Vituko vya Rais Kikwete dhidi ya Albino

Ileje

JF-Expert Member
Dec 20, 2011
8,784
12,227
Wakati bajeti ya wizara ya afya imekwisha somwa na kupitishwa bungeni kwa mwaka 2015/16, eti JK atahakikisha vifaa na madawa kwa ajili ya watu wenye albinism yanatengewa fedha na kununuliwa na kwamba vyote vitakuwa bure! Ahadi hii ameitoa leo huko Arusha katika sherehe ya siku ya kimataifa albinism!

Hiki ni kituko kwani waziri wake wa afya hakuzungumzia cho chote kuhusu suala hilo wakati wa bajeti ya afya! Na kama JK atalazimisha kutekelezwa kwa ahadi basi ama bajeti ya wizara itavurugika au itakuwa ahadi mpya ambayo haitatekelezeka hadi anamaliza muda wake October mwaka huu!!

Cha kujiuliza hivi JK hakomi kuahidi ahadi hewa au haoni aibu kwa kutotekelezeka kwa ahadi lukuki alizowaahidi wananchi nchini kote mwaka 2010?!


====================================

Dar/Arusha. Rais Jakaya Kikwete ametokwa na machozi wakati akisikiliza wimbo ya masikitiko ya watoto wenye ulemavu wa ngozi (albino), na akaeleza kuwa ni upumbavu kuamini kuwa viungo vyao vinaleta utajiri.

Akizungumza katika maadhimisho ya kimataifa ya siku ya kuongeza uelewa wa albino duniani, katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Rais Kikwete alisema mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi yanayoendelea nchini yanamsononesha na kulitia doa Taifa.

Rais Kikwete alisema wimbo wa watoto wenye albino kutoka Tanga, ulivyoanza alianza kuhisi angetokwa machozi na baadaye alishindwa kujizuia na kutokwa na machozi.

"Hawa watoto wameimba mambo ambayo yamenigusa sana, na tumepokea kilio chenu kwa umuhimu mkubwa na ninaahidi tutashirikiana kuyashughulikia matatizo yenu," alisema.

Alisema suala la matibabu ya albino ni jambo ambalo linashughulikiwa, ili kuhakikisha vifaa tiba ambavyo vinahitajika hasa kutibu magonjwa ya ngozi vinapatikana na kuwawezesha kupata matibabu bure.

Akizungumzia hatua za Serikali, Rais Kikwete alimpa nafasi Waziri wa Mambo ya Ndani, Mathias Chikawe kueleza hatua zilizofikiwa katika kuunda kamati ya kitaifa ya kuishauri Serikali.

Waziri Chikawe alieleza kuwa tayari wizara yake, imekamilisha mchakato wa kuunda kamati hiyo, ambayo itakuwa na wajumbe 15, watano kutoka chama cha wenye albino, watano chama cha waganga wa jadi na watano kutoka serikalini.

Awali Mwakilishi ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (Unicef) nchini, Zulmira Rodrigues aliiomba Serikali kuwaondoa watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) waliowekwa katika vituo maalumu, kwa kuwa kitendo hicho kinawanyanyapaa.

Akizungumza katika mkutano uliokuwa wa kuelezea maadhimisho ya siku ya kimataifa ya uelimishaji kuhusu albino jijini hapa jana, Rodrigues alisema vituo hivyo vinaweza kutumika kwa ajili ya kuwahifadhi albino kwa muda mfupi na si kuvifanya suluhisho la kudumu litakalowapa ulinzi.

"Kuwatenga albino na kuwaweka katika vituo ambavyo wanaishi pekee yao ni kukiuka haki za binadamu na kuwanyima uhuru wao, badala yake jamii iwatengenezee mazingira mazuri yatakayowafanya waishi kwa usalama kama watu wengine," alisema Rodrigues.
Chanzo: Mwananchi
 
Wakati bajeti ya wizara ya afya imekwisha somwa na kupitishwa bungeni kwa mwaka 2015/16, eti JK atahakikisha vifaa na madawa kwa ajili ya watu wenye albinism yanatengewa fedha na kununuliwa na kwamba vyote vitakuwa bure! Ahadi hii ameitoa leo huko Arusha katika sherehe ya siku ya kimataifa albinism!

Hiki ni kituko kwani waziri wake wa afya hakuzungumzia cho chote kuhusu suala hilo wakati wa bajeti ya afya! Na kama JK atalazimisha kutekelezwa kwa ahadi basi ama bajeti ya wizara itavurugika au itakuwa ahadi mpya ambayo haitatekelezeka hadi anamaliza muda wake October mwaka huu!!

Cha kujiuliza hivi JK hakomi kuahidi ahadi hewa au haoni aibu kwa kutotekelezeka kwa ahadi lukuki alizowaahidi wananchi nchini kote mwaka 2010?!
Jamani hebu tuache kumdhihaki mkulu waziri wake aliyasema hayo kwa ufasaha kabisa
 
Watanzania ni wajinga sana. Dawa yao kuwaambia uongo kwa sabb uongo ni mwepesi kueleweka. Big up my president!
 
