Vitu vya Kufanya Katika Maisha Yako Kabla ya Kupata Ujauzito

karv

JF-Expert Member
Dec 26, 2019
1,799
3,221
Haya ni mambo ya muhimu ya kuzingtia kabla kujaribu kupata ujauzito.

1)Acha maadili mabaya.

Uvutaji wa sigara na unywaji wa pombe wa kupitiliza vyote uweza kusababisha kuharibika kwa ujauzito na matatizo ya kiafya kwa mwanao atakapozaliwa. Cha msingi kujua ni muhimu kumtunza mtoto vizuri na kuachana na vitu hivi,ikiwemo pia matumizi ya kahawa kupitiliza.

2)Badilisha ulaji wako kuwa bora.

Kuanzia muda unapata ujauzito ukuaji wa mwanao unahitaji ulaji wa chakula bora kuweza ili kumtunza vyema mtoto wako, hivyo ili mwili wako uweze kujenga lishe bora kwa ukuaji wa mtoto ni jambo la busara kula lishe bora.

Kuwa na uzito uliozidi au uliopunguwa unaweza kufanya uwe na wakati mgumu kuweza kupata mtoto ambayo pia inaweza kuleta matatizo ya kiafya kwako na kwa mtoto. Kuzingatia lishe bora unaweza kuwa na BMI nzuri kwa ajili yako na mtoto. Unatakiwa pia uanze kutumia foliki asidi (mcg 400) kila siku kabla hujapata ujauzito.

3)Anza kufanya mazoezi mara kwa mara

Ni muhimu ukianza kufanya mazoezi mara kwa mara ambayo yatakupa nguvu zaidi, kuwa imara kutakusaidia kupata ujauzito wenye nguvu. Na pia utakupa nafasi ya kujifungua njia ya kawaida. Mazoezi ni njia ya muhimu kupata uzito bora.

4)Pumzika

Mazoezi mengi yanaweza yasiwe mazuri sana kwa afya ya uzazi, kupumzika sana kunaweza kukupa nafasi nzuri ya kujifungua na hata kupata ujauzito.

Kama unaweza kujitoa japo lisaa limoja kila siku kila wiki kuondoa mawazo kichwani na shinikizo la damu. Unaweza pia kufanya yoga. Hakikisha unajiandaa kwa kuanza kuweka akiba ya hela sasa.

5)Angalia uchumi wako

Kuwa na mtoto ni gharama! Tambua ni namna gani na kiasi gani gharama ya mtoto itakuathiri katika wiki ya kwanza na miezi ya kwanza. Hakikisha umejiandaa kwa kuanza kuweka akiba sasa.

6)Zungumza maswala ya uzazi na mwenzi wako.

Kuwa mzazi ni jambo zuri na ni gumu pia. Wewe na mwenza wako lazima mjiandae kwa ukweli kwamba maisha yenu yatabadilika sana. Zungumzeni kuhusu woga wenu na ndugu na marafiki. Kama utaona tatizo popote kati yako na mwenza wako na ni gumu kutatua, jaribuni kuwa na msululishi. Ni vyema kufanya mambo yakawa mazuri sasa, wakati kichanga kikiwa njiani. Mwisho usisahau kuongelea mambo mazuri pia,nini kinakufurahisha na kwa kiwango gani malengo yako yamefanikiwa.
mimba-800x500.jpg


Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom