TheChoji
JF-Expert Member
- Apr 14, 2009
- 4,974
- 15,310
Wengi hua tunadhani muvi za bongo tu ndio zina vitu vya hovyo. Kiukweli muvi za kizungu pia zina maujinga mengi yasiyo na uhalisia. Hivi ni kati ya vitu vya uongo na vinavyokera hasa kwenye muvi za kizugu.
1. Bunduki kutokuisha risasi. Ushawahi ona kwenye muvi mtu ana ki bastola au SMG anamwaga risasi lisaa lizima na haziishi? Uongo mtupu.
2. Watu kupigana juu ya treni huku inatembea! Hiki ni kitu cha hovyo kabisa hata kukiwaza tu. Hata kupigana juu ya treni iliyosimama ni shughuli pevu achilia mbali inayotembea.
3. Bomu la kutegwa kupiga alarm kabla ya kulipuka. Wanajeshi wanaingia kwenye nyumba, hawajui kama kuna bomu. Mara wanasikia mlio pi pi pi pi pipipipipipi...Booom! 😆 saa hiyo wanakua wameshatoka nje.
4. Watu wema kushinda. Katika muvi karibu nyingi, wale watu wema hua wanashinda na watu wabaya wanauawa. Hii haina uhalisia wowote kwenye maisha ya kawaida.
5. Kuwasha gari kwa kuchomoa nyaya chini ya usukani na kuzigusanisha. Japo hii inawezekana, lakini ni ngumu mno kutekelezeka kiuhalisia. Hata fundi mwenye vifaa, inakuchukua muda mrefu sana kufanikisha hili.
6. Maadui kuweka bunduki chini ili wapigane ngumi 😂
Hebu na wewe ongezea vitu vya kijinga ulivyowahi kuona kwenye movie
1. Bunduki kutokuisha risasi. Ushawahi ona kwenye muvi mtu ana ki bastola au SMG anamwaga risasi lisaa lizima na haziishi? Uongo mtupu.
2. Watu kupigana juu ya treni huku inatembea! Hiki ni kitu cha hovyo kabisa hata kukiwaza tu. Hata kupigana juu ya treni iliyosimama ni shughuli pevu achilia mbali inayotembea.
3. Bomu la kutegwa kupiga alarm kabla ya kulipuka. Wanajeshi wanaingia kwenye nyumba, hawajui kama kuna bomu. Mara wanasikia mlio pi pi pi pi pipipipipipi...Booom! 😆 saa hiyo wanakua wameshatoka nje.
4. Watu wema kushinda. Katika muvi karibu nyingi, wale watu wema hua wanashinda na watu wabaya wanauawa. Hii haina uhalisia wowote kwenye maisha ya kawaida.
5. Kuwasha gari kwa kuchomoa nyaya chini ya usukani na kuzigusanisha. Japo hii inawezekana, lakini ni ngumu mno kutekelezeka kiuhalisia. Hata fundi mwenye vifaa, inakuchukua muda mrefu sana kufanikisha hili.
6. Maadui kuweka bunduki chini ili wapigane ngumi 😂
Hebu na wewe ongezea vitu vya kijinga ulivyowahi kuona kwenye movie