Vitu gani hutavisahau kwa mwaka huu 2016 vilivovuma

Ushindi wa Leicester city
El-chapo kukamatwa tena.
Khan kuwa Mayor wa London.
Venezuela na mporomoko wa uchumi
 
Binafsi ni inshu ya faru, vifo vya viongozi, vifo vya wachezaji wa mpira brazili, kupata Mungu mtu Tz, wewe je?




KWELI KWELI NITAKUMBUKA:
1. Kwanza uchaguzi iliofanyika ambaye hakutegemewa akapata URAIS (Mh. Magufuli, Trump)
2. Nitakumbuka watu mwanzo walivyokuwa wakimshangilia Mh. Rais kwa kutumbua majipu na sasa kumgeuka sababu ya kuona kumbe kisu kinakata kote kote...kwani mwanzo walikuwa wanashabikia wengine kutumbuliwa wakifikiri wao haitawafika...

3. Nitakumbuka Jinisi baadhi ya watanzania walipopokea wakati mgumu kwa kukataa kukubali kukweli, na kukubali mfumo mpya wa maisha...Kuanza kuishi maisha ya kimalaika kwani walishazoea maisha ya kishetani...mfano RUSHWA, UFISADI, hawakuwa wamezoea KUPATA HELA KIHALALI...hivyo hii kupelekea kuwa na wakati mgumu sana. Ni sawa na Kijana K. K. K aliyezoea kuwategemea wazazi mara wazazi Mungu akawachukua ghafla...hivyo inakuwa ngumu sana kuzoea hali.

3. Nitakumbuka Mh. Rais kwa mwaka wa kwanza alivyokuwa anajitahidi kusafisha kwanza binadamu wa nchi yake na kupelekea kuchelewa kuanza kujenga nchi...Nchi ilikuwa imechafuka..

4. Nitakumbuka Binadamu wa Jamii forum pia kwa upande mwingine walivyomchangia Mh. Rais kutoa taarifa hivyo kupelekea kuwa rahisi kutumbua majipu.

Mengine baadae.........
 
Back
Top Bottom