Ninaomba wataalamu wa uchumi na mambo ya fedha wanisaidie katika hili.
Nilibahatika kwenda Thailand mwaka jana na nilikuwa na kama USD 600 ambazo jamaa alinituma nimnunulie laptop.Nilifika katika shopping mall majira ya saa moja usiku na jamaa walikataa kupokea USD na wakanitaka nibadili katika pesa ya kwao,nikashangaa!!Bahati mbaya bank zilikuwa zimefungwa na jamaa wakagoma kupokea USD ila wakaniahidi kuniwekea laptop niliyochagua mpaka kesho yake nitakapokuja na bhat (pesa za Thailand).
Juzi nilikuwa mlimani city na nikauliza bei ya simu na nikajibiwa katika USD,nilipohoji ikiwa sina USD itakuwaje nikajibiwa ya kuwa watabadilisha Tshs kwa rate yao na si ya bank au beuraeu de change.
Je kweli tuna udhibiti na fedha ya kigeni nchi hii,nisaidieni.
Jambo la pili ni kuwa nilifika katika soko la Mawenzi Morogoro hivi karibuni na katika vitu nilivyotumwa na Bi Mkubwa ni vitunguu swaumu.
Nilipouliza kwa wauzaji nilijibiwa kwa kupewa swali hili vya Tanzania au vya China? nikashtuka nami nikawauliza kuwa hivyo vya China ni kuwa vimelimwa na Wachina hapa nchini au vimeingizwa kutoka China?haraka nikajibiwa kuwa vimeingizwa toka China na nusu kilo ni shs 3000!!
Nilibahatika kwenda Thailand mwaka jana na nilikuwa na kama USD 600 ambazo jamaa alinituma nimnunulie laptop.Nilifika katika shopping mall majira ya saa moja usiku na jamaa walikataa kupokea USD na wakanitaka nibadili katika pesa ya kwao,nikashangaa!!Bahati mbaya bank zilikuwa zimefungwa na jamaa wakagoma kupokea USD ila wakaniahidi kuniwekea laptop niliyochagua mpaka kesho yake nitakapokuja na bhat (pesa za Thailand).
Juzi nilikuwa mlimani city na nikauliza bei ya simu na nikajibiwa katika USD,nilipohoji ikiwa sina USD itakuwaje nikajibiwa ya kuwa watabadilisha Tshs kwa rate yao na si ya bank au beuraeu de change.
Je kweli tuna udhibiti na fedha ya kigeni nchi hii,nisaidieni.
Jambo la pili ni kuwa nilifika katika soko la Mawenzi Morogoro hivi karibuni na katika vitu nilivyotumwa na Bi Mkubwa ni vitunguu swaumu.
Nilipouliza kwa wauzaji nilijibiwa kwa kupewa swali hili vya Tanzania au vya China? nikashtuka nami nikawauliza kuwa hivyo vya China ni kuwa vimelimwa na Wachina hapa nchini au vimeingizwa kutoka China?haraka nikajibiwa kuwa vimeingizwa toka China na nusu kilo ni shs 3000!!