa letu changa.

Imefika wakati watoto hawa hutoroka shule ili kwenda kucheza hii michezo katika game, hapo sijasema madhara ya kiafya ya kukaa muda mrefu sehemu moja, kama mjuavyo, mwili unahitaji kufanya vimazoezi vya hapa na pale.

Jambo la kuogofya zaidi ni kuwa kucheza hii michezo kunataka pesa, kwa minajili hii kunaleta vichocheo kwa watoto kuiba pesa kwa wazazi wao, au kurubuniwa na pengine kujikuta wakifanyiwa vitendo vichafu kama kulawitiwa.

Sisemi isiwepo, maana kila mtu na starehe yake, lakini serikali za mitaa kwa kushirikiana na jeshi la polisi wanaweza kuweka muda na siku maalumu wa kufungua hivi vituo, mfano iwe kila siku kuanzia saa 10 jioni mpaka saa mbili usiku.

Tufikiri kwa ajili ya mustakabali wetu.
 
Mphamvu,

Kwa mawazo yako ni mawazo mazuri ila Serikali ingelikuwa inaweka

Sheria kuhusu michezo ya game ya Computer kuanzia wakati wa jioni saa 9 au saa 10 ndio waruhusiwe watoto kuingia

kwenye hiyo michezo ya Game ya Computer. Pasipo hivyo watoto wengi watakuwa hawana akili Mashuleni na watoto

wengi watakuwa ni watoro wa kwenda shule. Matokeo yake kwenye mitihani watakuwa watoto wengi wanafeli mitihani yao.

Wizara inayo husika ishughulikie hilo Suala watakaruhusiwa ni wale watoto wenye umri zaidi ya miaka18. Na Siku za

Jumamosi na jumapili watoto waruhusiwe tangu asubuhi mpaka jioni kuchezea hizo Game za kwenye Computer huo ni

ushauri wangu.
 
Lea tu mtoto vizuri, muwekee ndani halafu umpe limit ya kucheza, games ni entertainment nzuri hata inachangamsha ubongo, mtafutie favorite games na kama unaona hata mazoezi hafanyi mvutie Microsoft kinect ya XBOX ili acheze games kwa vitendo limtoe jasho kidogo, fanya hivo dogo nje hatoki, mimi nimekua mtu mzima sasa najua umuhimu wa games nilizocheza utotoni, hata kwenye career yangu experience zote zinachangia kitu fulani, technology imekua, mtoto asipokua exposed na different kinds of technology unamuonea
 
Kwa mawazo yako ni mawazo mazuri ila Serikali ingelikuwa inaweka

Sheria kuhusu michezo ya game ya Computer kuanzia wakati wa jioni saa 9 au saa 10 ndio waruhusiwe watoto kuingia

kwenye hiyo michezo ya Game ya Computer. Pasipo hivyo watoto wengi watakuwa hawana akili Mashuleni na watoto

wengi watakuwa ni watoro wa kwenda shule. Matokeo yake kwenye mitihani watakuwa watoto wengi wanafeli mitihani yao.

Wizara inayo husika ishughulikie hilo Suala watakaruhusiwa ni wale watoto wenye umri zaidi ya miaka18. Na Siku za

Jumamosi na jumapili watoto waruhusiwe tangu asubuhi mpaka jioni kuchezea hizo Game za kwenye Computer huo ni

ushauri wangu.

Usisahau bia inaruhusiwa kwa 18+ lakini ukiangakia wanywa bia underage ni wengi mno, Sasa serikali kufunga under 18 kucheza games kwa muda flani ni kitu ambacho its obvious kitakua cha ajabu sana, swala ni kumnyoosha mtoto mwenyewe aumize kichwa ajue kusoma napo ni muhimu, kumbana mtoto ni sawa na wale wa geti kali, siku akipata nafasi ni mauaji, afu kama akili ya. mtoto ni kwenye games, hapa ukimpiga ban mawazo yatakua kule tu, swala ni kutwist akili ya mtoto ione umuhimu wa kusoma, games are also important
 
Usisahau bia inaruhusiwa kwa 18+ lakini ukiangakia wanywa bia underage ni wengi mno, Sasa serikali kufunga under 18 kucheza games kwa muda flani ni kitu ambacho its obvious kitakua cha ajabu sana, swala ni kumnyoosha mtoto mwenyewe aumize kichwa ajue kusoma napo ni muhimu, kumbana mtoto ni sawa na wale wa geti kali, siku akipata nafasi ni mauaji, afu kama akili ya. mtoto ni kwenye games, hapa ukimpiga ban mawazo yatakua kule tu,

swala ni kutwist akili ya mtoto ione umuhimu wa kusoma, games are also important
Huku Ulaya Polisi

Wanakwenda kwenye Sehemu za internet Cafe kila wiki mara 3 wakikukuta unamuweka mtoto kwenye net Cafe mtoto

Under 18 wakati wa saa za watoto kwenda shule unashitakiwa na kupelekwa mahakamani unaweza kufungwa au kupigwa

faini. Inawezekana kama Serikali inataka hakuna kitu kisichowezekana Mkuu.
 
