Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Unaweza kufikiria vitu vitatu au vinne ambavyo kwa kweli kwenye mahusiano watu wanakubali kuishi navyo lakini kwa kweli vinakera sana. NI vitu ambavyo unatamani mwenzako angeweza kuvibadilisha lakini baada ya muda umeamua kukubali kuwa huo "ndio" mzigo wako. Umejifunza kuishi navyo lakini kwa kweli ungeweza kuishi bila kuwa navyo. Kwa mfano watu wengine wanakereka na vitu kama kukoroma, kuimba imba, kulala mapema, kuzungumza usiku wa manane na maswali yanayoanza na "nikuulize swali" n.k Hivi siyo vitu vinavyohusiana na watu wengine (siyo mambo ya kucheat n.k) bali vijitabia, mazoea, mambo na hata vijimambo ambavyo ni "kero" kama zile "kero za Muungano".
Hapa tunaweza kufundishana maana wengine kuna vitu ambavyo hawajali kabisa na wala hawafikirii kuwa ni "kero"...
Hapa tunaweza kufundishana maana wengine kuna vitu ambavyo hawajali kabisa na wala hawafikirii kuwa ni "kero"...