Vituko vya Wadada kazi za ndani (House Girl )

bushland

JF-Expert Member
Mar 6, 2015
7,016
4,961
Jamani wadada wa siku hizi ni moto,

Wengi hawakai hata mwezi,
Jirani yangu kaleta Mdada nyumba ni full geti, (getikali) binti hakuna kutoka kila kitu kipo ndani

Basi siku moja wenye nyumba wameenda kwenye harusi kurudi usiku wanakuta na viatu vya kiume nje kucheki kumbe binti na jamaa wamejisahau baada ya kufanya yao wakapitiwa na usingizi, varangati baadaye Dada akaondolewa.

Kisa Kingine wenye Nyumba wanaondoka binti nae anasepa anawafungia Watoto ndani Watoto wanalia we wanajipupulia humohumo ndani majirani wakambonyezea Mama mwenye nyumba duh balaa,

Ntaendelea na vingine baadaye,
balaa lingine ni kwenye simu, usiku mzima ni kuchati

Waweza ongezea na vya kwako ulivyoviona au kukutokea wewe
 
Nafikiri hawa wenzetu kwa kuwa wanaacha makazi yao na kukaa/ kuishi kazini, basi wanachukuliwa kama ni mashine hivi, hawana mahitaji ya kimwili.

Wapeni siku za mapumziko, watoke, hamtakumbana na vituko. Geti kali, kwani mwanao huyo? Hata huyo mtoto unamtoa nje.
 
Tatizo majirani mnawabania Sana hawa viumbe nao ni binadamu wanahitaji mikuyenge,Uhuru nk.๐Ÿ˜Ž๐Ÿ˜Ž๐Ÿ˜Ž
 
Sisi wanaume hivyo visa tutavijulia wapi? Nyie wanawake ndo mnayajua hayo.


Jamani wadada wa siku hizi ni moto, wengi hawakai hatamwezi,
Jirani yangu Kaleta mdada nyumba ni full geti, (getikali) binti hakuna kutoka kila kitu kipo ndani basi siku moja Wenye nyumba wameenda kwenye harusi kurudiusikuwanakuta na viatu vya kiume nje kucheki kumbe binti na jamaawamejisahau baada ya kufanya Yao wakapitiwa na usingizi, varangati badae dada. Kuondoka,
Kisa Kingine Wenye nyumba wanaondoka binti nae anasepa anawafungia watoto ndani watoto wanalia wee wanajipupulia humohumo ndani maji rani wakambonyezea mama mwenye nyumba duh balaa,
Ntaendelea na vingine badae,
Balaa lingine ni kwenye simu, usiku mzima ni kuchati

Waweza ongezea na vya Kwako ulivoviona au kukutokea wewe
 
Ni wazi kuwa hawajuagi kukataa..

However you may not start conversation with the following recipient;Tairus
 
Wengi wamekarambuka kishamba!
Wakishazoea wanajisahau kabisa...
Mmoja alisema yeye alikuwa anataka tu kutoka kule kijijini kwao...aje kujionea mji...sio kukaa ndani afanye kazi!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom