Vitunguu ndo vinapaswa kutuliza na sio mapenzi

SectionTwenty

JF-Expert Member
Aug 3, 2013
674
604
Kawaida ukiwa unamenya au kukata vtunguu unaeza kutoka machozi.... asa kuna mijitu ipo katika mapenzi na binadam wenzao ila unaeza ukahisi wanapendana na vitunguu maana hawaishi kutoa MACHOZI...

Kama unajijua umekufa umeoza kwa mpenzi wako na hujiwezi basi usjisumbue sana kumchunguza.
Mara "Oooh beby nipe password zako za FB nijue unachat na akina nan Inbox" hujakaa sawa "mpenzi naomba simu yako niiangalie" Yaan mkono unakuwasha umpekue mpenzi wako... Huo ni UJINGA

Unajijua ubavu wa kumuacha huna ila unahangaika kumchunguza kama afisa upelelez usalama wa taifa... huko ni KUJITESA na utakua unatoa MACHOZI daily... haya ushagundua sasa anafanya ndivyo sivyo haya basi muache,, eti huwezi umekufa umeoza... SHENZIIIIIII... Unaishia kulia lia kama umetupiwa bomu la machozi kwenye maandamano.

Kama una mahaba niue kwa mpenz wako we kausha tu usianze upelelezi kama unaigiza tamthilia ya "IRIS".... acha hayo mambo yakufate mwenyewe uyajue kwa bahati mbaya sio uanze kuyapekua pekua.

Hizi kazi za kututoa machozi tuviachie vitunguu... Kama una hamu ya kulia lia we nenda kamenye vitunguu utaona shughuli yake sio kumpekua mpenzi wako na unajijua kumuacha huwezi.... utabaki unalia utataman ata usingejua... na nyie ndo mnajitafutia kifo kwa presha za kushuka shauri yenu. Dedication Song "I don't wanna know by Mario winans"
√√√√√
 
Wacha watu walilie tamuuuu..Hakuna educated wala mtoto wa mtaani. wote choziiiii.
 
Mi huwa nikiwaza kukupekua roho yangu ikisema pekua ujue kuna kitu na huwa sikosei ila kulia ilikua zamaniii siku hiz bana kwaheri ya kuonana baba
 
vitunguu silii hata kama vya sumbawanga!!! ila mapenzi naweza kulia
 
Nina hamu ya kubemenda mutu, nikikumbuka mapenzi yalivyo niliza hadi nikalazwa Igogwe hospitali mweee, andikwibwamo siku......
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom