Vituo 13 vya habari, vyafungiwa nchini Uganda

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,495
9,275
Tume ya mawasiliano ya nchini Uganda imeagiza kufungwa kwa vituo 13 vya radio na Televisheni pamoja na kufutwa kazi baadhi ya wanahabari kwa ''kupotoshaji' na kuchochea ghasia kwa kutangaza taarifa zilizo na "ujumbe na hisia kali".

Tume hiyo inasema kuwa vyombo hivyo vya habari vilikiuka kanuni ya kifungo cha 31 ibara ya 4 ya sheria ya mawasiliano ya Uganda ya mwaka 2013.

Japo kuwa haikufafanua jinsi sheria hiyo ilivyokiukwa katika agizo lake kwa vyombo hivyo vya habari ikiwa ni pamoja na - Vituo vya televisheni vya NBS, Bukedde TV, NTV, CBS FM na Capital FM.

Inataka hatua dhidi ya wazalishaji vipindi, wahariri wa kuu na wasimamizi wa matangazo kusimamishwa kazi katika mda wa siku tatu.

"Hii ni kufuatia jinsi zinavyoshughulikia mada zinazopeperushwa hewani wakati wa matangazo ya moja kwa moja, Habari za hivi punde na Habari zingine kwa ujumla bila kuzingatia kanuni ," iliongeza Tume ya UCC.

Hatua hiyo imepokelewaje?
Chama cha wanahabari nchini Uganda (UJA) kimeelezea kughadhabishwa na hatua hiyo.

''Wanahabari karibu 30 wanakabiliwa na tishio la kufutwa kazi na hili litakuwa na athiri kwa taalumu zao tu bali mamilioniya waganda watakosa huduma ya kupashwa habari'' alisema taarifa ya chama hicho.

UJA pia iliongeza kuwa serikali kupitia mashirika yake ya udhibiti wa mawasiliano inatakiwa kuheshimu uhuru wa vyombo vya habari.

Kuna madai kuwa huenda hiyo imetokana na mtangazo ya moja kwa moja ya kukamatwa na kushtakiwa kwa mbunge wa Kyadondo Mashariki, Robert Kyagulanyi maarufu Bobi Wine.

Kyagulanyi kwa sasa anazuiliwa rumande na anatarajiwa kufikishwa tena mbele ya hakimu mkuu wa mahakama ya Buganda Road leo Alhamisi.


BBC
 
Tume ya mawasiliano ya nchini Uganda imeagiza kufungwa kwa vituo 13 vya radio na Televisheni pamoja na kufutwa kazi baadhi ya wanahabari kwa ''kupotoshaji' na kuchochea ghasia kwa kutangaza taarifa zilizo na "ujumbe na hisia kali".

Tume hiyo inasema kuwa vyombo hivyo vya habari vilikiuka kanuni ya kifungo cha 31 ibara ya 4 ya sheria ya mawasiliano ya Uganda ya mwaka 2013.

Japo kuwa haikufafanua jinsi sheria hiyo ilivyokiukwa katika agizo lake kwa vyombo hivyo vya habari ikiwa ni pamoja na - Vituo vya televisheni vya NBS, Bukedde TV, NTV, CBS FM na Capital FM.

Inataka hatua dhidi ya wazalishaji vipindi, wahariri wa kuu na wasimamizi wa matangazo kusimamishwa kazi katika mda wa siku tatu.

"Hii ni kufuatia jinsi zinavyoshughulikia mada zinazopeperushwa hewani wakati wa matangazo ya moja kwa moja, Habari za hivi punde na Habari zingine kwa ujumla bila kuzingatia kanuni ," iliongeza Tume ya UCC.

Hatua hiyo imepokelewaje?
Chama cha wanahabari nchini Uganda (UJA) kimeelezea kughadhabishwa na hatua hiyo.

''Wanahabari karibu 30 wanakabiliwa na tishio la kufutwa kazi na hili litakuwa na athiri kwa taalumu zao tu bali mamilioniya waganda watakosa huduma ya kupashwa habari'' alisema taarifa ya chama hicho.

UJA pia iliongeza kuwa serikali kupitia mashirika yake ya udhibiti wa mawasiliano inatakiwa kuheshimu uhuru wa vyombo vya habari.

Kuna madai kuwa huenda hiyo imetokana na mtangazo ya moja kwa moja ya kukamatwa na kushtakiwa kwa mbunge wa Kyadondo Mashariki, Robert Kyagulanyi maarufu Bobi Wine.

Kyagulanyi kwa sasa anazuiliwa rumande na anatarajiwa kufikishwa tena mbele ya hakimu mkuu wa mahakama ya Buganda Road leo Alhamisi.


BBC
'Kicks of a dying horse' m7 mda wowote anaondolewa na wananchi wa Uganda
 
M7 Anatakiwa atulize mshono aangalie mwenzake wa Sudan hali aliyonayo.
 
Back
Top Bottom