Vituko vya watoto na ripoti za matokeo

Aaah baada ya hapo ndio ilibidi niwe na mawasiliano mujarab na mwalimu wake maana mambo ya "mama wewe hujui" siyataki tena

Maana wakati nimekazana na ile ya zamani akawa ananitazama tu usoni kama hanisomi hivi, ndio akaona mambo yasiwe mengi akanyanyuka na daftari lake
Mimi nltaka niwafate walimu wao bwana wee sisi tunalipa hawa muwafundishe halafu nyie mnazngua mnaleta maswali magumu 🤦🏾‍♂️
 
Watoto ndo wanarudi likizo

Swalehe hapa karudi kawa wa 34 namwuliza imekuwaje umeporomoka toka namba moja ananambia

Baba kwani elfu moja na elfu kumi ipi kubwa nkamjibu elfu kumi

Akanambia Basi sawa mzee , Mimi ndo namba kubwa hapo kuliko wote na kuliko pacha wake Micaela (yeye kawa wa tano )nmeshindwa kumjibu chochote maana Kuna homework alileta akakosa zote nlifanya nae kwenda shuleni wakamwambia wewe na baba yako wote wajinga

Nmewaacha na ugomvi hapa yeye na dada ake waamue nani ana namba kubwa

Wewe umekutana na kituko gani ?
Kama na wewe umeandika utumbo huu,ni dhahiri akili yako ni sawa na ya walevi kumi wakikaa pamoja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah wadogo zangu safari hii sijawaelewa kabisa matokeo yao mmoja yupo Darasa la kwanza amekua wa 42 afu ukimuuliza ni mkali anajibu "nimeshasema nilikua wa 42" aaii akaambiwa subiri mdingi arudi umwambie hivo eeh si akarudi jioni ulikua wa ngapi 42? Kamechapwa hadi kamenyooka. Dada mwingine kaporomoka kawa 25 wakti alikuaga top 5 naye fimbo tu kaahidi atafanya vizuri, yupo darasa la 5🤔
 
Dah,masuala ya elimu kwa watoto wadogo bana yanafurahisha,jirani mmoja alipelekewa swali la hisabati sehemu(kuzidisha na kutoa)na mtoto wake ikabidi amkimbilie jirani yake wa nyumba ya pili akafanye hilo swali la hisabati...
 
Yes,wanunulie but kwa hayo makubaliano kuwa ni Mkopo,unawadanganya wakifail Dec kufikia malengo unabeba Bicycles zako,nakuhakikishia hapatakalika,maana watakuwa wameshaonja na uzuri wa kuride bicycles.
mimi binafsi sikubaliani na kumuahidi mtoto zawadi ndio afaulu, kufaulu kwa mtoto kunapaswa kuwa ni wajibu wake, ila akishafaulu unaweza kumpa zawadi.

siku kusipokua na zawadi/ahadi itakuwaje?
 
Huu uzi ulikuja kama joke lakini nikiuangalia kwa jocho la tatu hii sio joke. Ni uhalisia.

Kijana wangu, nimemtupa lockup baada ya kufanya vibaya. Ki ukweli kafail haswa. Na ni std 7 graduate to be. Sasa nikamweka lockup kwa siku nzima ya j'mosi iliyopita. Lengo lilikuwa ni kumchimba bit.
Sasa akitoka tuition haendi popote ni kujisomea tu.
 
Huu uzi ulikuja kama joke lakini nikiuangalia kwa jocho la tatu hii sio joke. Ni uhalisia.

Kijana wangu, nimemtupa lockup baada ya kufanya vibaya. Ki ukweli kafail haswa. Na ni std 7 graduate to be. Sasa nikamweka lockup kwa siku nzima ya j'mosi iliyopita. Lengo lilikuwa ni kumchimba bit.
Sasa akitoka tuition haendi popote ni kujisomea tu.

Nadhani harudii tena.Hapa Mkuu tunashare real experience na inatusaidia sana kama mtoto anatatizo kupata mawazo mbadala.
 
mimi binafsi sikubaliani na kumuahidi mtoto zawadi ndio afaulu, kufaulu kwa mtoto kunapaswa kuwa ni wajibu wake, ila akishafaulu unaweza kumpa zawadi.

siku kusipokua na zawadi/ahadi itakuwaje?

But pia hii inaweza kuwa kama motisha ya kumpush afanye vizuri zaidi.Kumbuka kuna watoto wengine ni average,wanahitaji kuwa pushed ili wafanye vizuri,so ahadi ya zawadi itamfaa zaidi mtoto huyu.Ni kama tu wewe kazini unavyopewa malengo na ukiyafikia unapata bonus,why huwa unapewa malengo na mwajiri wako?
 
But pia hii inaweza kuwa kama motisha ya kumpush afanye vizuri zaidi.Kumbuka kuna watoto wengine ni average,wanahitaji kuwa pushed ili wafanye vizuri,so ahadi ya zawadi itamfaa zaidi mtoto huyu.Ni kama tu wewe kazini unavyopewa malengo na ukiyafikia unapata bonus,why huwa unapewa malengo na mwajiri wako?
ziko njia nyingi za kumpush mtoto zaidi ya hiyo ya ahadi, hata kazini napewa malengo baada ya KUYAFIKIA ndo napewa zawadi, hata mtoto unaweza kumpa malengo na kutumia njia nyinginezo kumpush, baada ya kuyafikia malengo ndio unampa zawadi, na sio ahadi ili ayafikie malengo.

hii tabia inawaathiri sana watoto hatujui tu, haina tofauti na ile unamtuma mtoto dukani kwa ahadi kuwa akienda atapewa pipi au chenchi, unampa kazi kwa ahadi akifanya unampa zawadi..
hii kwanza itamfanya mtoto asijue kuwa kusoma na kufaulu ni wajibu wake,
pili hii tabia anakua nayo hadi akiwa mkubwa kila anachokifanya (hata kama ni wajibu wake) anatarajia "kupoozwa" na asipoozwa hafanyi. nadhani unanielewa namaanisha nini? tunaandaa kizazi cha wala rushwa. Rushwa nyingi tu zinaanzia nyumbani na sisi wazazi ndio tumekua watoaji wazuri wa rushwa, kwa kisingizio cha kumpush mtoto.

sasa ndio unaona mheshimiwa hapo analalamika kuwa watoto wenyewe wameshindwa kufikia malengo na wamemnunia.. sasa fikiria wangefikia malengo alafu mzazi kwa namna moja au nyingine ashindwe kutekeleza makubaliano... can you imagine hapo ingekuwaje??
 
Nadhan hawa waliomfanyia hv huyu mwamba lengo halikua kumfunza labda walitaka kumtesa na sijui alifanya kosa gani
Screenshot_20210130-120629.jpg
 
Back
Top Bottom