Vituo vitatu vikubwa vya televisheni nchini Kenya vimezima mitambo

Kibo10

JF-Expert Member
Aug 20, 2013
11,277
8,840
Vituo vitatu vikubwa vya televisheni nchini Kenya vimezima mitambo yao baada ya Mahakama Kuu nchini humo kutoa uamuzi kwamba vinapaswa kuingia katika mfumo wa utangazaji wa dijitali na kuachana na mfumo wa analojia. Vituo hivyo vya Standard Group, Nation Media Group na Royal Media Services, awali vilikwenda mahakamani kuomba kuahirishwa muda wa kuhamia kwenye mfumo huo, hadi masuala kadhaa yatakapofafanuliwa. Jee, una maoni gani?
 
Kumbe Kenya na ujanja wote wao wa kupenda misifa walikua bado wako analojia. Maoni yangu ni kwamba wahamie digito haraka sana. Over.
 
Back
Top Bottom