Naye Jk na CCM yake akawaambia MAWAZIRI wake na wanachama wa CCM

KESHENI mkiomba kwani hamjui siku wala saa atakayokuja Dr
Slaa na UKAWA yake,Nami naenda Ulaya kuwaandalia MAKAZI ya kudumu,ili nitakapokuwa nanyi
muwepo,kwani CHADEMA ikichukua nchi mwaka huu,lazima mafisadi tuhame nchi.

Nanyi muonapo wa-Tz wanaipinga sana CCM na kuisapoti CHADEMA ,huku tume mbalimbali zikiundwa, basi mtambue muda wa wa MATESO kwa MAFISADI
umekaribia.

Wala msitishwe na wingi wa watia nia wenu wa CCM,kwani hata Lowassa mwenye pesa nyingi za KIFiSADI,lakini kamwe hawezi kuwa rais wa nchi hii.

Kisha Lowassa alipoyasikia hayo na kauli za makutano,basiakakwea tena IKULU kumuomba Rais ASIMFILISI,ASIMFUNGE WALA ASIKUBALI LOWASSA AJIUZURU, Lakini kabla ya wananchi hawajamsahau Lowassa na ufisadi wa RICHMOND,EPA,na RADA na ndicho kipindi yule katibu mkuu wa CCM mwizi wa tembo akijiandaa kuanzaa ziara za kuwahadaa wananchi mikoa mbalimbali,
akatokea Kafulila,Mbowe ,Mnyika na Zitto na jeshi lao lote wakaibua ufisadi wa ESCROW,na Kafulila akasema na "Nitakaowabusu hao ndio wezi waliokula pesa za Escrow na kulifisi taifa",basi akiwa bungeni akawataja jaji Werema,Pinda na Chenge nayo kamati ya PAC kupitia Zitto Kabwe ikawataja wengine wengi hata wale waliokuwa wamefichwa na wengine walioiba na kubeba fedha kwenye magunia kule kwenye benki ya Stanbic,bt Ikulu ikawalinda.

Mara AG WEREMA akatoa UPANGA ALANI na kumtishia Kafulila,mfuasi wa UKAWA kutaka kumkata shingo,ndipo PINDA kwa fedheha kubwa akamwambia WEREMA"rudisha upanga wako
alani,KIKOMBE tulichotupiwa na Kikwete hatunabudi Kukinywa.

Moja kati wa mayahudi wale aitwaye Muhongo hakuamini kama Kafulila
anaweza kitikisa serikali,mara TIBAIJUKA akasimama na kusema yeye hakujua kama pesa aliyokula ilikuwa ni ya kifisadi ya Escrow na Rugemalila aliyempa,ati alimpa kama kaka yake kwa ajili ya shule zake za Kajumulo

Basi siku ya3 wezi wakaenda pale ofisini kwa spika na ofisi ya PAC ili waibe nyaraka,lakini wakazikosa.

yule morani waliyemkuta getini
akawaambia mnayemtafuta(document za PAC) hazipo..Kafulila na Zzk wameshapaa nazo kwenda Kigoma na wapo
kuume kwa UKAWA

Basi wanaCCM walipoyaona hayo,kwa masikitiko wakasema"HAKIKA MWAKA HUU LAZIMA CCM ING'OKE NA CHADEMA KUPITIA UKAWA WACHUKUE NCHI"
 
President anauwezo na mamlaka kikatiba kutamka lolote na likatekelezwa...over!

Kama ndio hivyo ile meli mpya na kubwa ziwa victoria na uwanja wa ndege wa kimataifa wa bukoba vitapatikana mwaka huu,ndugu zangu wahaya mpooooooo?
 
Wakati bajeti ya wizara ya afya imekwisha somwa na kupitishwa bungeni kwa mwaka 2015/16, eti JK atahakikisha vifaa na madawa kwa ajili ya watu wenye albinism yanatengewa fedha na kununuliwa na kwamba vyote vitakuwa bure! Ahadi hii ameitoa leo huko Arusha katika sherehe ya siku ya kimataifa albinism!

Hiki ni kituko kwani waziri wake wa afya hakuzungumzia cho chote kuhusu suala hilo wakati wa bajeti ya afya! Na kama JK atalazimisha kutekelezwa kwa ahadi basi ama bajeti ya wizara itavurugika au itakuwa ahadi mpya ambayo haitatekelezeka hadi anamaliza muda wake October mwaka huu!!

Cha kujiuliza hivi JK hakomi kuahidi ahadi hewa au haoni aibu kwa kutotekelezeka kwa ahadi lukuki alizowaahidi wananchi nchini kote mwaka 2010?!

Kwani kwenye bajeti hakuna fungu la madawa? si hilo hilo ndiyo atatenga za hao ndugu zetu.

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
 
Back
Top Bottom