Vituko haviishi

Kimbweka

JF-Expert Member
Jul 16, 2009
8,597
1,683
Kuna mambo yanashangaza sana na kukupelekea uwaze sana na hupati jibu

Ilikuwa hivi: Jamaa amempeleka mkewe hosp na ikabidi alazwe na vipimo vilionyesha kuwa ana upungufu wa damu. Hivyo ikabidi wacheki kama group ya mumewe inaendana na ya mkewe ili amchangie damu, kwa bahati siyo nzuri haikuendana, Katika hangaika akakutana na rafikie ambaye yeye alikuwa anajitambua ni group gani na itamfaa mkewe, cha msingi ni kupima ngoma kama hana aweze kutoa damu kwa ajili ya mke wa rafikie. Cha ajabu jamaa akakataa katakata kwamba hataki damu ya rafikie iingie kwa mkewe, hivyo aliendelea kutafuta mpaka akampata rafiki wa kike wa mkewe ndipo akatoa damu na kufanikisha kuwekewa mkewe

Sasa nimekuwa nikijiuliza huyu jamaa alihisi nini mpaka kukataa rafikie asimtolee damu mkewe mpaka akatafuta mwanamke rafiki wa mkewe
Nimekuwa nikijiuliza sipati jibu
Kama huyo jamaa yupo hapa JF anisamehe sana au kama ana jibu anipe
Bado nawaza.............
 
kweli vituko havitakaa viishe.......je kama ilikuwa imebaki dakika chache wife afe....angekataa jamaa asimwekee damu
 
kweli vituko havitakaa viishe.......je kama ilikuwa imebaki dakika chache wife afe....angekataa jamaa asimwekee damu

sijapata jibu na sijajua mpaka sasa huyu jamaa alihisi au fikiri nini?
 
Wivu tu unamsumbua huyo jamaa,naona alijua rafiki yake akitoa damu yake iko siku ataomba naye achangamshwe damu yake iliyobaki.
 
Kuna mambo yanashangaza sana na kukupelekea uwaze sana na hupati jibu

Ilikuwa hivi: Jamaa amempeleka mkewe hosp na ikabidi alazwe na vipimo vilionyesha kuwa ana upungufu wa damu. Hivyo ikabidi wacheki kama group ya mumewe inaendana na ya mkewe ili amchangie damu, kwa bahati siyo nzuri haikuendana, Katika hangaika akakutana na rafikie ambaye yeye alikuwa anajitambua ni group gani na itamfaa mkewe, cha msingi ni kupima ngoma kama hana aweze kutoa damu kwa ajili ya mke wa rafikie. Cha ajabu jamaa akakataa katakata kwamba hataki damu ya rafikie iingie kwa mkewe, hivyo aliendelea kutafuta mpaka akampata rafiki wa kike wa mkewe ndipo akatoa damu na kufanikisha kuwekewa mkewe


Sasa nimekuwa nikijiuliza huyu jamaa alihisi nini mpaka kukataa rafikie asimtolee damu mkewe mpaka akatafuta mwanamke rafiki wa mkewe
Nimekuwa nikijiuliza sipati jibu
Kama huyo jamaa yupo hapa JF anisamehe sana au kama ana jibu anipe
Bado nawaza.............

aliogopa kuwa angempa damu ingekuwa ndio nji ya huyo rafikiye kumpata mkewe...labda alishahisi kuwa mshikaji anammega mkewe ndio maana kakataa damu yake.
 
Ama kweli sikio/jicho halilali na njaa!
Kwanza huyo jamaa ni ujinga na ushamba tu vinamsumbua kwa sababu haina maana damu iliyogemwa saa hiyo ndio hiyohiyo inaenda kutundikwa kwa mkewe! Damu hiyo ingingia kwenye bank ya damu ili kuziba pengo na haiyumkini mke angewekewa ya mtu mwingine tu.
Vile vile, kama angekuwa na akili na uwezo wa kuwa na kibri cha wivu, basi wenziwe wanachofanya ni kujiwekea akiba zao ziweze kutumika itakapobidi!
 
Ama kweli sikio/jicho halilali na njaa!
Kwanza huyo jamaa ni ujinga na ushamba tu vinamsumbua kwa sababu haina maana damu iliyogemwa saa hiyo ndio hiyohiyo inaenda kutundikwa kwa mkewe! Damu hiyo ingingia kwenye bank ya damu ili kuziba pengo na haiyumkini mke angewekewa ya mtu mwingine tu.
Vile vile, kama angekuwa na akili na uwezo wa kuwa na kibri cha wivu, basi wenziwe wanachofanya ni kujiwekea akiba zao ziweze kutumika itakapobidi!

Hili pia nafikiri hakulijua
 
Hehe, huyo alidhani kuwa damu in sumaku hivyo damu ya mkewe na ya jamaa zitavutana na matokeo yake wata-du....
 
Kuna mambo yanashangaza sana na kukupelekea uwaze sana na hupati jibu

Ilikuwa hivi: Jamaa amempeleka mkewe hosp na ikabidi alazwe na vipimo vilionyesha kuwa ana upungufu wa damu. Hivyo ikabidi wacheki kama group ya mumewe inaendana na ya mkewe ili amchangie damu, kwa bahati siyo nzuri haikuendana, Katika hangaika akakutana na rafikie ambaye yeye alikuwa anajitambua ni group gani na itamfaa mkewe, cha msingi ni kupima ngoma kama hana aweze kutoa damu kwa ajili ya mke wa rafikie. Cha ajabu jamaa akakataa katakata kwamba hataki damu ya rafikie iingie kwa mkewe, hivyo aliendelea kutafuta mpaka akampata rafiki wa kike wa mkewe ndipo akatoa damu na kufanikisha kuwekewa mkewe

Sasa nimekuwa nikijiuliza huyu jamaa alihisi nini mpaka kukataa rafikie asimtolee damu mkewe mpaka akatafuta mwanamke rafiki wa mkewe
Nimekuwa nikijiuliza sipati jibu
Kama huyo jamaa yupo hapa JF anisamehe sana au kama ana jibu anipe
Bado nawaza.............

Hiyo nimeipenda!
Jamaa alikuwaright na aliona mbali wanawake wengi wao niwepesi wa kulipa fadhira so yangeweza kujitokeza mengine km jamaa angeaccept zawadi toka kwa shemejiye na nauhakika shemeji mtu angeombwa TUNDI bila shaka angesaula si unajua tena wanawake huruma yao huwa njenje hata km ni risk!
 
Shemeji ahsante sana kwa kunichangai damu nilipokuwa na upungufu damu. Nakushukuru sana. Ahsante sana shemeji ukishapata nafuu basi tutaongea zaidi kuhusu hili kusanya nguvu kwanza.

Njemba ilikuwa na wasiwasi labda rafiki amekuwa akimsifiasifia shemeji yake kwa uzuri mara nyingi tu hivyo akahofia kwamba anaweza kulitumia hili la kumchangia damu ili ajisogeze karibu naye zaidi. Marafiki wengine ndivyo walivyo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom