beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Tume ya uchaguzi katika Jamhuri ya Afrika ya kati imesema zaidi ya asilimia 14 ya vituo vya kupigia kura nchini humo, vilishindwa kuendesha zoezi la kura ya urais na bunge kutokana na waasi kuwavamia wapiga kura na maafisa wa uchaguzi. Takribani vituo 800 kati ya 5,408 vya kupigia kura nchi nzima, havikufunguliwa siku ya uchaguzi uliofanyika jumapili.
Kulingana na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Theophile Momokouama, baadhi ya wapiga kura walipigwa na kutishiwa kuuawa. Jamhuri ya afrika ya Kati iliyo na utajiri wa almasi na dhahabu imekuwa ikikabiliana na wimbi la machafuko ya wanamgambo tangu mwaka 2013, ambayo yamewaua maelfu ya raia na kuwalazimisha zaidi ya milioni kuyakimbia makaazi yao.
Kampeni za uchaguzi ziligubikwa na ghasia kutoka makundi ya waasi ambayo yaliapa kuvuruga uchaguzi.
Kulingana na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Theophile Momokouama, baadhi ya wapiga kura walipigwa na kutishiwa kuuawa. Jamhuri ya afrika ya Kati iliyo na utajiri wa almasi na dhahabu imekuwa ikikabiliana na wimbi la machafuko ya wanamgambo tangu mwaka 2013, ambayo yamewaua maelfu ya raia na kuwalazimisha zaidi ya milioni kuyakimbia makaazi yao.
Kampeni za uchaguzi ziligubikwa na ghasia kutoka makundi ya waasi ambayo yaliapa kuvuruga uchaguzi.