Kwa mawazo yako ni mawazo mazuri ila Serikali ingelikuwa inaweka

Sheria kuhusu michezo ya game ya Computer kuanzia wakati wa jioni saa 9 au saa 10 ndio waruhusiwe watoto kuingia

kwenye hiyo michezo ya Game ya Computer. Pasipo hivyo watoto wengi watakuwa hawana akili Mashuleni na watoto

wengi watakuwa ni watoro wa kwenda shule. Matokeo yake kwenye mitihani watakuwa watoto wengi wanafeli mitihani yao.

Wizara inayo husika ishughulikie hilo Suala watakaruhusiwa ni wale watoto wenye umri zaidi ya miaka18. Na Siku za

Jumamosi na jumapili watoto waruhusiwe tangu asubuhi mpaka jioni kuchezea hizo Game za kwenye Computer huo ni

ushauri wangu.

Hapa unaizungumzia serikali ipi?
 
Kuna kipindi nilitaka kufungua kijisehemu cha watoto kucheza game (hata mi napenda sana game)lakini kuna siku nilienda cafe nikakuta dogo kavaa uniform anacheza game mpaka amejikojolea kwenye kiti na ameng'ang'ana hpo nikaachana kabisa na huo mpango mana nikaamini nitahikumiwa kwa kuharibu taifa hili kesho
 
cha muhimu ni kuifahamu zaidi teknolojia si kuipinga. watoto ambao kwao mambo safi mbona wanazo majumbani kwao kabisa na hakuna madhara?
 
karibun tucheze GTA vice city na FIFA.
kila mtu na starehe yake mlitaka hao watoto wanyee pombe au wacheze kibaba na mama wagegedane?

game ni nzuri sana inafanya akili ya mtoto kuchangamka kwa haraka .

marekani kuna watoto wa miaka 6 ushikwa wakiendesha gari ukifatilia zahidi utagundua wamejifunzia kwenye magemu.

cha muhimu ni kutenga muda maalumu ambao si wamasomo ili wacheze game.

nina rafik zangu 3 mmoja black america na wawili wachina ndoa zao zimevunjika sababu ya hao rafik zangu kucheza game usiku kucha.

game zina faida na hasara zake kama ilivyo michezo mingine ila kwa mtoto game ni burudani tosha na ukimuwekea game ndani hawezi kuzurula
 
Lea tu mtoto vizuri, muwekee ndani afu umpe limit ya kucheza, games ni entertainment nzuri hata inachangamsha ubongo, mtaftie favorite games na kama unaona hata mazoezi hafanyi mvutie Microsoft kinect ya XBOX ili acheze games kwa vitendo limtoe jasho kidogo, fanya hivo dogo nje hatoki, mimi nimekua mtu mzima sasa najua umuhimu wa games nlizocheza utotoni, hata kwenye career yangu experience zote zinachangia kitu flani, technology imekua, mtoto asipokua exposed na different kinds of technology unamuonea
Kwa sisi tunaoishi uswahilini ngumu!
 
Kikubwa ni kuweka limit tu vinginevyo wanaomaliza shule ya msingi bila kujua kusoma wala kuandika watazidi zaidi ya hawa wa sasa
 
Kwa sisi tunaoishi uswahilini ngumu!
Sasa kama mtu anaishi pande za uswahilini muda na hela ya kwenda kucheza playstation anaitoa wapi?
Kama ambavyo hawezi kumiliki playstation basi pia hawezi kua na hela ya kucheza masaa 12 kwenye centre, labda akusanye hela ya nusu saa tu, mtu hawezi kua na hela ya kutoroka shule daily kupoteza muda kwenye games afu home wakakosa ya kumnunulia gaming console unless ni mwizi which brings us to a different problem sasa, huyo ni wa kushughulikiwa kivingine
 
  • Thanks
Reactions: vvm
Lea tu mtoto vizuri, muwekee ndani afu umpe limit ya kucheza, games ni entertainment nzuri hata inachangamsha ubongo, mtaftie favorite games na kama unaona hata mazoezi hafanyi mvutie Microsoft kinect ya XBOX ili acheze games kwa vitendo limtoe jasho kidogo, fanya hivo dogo nje hatoki, mimi nimekua mtu mzima sasa najua umuhimu wa games nlizocheza utotoni, hata kwenye career yangu experience zote zinachangia kitu flani, technology imekua, mtoto asipokua exposed na different kinds of technology unamuonea

Watoto wa kishua ndio wameathirika sana na gaming, hawajichanganyi na wenzao na dizaini ni wazembe wazembe fulani ivi. Obzavesheni imefanyika Dar.
 
Sasa kama mtu anaishi pande za uswahilini muda na hela ya kwenda kucheza playstation anaitoa wapi?
Kama ambavyo hawezi kumiliki playstation basi pia hawezi kua na hela ya kucheza masaa 12 kwenye centre, labda akusanye hela ya nusu saa tu, mtu hawezi kua na hela ya kutoroka shule daily kupoteza muda kwenye games afu home wakakosa ya kumnunulia gaming console unless ni mwizi which brings us to a different problem sasa, huyo ni wa kushughulikiwa kivingine
Kununua hiyo shetani ni laki kadhaa, lakini kucheza session moja ya kibandani ni mia mbili kama sikosei. Mtoto akiwa na buku (kitu ambacho kinawezekana) anacheza session tano.

Yawezekana mtu akakaa uswazi na akaweza kucheza hii ya vibandani.
 
Back
Top Bottom